Ayubu 17
1 Moyo wangu umevunjika, siku zangu zimefupishwa, kaburi linaningojea.
2 Hakika wenye mizaha wamenizunguka; macho yangu yamebaki kutazama uadui wao.
3 “Ee Mungu, nipe dhamana unayodai. Ni nani mwingine atakayeweka dhamana kwa ajili yangu?
4 Umezifunga akili zao zisipate ufahamu, kwa hiyo hutawaacha wapate ushindi.
5 Kama mtu akiwashutumu rafiki zake ili apate ujira, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
6 “Mungu amenifanya kitu cha dhihaka kwa kila mtu, mtu ambaye watu humtemea mate usoni.
7 Macho yangu yamefifia kwa ajili ya majonzi; umbile langu lote ni kama kivuli.
8 Watu wanyofu wanatishwa na hili; watu wasio na hatia wanasimama dhidi ya wasiomcha Mungu.
9 Hata hivyo, waadilifu watazishika njia zao, nao wale wenye mikono safi wataendelea kupata nguvu.
10 “Lakini ninyi njooni, ninyi nyote, jaribuni tena! Sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu.
11 Siku zangu zimepita, mipango yangu imevunjika, vivyo hivyo shauku za moyo wangu.
12 Watu hawa hufanya usiku kuwa mchana, kwenye giza wao husema, ‘Mwanga u karibu.’
13 Kama nyumba pekee ninayoitarajia ni kaburi, nikikitandika kitanda changu gizani,
14 nikiuambia uharibifu, ‘Wewe u baba yangu,’ na kuliambia buu, ‘Wewe u mama yangu’ au ‘Dada yangu,’
15 liko wapi basi tarajio langu? Ni nani awezaye kuona tarajio lolote kwa ajili yangu?
16 Je, litashuka chini hadi kwenye malango ya mauti? Je, tutashuka pamoja mavumbini?”
Querverweise
115
- 1Isa 38:10–14, Psa 88:3–5, Job 42:16, Isa 57:16, Job 17:13–14, Job 19:17, Job 6:11
- 2Job 16:20, Job 12:4, 1Sa 1:6–7, Mat 27:39–44, Job 21:3, Job 13:9, Psa 35:14–16, Psa 25:13
- 3Heb 7:22, Isa 38:14, Pro 11:15, Psa 119:122, Gen 44:32, Gen 43:9, Pro 22:26, Job 9:33
- 4Mat 11:25, Mat 13:11, 2Sa 17:14, 1Co 1:20, Rom 11:8, Isa 19:14, 2Ch 25:16, 2Sa 15:31
- 5Psa 12:2–3, Pro 29:5, Pro 20:19, Job 32:21–22, Exo 20:5, 1Ki 11:12, Job 11:20, Deu 28:65
- 6Psa 44:14, Job 30:9, 1Ki 9:7, Gen 31:27, Isa 5:12
- 7Psa 6:7, Job 16:16, Psa 31:9–10, Job 16:8, Psa 109:23, Ecc 6:12, Lam 5:17
- 8Ecc 5:8, Hab 1:13, Act 13:46, Job 22:19, Rom 11:33, Psa 73:12–15, Job 34:30
- 9Pro 4:18, Isa 1:15–16, Job 22:30, 2Co 12:9–10, Pro 14:16, Psa 84:7, Gen 20:5, Isa 40:29–31
- 10Job 42:7, Job 6:29, Job 15:9, 1Co 6:5, Job 32:9, Mal 3:18, Job 17:4, Job 12:2
- 11Job 7:6, Isa 38:10, Pro 16:9, Isa 8:10, Jas 4:13–15, Lam 3:37, 2Co 1:15–17, Job 9:25–26
- 12Job 7:3–4, Job 7:13–14, Deu 28:67, Job 24:14–16
- 13Job 10:21–22, Psa 139:8, Job 3:13, Lam 3:25–26, Psa 27:14, Job 17:1, Job 30:23, Isa 57:2
- 14Psa 16:10, Job 30:30, Job 24:20, 1Co 15:53–54, 1Co 15:42, Act 13:34–37, Isa 14:11, Job 21:26
- 15Job 13:15, Job 6:11, Job 4:6, Job 19:10, Job 7:6
- 16Job 3:17–19, Jon 2:6, 2Co 1:9, Ezk 37:11, Psa 88:4–8, Job 33:18–28, Job 18:13–14, Isa 38:17–18