Ayubu 18
1 Bildadi Mshuhi akajibu:
2 “Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya? Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.
3 Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama, na kuonekana wajinga machoni pako?
4 Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande katika hasira yako, je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe? Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?
5 “Taa ya mwovu imezimwa, nao mwali wa moto wake umezimika.
6 Mwanga kwenye hema lake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7 Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; hila zake mwenyewe zinamwangusha.
8 Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11 Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12 Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 Atang’olewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16 Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17 Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18 Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19 Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20 Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21 Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Querverweise
142
- 1Job 2:11, Job 8:1, Job 25:1, Job 42:7–9
- 2Job 13:5–6, Pro 18:13, Job 33:1, Job 11:2, Job 3:17, Job 21:2, Jas 1:19, Job 16:2–3
- 3Psa 73:22, Job 17:10, Job 17:4, Job 12:7–8, Rom 12:10, Ecc 3:18
- 4Job 14:18, Job 16:9, Job 13:14, Job 5:2, Isa 54:10, Mrk 9:18, Luk 9:39, Jon 4:9
- 5Pro 13:9, Pro 24:20, Pro 20:20, Job 21:17, Pro 4:19, Isa 50:11, Job 20:5
- 6Rev 18:23, Job 21:17, Psa 18:28
- 7Pro 4:12, Psa 33:10, Psa 18:36, Hos 10:6, Job 5:12–13, 1Co 3:19, Job 15:6, Pro 1:30–32
- 8Psa 9:15, Job 22:10, Psa 35:8, Est 3:9, 2Ti 2:26, Pro 29:6, Ezk 32:3, Est 7:10
- 9Job 1:17, Isa 8:14–15, Job 5:5, Job 1:15
- 10Rom 11:9, Psa 11:6, Ezk 12:13
- 11Job 15:21, Jer 6:25, Lev 26:36, Job 20:25, Jer 49:29, Jer 46:5, Pro 28:1, Psa 53:5
- 12Psa 7:12–14, 1Th 5:3, Psa 109:10, Isa 8:21, 1Sa 2:5, 2Pe 2:3, Psa 34:10, Job 15:23–24
- 13Gen 49:3, Job 17:16, Zec 14:12, Jon 2:6, Rev 6:8, Isa 14:30
- 14Pro 10:28, Pro 14:32, Job 41:34, Psa 112:10, Job 8:22, Heb 2:15, 1Co 15:55–56, Mat 7:26–27
- 15Psa 11:6, Isa 34:9–10, Deu 29:23, Job 18:12–13, Job 20:18–21, Jer 22:13, Rev 19:20, Hab 2:6–11
- 16Hos 9:16, Isa 5:24, Mal 4:1, Amo 2:9, Job 15:30, Job 29:19, Job 5:3–4
- 17Psa 34:16, Pro 10:7, Psa 109:13, Pro 2:22, Psa 83:4, Job 13:12
- 18Job 20:8, Job 10:22, Dan 5:21, Pro 14:32, Job 5:14, Dan 4:33, Jud 1:13, Job 11:14
- 19Jer 22:30, Isa 14:21–22, Job 8:4, Job 20:26–28, Isa 5:8–9, Psa 109:13, Job 27:14–15, Job 1:19
- 20Psa 37:13, Ezk 21:25, Jer 50:27, Jer 18:16, Deu 29:23–24, Psa 137:7, Luk 19:44, Oba 1:11–15
- 21Tit 1:16, Jer 9:3, 2Th 1:8, Jdg 2:10, Jer 10:25, 1Th 4:5, Job 21:14, Psa 79:6