Ayubu 14
1 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 “Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 Kama vile maji yanavyotoweka katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka usingizi wao.
13 “Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka!
14 Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 Makosa yangu yatatiwa muhuri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 “Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wazao wake wakidharauliwa, yeye haoni.
22 Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”
Querverweise
145
- 1Job 5:7, Ecc 2:23, Job 25:4, Mat 11:11, Job 7:1, Job 9:25, Job 7:6, Job 15:14
- 2Isa 40:6–8, 1Pe 1:24, Job 8:9, Psa 103:15–16, 1Ch 29:15, Jas 4:14, Jas 1:10–11, Psa 144:4
- 3Psa 144:3, Psa 143:2, Psa 8:4, Job 9:19–20, Job 13:27, Rom 3:19, Job 7:17–18, Job 13:25
- 4Jhn 3:6, Job 15:14, Eph 2:3, Rom 8:8–9, Psa 51:5, Luk 1:35, Job 25:4–6, Rom 5:12
- 5Psa 39:4, Act 17:26, Job 12:10, Heb 9:27, Psa 104:29, Dan 5:26, Job 21:21, Luk 12:20
- 6Job 7:19, Psa 39:13, Job 7:1–2, Job 10:20, Job 7:16, Mat 20:1–8
- 7Isa 27:6, Isa 11:1, Job 14:14, Dan 4:23–25, Job 19:10, Dan 4:15
- 81Co 15:36, Isa 26:19, Jhn 12:24
- 9Rom 11:17–24, Ezk 17:22–24, Ezk 19:10, Ezk 17:3–10
- 10Job 19:26, Job 7:7–10, Pro 14:32, Gen 49:33, Luk 16:22–23, Mat 27:50, Job 11:20, Job 14:12
- 11Isa 19:5, Jer 15:18, Job 6:15–18
- 12Job 10:21–22, Isa 26:19, Job 3:13, Ecc 3:19–21, 2Pe 3:10–13, Job 30:23, 2Pe 3:7, Job 7:21
- 13Mrk 13:32, Isa 26:20–21, Isa 57:1–2, Act 17:31, Psa 106:4, Gen 8:1, Luk 23:42, Act 1:7
- 141Co 15:51–52, Psa 27:14, Job 7:1, Act 26:8, Php 3:21, Rev 20:13, Job 14:5, Jhn 5:28–29
- 15Psa 138:8, Job 13:22, 1Pe 4:19, Job 10:3, Job 10:8, Job 7:21, 1Jn 2:28, 1Th 4:17
- 16Job 10:6, Job 31:4, Job 34:21, Psa 139:1–4, Pro 5:21, Job 33:11, Jer 32:19, Job 13:27
- 17Deu 32:34, Hos 13:12, Job 21:19
- 18Rev 6:14, Job 18:4, Jer 4:24, Rev 8:8, Isa 41:15–16, Rev 20:11, Mat 27:51, Isa 64:1
- 19Job 27:8, Job 7:6, Job 19:10, Luk 12:19–20, Gen 6:17, Psa 30:6–7, Gen 7:21–23, Ezk 37:11
- 20Job 2:12, Job 14:14, Ecc 8:8, Lam 4:8
- 21Ecc 9:5, Isa 63:16, Ecc 2:18–19, 1Sa 4:20, Psa 39:6, Isa 39:7–8
- 22Job 19:26, Luk 16:23–24, Job 19:20, Pro 14:32, Job 19:22, Job 33:19–21