Ayubu 27
1 Ndipo Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 “Hakika kama Mungu aishivyo, aliyeninyima haki yangu, Mwenyezi ambaye amenifanya nionje uchungu wa nafsi,
3 kwa muda wote nitakaokuwa na uhai ndani yangu, nayo pumzi ya Mungu ikiwa puani mwangu,
4 midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5 Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6 Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7 “Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
8 Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
9 Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
10 Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
11 “Nitawafundisha kuhusu uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
12 Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
13 “Hili ndilo fungu ambalo Mungu humpa mtu mwovu, urithi ule mtu mdhalimu anapokea kutoka kwa Mwenyezi:
14 Hata watoto wake wawe wengi kiasi gani, fungu lao ni kuuawa kwa upanga; wazao wake hawatakuwa kamwe na chakula cha kuwatosha.
15 Tauni itawazika wale watakaonusurika miongoni mwao, nao wajane wao hawatawaombolezea.
16 Ajapokusanya fedha nyingi kama mavumbi, na mavazi kama malundo ya udongo wa mfinyanzi,
17 yale yote mtu mwovu aliyojiwekea akiba, mwenye haki atayavaa, naye asiye na hatia ataigawanya fedha yake.
18 Nyumba aijengayo ni kama utando wa buibui, kama kibanda alichotengeneza mlinzi.
19 Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.
20 Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.
21 Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.
22 Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.
23 Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.”
Querverweise
156
- 1Job 29:1, Num 23:7, Num 24:15, Num 24:3, Psa 78:2, Pro 26:7, Psa 49:4
- 2Job 34:5, Num 14:21, 2Ki 4:27, Isa 40:27, 1Sa 25:34, Ezk 33:11, Job 9:18, Rut 1:20–21
- 3Gen 2:7, Job 33:4, Job 32:8, Isa 2:22, Act 17:25
- 4Job 13:7, Jhn 8:55, Job 34:6, 2Co 11:10, Job 6:28
- 5Job 2:9, Job 13:15, Pro 17:15, Job 42:7, Job 29:14, Deu 25:1, Job 32:3, Gal 2:11
- 6Job 2:3, 1Jn 3:20–21, Act 24:16, 2Co 12:11, Pro 4:13, Psa 18:20–23
- 7Dan 4:19, 2Sa 18:32, 1Sa 25:26
- 8Mat 16:26, Job 8:13, Luk 12:20–21, Job 11:20, Job 31:3, Job 20:5, Job 15:34, Mat 23:13
- 9Jer 14:12, Pro 1:28, Isa 1:15, Psa 18:41, Job 35:12–13, Mic 3:4, Hos 7:14, Pro 28:9
- 10Job 22:26–27, Psa 37:4, Hab 3:18, 1Th 5:17, Act 10:2, Luk 18:1, Eph 6:18, Psa 78:34–36
- 11Psa 71:17, Isa 8:11, Job 4:3–4, Job 6:10, Deu 4:5, Act 20:20, Job 32:8–10
- 12Job 16:3, Job 21:3, Job 19:2–3, Ecc 8:14, Job 26:2–4, Job 6:25–29, Job 17:2, Job 21:28–30
- 13Job 20:19–29, 2Pe 2:9, Job 15:20–35, Isa 3:11, Pro 22:22–23, Jas 5:4–6, Psa 11:6, Mal 3:5
- 14Deu 28:41, Job 20:10, Luk 23:29, 2Ki 9:7–8, 1Sa 2:5, Est 9:5–10, Job 15:22, Hos 9:13–14
- 15Psa 78:64, Jer 22:18, 1Ki 14:10–11, 1Ki 16:3–4, 1Ki 21:21–24
- 16Zec 9:3, Mat 6:19, Jas 5:2, 1Ki 10:27, Job 22:24, Hab 2:6
- 17Pro 13:22, Pro 28:8, Ecc 2:26
- 18Job 8:14–15, Isa 1:8, Isa 51:8, Isa 38:12, Lam 2:6
- 19Job 24:24, Psa 58:9, Jer 8:2, Psa 73:19–20, Job 21:23–26, Job 7:8, Job 30:23, Job 14:12–15
- 20Job 15:21, Job 18:11, Job 21:18, Job 20:23, 2Ki 19:35, Exo 12:29, Psa 69:14–15, Psa 18:4
- 21Psa 11:6, Psa 83:15, Psa 58:9, Job 21:18, Job 7:10, Mat 7:27, Jer 18:17, Exo 9:23–25
- 222Pe 2:4–5, Ezk 5:11, Job 11:20, Ezk 24:14, Rom 8:32, Jos 10:11, Jer 13:14, Ezk 9:5–6
- 23Lam 2:15, 1Ki 9:8, Jer 19:8, Zep 2:15, Est 9:22–25, Rev 18:20, Job 18:18, Mic 6:16