Yohana 9
1 Isa alipokuwa akipita, akamwona mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
2 Wanafunzi wake wakamuuliza, “Mwalimu, ni nani aliyetenda dhambi; ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
3 Isa akawajibu, “Huyu mtu wala wazazi wake hawakutenda dhambi. Alizaliwa kipofu ili kazi za Mungu zidhihirishwe katika maisha yake.
4 Yanipasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana, kwa kuwa usiku waja ambapo hakuna mtu awezaye kufanya kazi.
5 Wakati niko ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
6 Baada ya kusema haya, akatema mate ardhini, akatengeneza tope kwa mate na kumpaka yule kipofu machoni.
7 Kisha akamwambia, “Nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu” (Siloamu maana yake ni Kutumwa). Ndipo yule kipofu akaenda, akanawa, naye akarudi akiwa anaona.
8 Majirani zake na wale wote waliokuwa wamemwona hapo awali akiombaomba wakaanza kuuliza, “Je, huyu si yule aliyekuwa akiketi akiombaomba?”
9 Wengine wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “Siye, bali anafanana naye.” Lakini yeye akawaambia, “Mimi ndiye.”
10 Wakamuuliza, “Basi macho yako yalifumbuliwaje?”
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Isa alitengeneza tope, akanipaka machoni mwangu, naye akaniambia, ‘Nenda ukanawe katika Bwawa la Siloamu,’ ndipo nikanawa nami nikapata kuona!”
12 Wale wakamuuliza, “Yeye huyo mtu yuko wapi?” Akawajibu, “Sijui.”
13 Wakamleta yule mtu aliyekuwa kipofu hapo awali kwa Mafarisayo.
14 Basi siku hiyo Isa alitengeneza tope na kuyafungua macho ya huyo mtu ilikuwa Sabato.
15 Mafarisayo nao wakaanza kumuuliza yule mtu alivyopata kuona. Naye akawaambia, “Alinipaka tope kwenye macho yangu, nikanawa na sasa ninaona.”
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Huyu mtu hatoki kwa Mungu, kwa sababu hashiki Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya miujiza kama hii?” Wakagawanyika.
17 Hivyo wakamwambia tena yule mtu aliyekuwa kipofu, “Wewe ndiwe uliyefumbuliwa macho. Wasemaje kuhusu mtu huyo?” Yeye akawajibu, “Yeye ni nabii.”
18 Wale Wayahudi hawakuamini ya kuwa mtu huyo alikuwa kipofu akapata kuona, hadi walipowaita wazazi wake.
19 Wakawauliza, “Je, huyu ni mtoto wenu, ambaye mnasema alizaliwa kipofu? Imekuwaje basi sasa anaona?”
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua ya kuwa huyu ni mtoto wetu na ya kuwa alizaliwa kipofu.
21 Lakini hatujui jinsi anavyoweza kuona sasa, wala hatujui ni nani aliyemfungua macho yake. Muulizeni; yeye ni mtu mzima na anaweza kujieleza mwenyewe.”
22 Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi, kwani walikuwa wamekubaliana kuwa mtu yeyote atakayemkiri Isa kuwa ndiye Al-Masihi atafukuzwa kutoka sinagogi.
23 Kwa hiyo wazazi wake wakasema, “Yeye ni mtu mzima. Muulizeni.”
24 Hivyo kwa mara ya pili wakamwita yule aliyekuwa kipofu, nao wakamwambia, “Mpe Mungu utukufu! Sisi tunafahamu kuwa mtu huyu aliyekuponya ni mwenye dhambi.”
25 Akawajibu, “Mimi sijui kama yeye ni mwenye dhambi. Lakini jambo moja ninalojua, nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”
26 Wakamuuliza, “Alikufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
27 Akawajibu, “Tayari nimekwisha kuwaambia, nanyi hamtaki kunisikiliza. Mbona mnataka kusikia tena? Je, ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake?”
28 Ndipo wakamtukana na kusema, “Wewe ndiwe mwanafunzi wake! Sisi ni wanafunzi wa Musa.
29 Tunajua kwamba Mungu alisema na Musa, lakini mtu huyu hatujui anakotoka.”
30 Yule mtu akawajibu, “Hili ni jambo la ajabu! Hamjui anakotoka, naye amenifungua macho yangu!
31 Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.
