Ayubu 20
1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2 “Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu, kwa sababu nimehangaika sana.
3 Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima, nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.
4 “Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
5 macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
6 Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
7 ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
8 Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
10 Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyang’anya watu.
11 Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
12 “Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
13 ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
14 Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.
15 Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.
16 Atanyonya sumu za majoka; meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.
17 Hatafurahia vijito, mito inayotiririsha asali na siagi.
18 Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila; hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.
19 Kwa kuwa aliwadhulumu maskini na kuwaacha bila kitu; amenyang’anya kwa nguvu nyumba asizozijenga.
20 “Hakika hatakuwa na amani katika kutamani kwake; hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.
21 Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale; kufanikiwa kwake hakutadumu.
22 Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.
23 Atakapokuwa amelijaza tumbo lake, Mungu ataionesha ghadhabu kali dhidi yake, na kumnyeshea mapigo juu yake.
24 Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma, mshale wa shaba utamchoma.
25 Atauchomoa katika mgongo wake, ncha inayong’aa kutoka ini lake. Vitisho vitakuja juu yake;
26 giza nene linavizia hazina zake. Moto usiopepewa na mtu utamteketeza, na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.
27 Mbingu zitaweka wazi hatia yake, nayo nchi itainuka kinyume chake.
28 Mafuriko yataichukua nyumba yake, maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
29 Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu, urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”
Querverweise
195
- 1Job 2:11, Job 42:9, Job 11:1
- 2Pro 14:29, Psa 31:22, Pro 29:20, Psa 116:11, Ecc 7:9, Mrk 6:25, Psa 39:2–3, Jer 20:9
- 3Job 33:3, Job 20:2, Job 19:3, Job 27:11, Job 19:29, Psa 78:2–5, Psa 49:3
- 4Job 8:8–9, Job 15:10, Gen 1:28, Gen 9:1–3, Job 32:7, Psa 115:16
- 5Psa 37:35–36, Job 18:5–6, Job 5:3, Psa 73:18–20, Job 27:8, Act 12:22–23, Job 8:12–13, Mat 13:20–21
- 6Isa 14:13–14, Oba 1:3–4, Gen 11:4, Mat 11:23, Amo 9:2, Dan 4:22, Dan 4:11
- 7Psa 83:10, Job 7:10, 2Ki 9:37, Job 4:20, Job 14:10, 1Ki 14:10, Job 8:18, Jer 8:2
- 8Psa 90:5, Psa 73:20, Job 18:18, Isa 29:7–8, Psa 18:10, Job 27:21–23
- 9Job 7:8, Job 7:10, Job 8:18, Psa 37:36, Psa 37:10, Job 20:7, Psa 103:15–16, Job 27:3
- 10Job 20:18, Luk 19:8, Job 27:16–17, Pro 28:3, Exo 9:2, Exo 22:3, Exo 22:1, Psa 109:10
- 11Job 13:26, Psa 25:7, Job 21:26, Ezk 32:27, Ezk 24:13, Jhn 8:24, Act 1:25, Pro 14:32
- 12Job 15:16, Psa 10:7, Ecc 11:9, Pro 9:17–18, Psa 109:17–18, Gen 3:6, Pro 20:17
- 13Mrk 9:43–49, Mat 5:29–30, Rom 8:13, Num 11:18–20
- 14Rom 3:13, Deu 32:24, Psa 51:8–9, 2Sa 11:2–5, Job 20:16, Psa 38:1–8, Mal 2:2, Pro 1:31
- 15Pro 23:8, Mat 27:3–4
- 16Rom 3:13, Act 28:3–6, Isa 30:6, Mat 3:7, Deu 32:24
- 17Deu 32:13–14, Luk 16:24, Job 29:6, Rev 22:1, Jer 17:6–8, Num 14:23, Isa 7:15, Isa 7:22
- 18Job 20:10, Pro 1:12, Jer 51:44, Job 20:15, Jer 22:13, Hos 8:7–8, Job 31:25, Jer 51:34
- 19Job 35:9, Pro 14:31, Jas 5:4, Jas 2:6, Pro 22:22–23, Ezk 22:29, Jas 2:13, Job 31:13–22
- 20Ecc 5:13–14, Isa 57:20–21
- 21Job 15:29, Jer 17:11, Job 18:19, Luk 16:24–25
- 22Rev 18:7, Job 15:29, Ecc 2:18–20, Job 18:7, Psa 39:5, Job 1:17, Job 1:15, Job 3:17
- 23Psa 78:30–31, Num 11:33, Gen 19:24, Luk 12:17–20, Isa 21:4, Exo 9:23, Mal 2:2, Psa 11:6
- 24Amo 5:19, Isa 24:18, 2Sa 22:35, Pro 7:23, Jer 48:43–44, Amo 9:1–3, 1Ki 20:30
- 25Job 18:11, Job 16:13, Job 15:21, Deu 32:41, Job 27:20, Psa 7:12, 2Co 5:11, Psa 73:19
- 26Psa 21:9, Psa 120:4, Jud 1:13, Mat 8:12, Job 18:18–19, Job 18:5–6, Isa 14:20–22, Isa 8:22
- 27Luk 12:2–3, Job 16:18, Isa 26:21, Psa 44:20–21, Jer 29:23, Rom 2:16, 1Co 4:5, Job 18:18
- 28Job 27:14–19, Zep 1:18, Jas 5:1–3, Rev 18:17, Job 20:10, Job 5:5, Pro 11:4, 2Ki 20:17
- 29Job 27:13, Job 31:2–3, Job 18:21, Psa 11:5–6, Mat 24:51, Lam 3:38, Deu 29:20–28
Themen in diesem Kapitel
29
Afflictions and Adversities, Ambition, Asp, Belly, Bow, Butter, Children, Covetousness, Creditor, Death, Debtor, Dream, Gall, Happiness, Hypocrisy, Iron, Job, Joy, Pleasure, Poor, Restitution, Serpent, Sin, Steel, Uncharitableness, Viper, Wicked (People), Worldliness, Zophar