Ayubu 23
1 Ndipo Ayubu akajibu:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni ya uchungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
3 Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4 Ningeleta kesi yangu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5 Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile angeniambia.
6 Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, hangenigandamiza.
7 Hapo mtu mwadilifu angeleta kesi yake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
8 “Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9 Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10 Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
11 Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
12 Sijaziacha amri zilizotoka mdomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
13 “Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
14 Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
15 Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
16 Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
17 Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.
Querverweise
113
- 2Job 10:1, Job 7:11, Psa 32:4, Job 6:2–3, Lam 3:19–20, Psa 77:2–9, Job 11:6
- 3Job 16:21, Job 13:3, Job 31:35–37, Heb 4:6, Jer 14:7, Isa 26:8, Job 40:1–5, 2Co 5:19–20
- 4Job 13:18, Dan 9:18–19, Num 14:13–19, Psa 43:1, Isa 43:26, Gen 18:25–32, Exo 32:12–13, Job 37:19
- 51Co 4:3–4, Job 10:2, Job 13:22–23, Job 42:2–6
- 6Job 13:21, Job 9:33–34, 2Co 12:9–10, Job 9:19, Isa 27:8, Ezk 20:33, Isa 27:4, Ezk 20:35
- 7Job 13:3, Isa 1:18, Rom 8:1, Jer 3:5, Job 9:15, Rom 3:19–22, Jer 12:1, Rom 8:33–34
- 8Job 9:11, Psa 10:1, 1Ti 6:16, Job 35:14, Isa 45:15, Psa 13:1–3
- 9Psa 89:46, Isa 8:17
- 10Jas 1:12, 1Pe 1:7, Jas 1:2–4, Psa 139:1–3, Psa 66:10, Zec 13:9, Pro 17:3, Psa 17:3
- 11Psa 44:18, 2Pe 2:20–22, Psa 125:5, Job 17:9, Rom 2:7, Psa 17:5, Psa 18:20–24, 2Co 1:12
- 12Jer 15:16, Psa 119:11, Psa 119:103, Jhn 4:34, Psa 19:9–10, Job 22:22, Jhn 4:32, Jhn 8:31
- 13Psa 115:3, Pro 19:21, Dan 4:35, Isa 46:10, Job 12:14, Ecc 3:14, Num 23:19–20, Psa 135:6
- 141Th 3:3, 1Th 5:9, Rom 11:33, Psa 77:19, Isa 40:27–28, Psa 97:2, 1Pe 2:8, Job 7:3
- 15Psa 119:120, Psa 77:3, Job 31:23, Job 23:3, Job 10:15, Hab 3:16
- 16Psa 22:14, Job 27:2, Psa 88:16, Deu 20:3, Isa 6:5, Isa 57:16, Rut 1:20, Jol 1:15
- 17Job 19:8, Isa 57:1, 2Ki 22:20, Job 6:9, Job 18:6, Job 18:18, Job 22:11, Job 15:22