Ayubu 26
1 Kisha Ayubu akajibu:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonesha!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji, na wale wanaoishi ndani yake.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa.
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huining’iniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnong’ono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Querverweise
96
- 2Job 4:3–4, Isa 35:3–4, Job 16:4–5, Psa 71:9, Job 6:25, 1Ki 18:27, Job 12:2, Isa 41:5–7
- 3Job 12:3, Act 20:20, Job 15:8–10, Psa 71:15–18, Psa 49:1–4, Job 33:33, Act 20:27, Job 17:10
- 41Ki 22:23–24, Ecc 12:7, Job 20:3, Job 32:18, 1Co 12:3, 1Jn 4:1–3, Rev 16:13–14
- 5Gen 6:4, Psa 88:10, Job 41:1–34, Ezk 29:3–5, Psa 104:25–26
- 6Pro 15:11, Psa 139:8, Heb 4:13, Job 28:22, Amo 9:2, Psa 139:11, Isa 14:9, Job 41:11
- 7Job 9:8, Psa 104:2–5, Isa 40:22, Isa 42:5, Psa 24:2, Pro 8:23–27, Gen 1:1–2, Isa 40:26
- 8Job 37:11–16, Pro 30:4, Jer 10:13, Isa 5:6, Job 38:9, Psa 18:10–11, Job 38:37, Psa 135:7
- 9Psa 97:2, Job 22:14, Exo 34:3, 1Ki 8:12, Exo 20:21, Exo 33:20–23, Hab 3:3–5, 1Ti 6:16
- 10Pro 8:29, Job 38:8–11, Jer 5:22, Psa 33:7, Gen 8:22, Psa 104:6–9, Isa 54:9–10
- 111Sa 2:8, Job 15:15, Hag 2:21, Psa 18:7, Heb 12:26–27, 2Pe 3:10, Rev 20:11
- 12Isa 51:15, Jer 31:35, Job 9:13, Isa 51:9, Psa 89:9–10, Job 12:13, Psa 74:13, Psa 93:3–4
- 13Isa 27:1, Psa 104:30, Psa 74:13–14, Gen 1:2, Psa 33:6–7, Rev 12:9
- 14Isa 40:26–29, Job 11:7–9, Psa 139:6, Rom 11:33, Psa 145:3, Job 36:29, 1Co 13:9–12, Job 4:12