Ayubu 11
1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2 “Je, maneno haya yote yapite bila kujibiwa? Je, huyu mnenaji athibitishwe kuwa na haki?
3 Je, maneno yako ya upuzi yawafanye watu wanyamaze kimya? Je, mtu asikukemee unapofanya dhihaka?
4 Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
5 Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
6 naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.
7 “Je, unaweza kujua siri za Mungu? Je, unaweza kuyachunguza mambo yote kumhusu Mwenyezi?
8 Ni juu mno kuliko mbingu: unaweza kufanya nini? Kina chake ni kirefu kuliko Kuzimu: wewe unaweza kujua nini?
9 Kipimo chake ni kirefu kuliko dunia, nacho ni kipana kuliko bahari.
10 “Akija na kukufunga gerezani, na kuitisha mahakama, ni nani awezaye kumpinga?
11 Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?
12 Mpumbavu aweza kuwa mwenye hekima, endapo mtoto wa punda-mwitu atazaliwa mwanadamu.
13 “Hata sasa ukiutoa moyo wako kwake na kumwinulia mikono yako,
14 ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako, wala usiuruhusu uovu ukae kwenye hema lako,
15 ndipo utainua uso wako bila aibu; utasimama imara bila hofu.
16 Hakika utaisahau taabu yako, utaikumbuka tu kama maji yaliyokwisha kupita.
17 Maisha yako yatang’aa kuliko adhuhuri, nalo giza litakuwa kama alfajiri.
18 Utakuwa salama, kwa kuwa lipo tumaini; utatazama pande zote na kupumzika kwa salama.
19 Utalala, wala hakuna atakayekuogofya, naam, wengi watajipendekeza kwako.
20 Bali macho ya waovu hayataona, wokovu utawaepuka; tarajio lao litakuwa ni hangaiko la mtu anayekata roho.”
Querverweise
147
- 1Job 2:11, Job 20:1
- 2Jas 1:19, Job 18:2, Pro 10:19, Act 17:18, Psa 140:11, Job 8:2, Job 16:3
- 3Job 17:2, Job 12:4, Job 24:25, Jud 1:18, Job 34:7, Psa 35:16, Psa 83:16, Job 13:9
- 4Job 10:7, Job 6:10, Job 7:20, Job 9:2–3, Job 6:29–30, 1Pe 3:15, Job 35:2, Job 34:5–6
- 5Job 38:1–2, Job 31:35, Job 33:6–18, Job 40:8, Job 40:1–5, Job 23:3–7, Job 42:7
- 6Ezr 9:13, Lam 3:22, Mat 13:35, Dan 2:28, Eph 3:5, Job 15:8, Job 9:4, Dan 2:47
- 7Rom 11:33, Ecc 3:11, Psa 145:3, Psa 77:19, Job 37:23, Isa 40:28, Eph 3:8, Job 5:9
- 8Job 22:12, Isa 55:9, Psa 139:6–8, Job 35:5, Psa 148:13, Amo 9:2, Job 26:6, Eph 3:18–19
- 9Psa 139:9–10, Psa 65:5–8, Job 28:24–25
- 10Job 9:12–13, Job 12:14, Rev 3:7, Isa 41:27, Dan 4:35, Job 38:8, Job 34:29, Job 9:4
- 11Heb 4:13, Psa 10:14, Rev 2:23, Jhn 2:24–25, Hab 1:13, Hos 7:2, Psa 10:11, Jer 17:9–10
- 12Job 39:5–8, Jas 2:20, Ecc 3:18, Psa 73:22, Jer 2:24, Jas 3:13–17, 1Co 3:18–20, Job 15:14
- 13Psa 143:6, Psa 88:9, 1Sa 7:3, Psa 78:8, Job 8:5–6, Luk 12:47, 2Ch 12:14, Job 22:21–22
- 14Job 22:23, Job 4:7, Jas 4:8, Zec 5:3–4, Psa 101:2, Job 22:5, Isa 1:15, Job 34:32
- 15Job 22:26, 1Jn 2:28, 1Jn 3:19–22, 1Ti 2:8, Psa 119:6–7, Pro 14:26, Pro 28:1, Psa 112:6–8
- 16Isa 65:16, Ecc 5:20, Jhn 16:21, Isa 54:9, Isa 54:4, Isa 12:1–2, Gen 41:51, Rev 7:14–17
- 17Isa 58:8–10, Psa 37:6, Pro 4:18, Zec 14:6–7, Mic 7:8–9, Hos 6:3, Psa 112:4, Job 42:11–17
- 18Pro 3:24–26, Psa 43:5, Psa 3:5, Psa 4:8, Lev 26:5–6, Rom 5:3–5, Pro 14:32, Job 7:6
- 19Isa 60:14, Psa 45:12, Lev 26:6, Isa 45:14, Pro 19:6, Job 42:8–9, Rev 3:9, Gen 26:26–31
- 20Deu 28:65, Job 17:5, Job 31:16, Job 27:8, Pro 10:24, Amo 5:19–20, Pro 20:20, Amo 2:14