32 Tangu zamani hatujasikia kwamba mtu amemponya yeyote aliyezaliwa kipofu.
33 Kama huyu mtu hakutoka kwa Mungu, asingeweza kufanya lolote.”
34 Wakamjibu, “Wewe ulizaliwa katika dhambi kabisa, nawe unajaribu kutufundisha?” Wakamfukuza atoke nje.
35 Isa aliposikia kuwa wamemfukuza atoke nje yule mtu aliyemfumbua macho, alimkuta, akamuuliza, “Je, unamwamini Mwana wa Adamu?”
36 Yule mtu akamjibu, “Yeye ni nani, Bwana? Niambie ili nipate kumwamini.”
37 Isa akamjibu, “Umekwisha kumwona; naye anayezungumza nawe, ndiye.”
38 Yule mtu akasema, “Bwana, naamini.” Naye akamwabudu.
39 Isa akasema, “Nimekuja ulimwenguni humu kwa ajili ya kuhukumu, ili wale walio vipofu wapate kuona, nao wale wanaoona wawe vipofu.”
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa karibu naye wakamsikia na kumwambia, “Je, kweli sisi ni vipofu?”
41 Isa akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu kweli, msingekuwa na hatia ya dhambi, lakini kwa kuwa mnasema, ‘Tunaona,’ basi mna hatia.
ข้ออ้างอิงโยง
219
- 2Luk 13:2, Jhn 9:34, Act 28:4, Exo 20:5
- 3Jhn 11:4, Jhn 11:40, Ecc 9:1–2, Job 2:3–6, Mat 11:5, Act 4:21, Job 42:7, Job 1:8–12
- 4Jhn 12:35, Eph 5:16, Jhn 4:34, Ecc 9:10, Jhn 11:9–10, Gal 6:10, Jhn 17:4, Col 4:5
- 5Jhn 8:12, Jhn 12:46, Act 13:47, Jhn 1:4–9, Isa 42:6–7, Rev 21:23, Act 26:18, Eph 5:14
- 6Mrk 7:33, Mrk 8:23, Rev 3:18
- 7Isa 35:5, Jhn 11:37, Jhn 9:11, Isa 8:6, Psa 146:8, Act 26:18, Neh 3:15, Luk 13:4
- 81Sa 2:8, 1Sa 21:11, Luk 16:20–22, Act 3:2–11, Luk 18:35, Mrk 10:46, Rut 1:19
- 10Ecc 11:5, Mrk 4:27, Jhn 3:9, 1Co 15:35, Jhn 9:26, Jhn 9:21, Jhn 9:15
- 11Jhn 9:6–7, Jhn 9:27
- 12Exo 2:18–20, Jhn 5:11–13, Jhn 7:11
- 13Jhn 12:42, Jhn 11:46–47, Jhn 8:3–8, Jhn 11:57, Jhn 12:19
- 14Jhn 5:9, Mat 12:1–14, Luk 13:10–17, Jhn 7:21–23, Mrk 2:23–3:6, Luk 6:1–11, Jhn 5:16, Luk 14:1
- 15Jhn 9:26–27, Jhn 9:10–11
- 16Jhn 7:43, Jhn 10:19, Jhn 3:2, Jhn 7:12, Mat 12:2, Jhn 5:36, Jhn 9:30–33, Jhn 15:24
- 17Jhn 4:19, Jhn 6:14, Act 3:22–26, Act 2:22, Mat 21:11, Act 10:38, Luk 24:19
- 18Heb 3:15–19, Heb 4:11, Jhn 5:44, Luk 16:31, Isa 53:1, Gen 19:14, Isa 26:11, Jhn 9:22
- 19Act 4:14, Jhn 9:8–9, Act 3:10
- 22Jhn 7:13, Jhn 16:2, Luk 6:22, Jhn 12:42–43, Jhn 9:34, Isa 57:11, Gal 2:11–13, Jhn 7:45–52
- 23Jhn 9:21
- 24Jhn 9:16, Jos 7:19, Jhn 8:49, Psa 50:14–15, 2Co 5:21, Jhn 19:6, Jhn 8:46, Jhn 5:23
- 251Jn 5:10, Jhn 9:30, Jhn 5:11
- 27Luk 22:67
- 28Rom 2:17, 1Co 6:10, 1Co 4:12, Mat 27:39, Mat 5:11, Jhn 7:47–52, Act 6:11–14, Isa 51:7
- 29Jhn 8:14, Mal 4:4, Jhn 7:27, Mat 12:24, Psa 105:26, 1Ki 22:27, Num 12:2–7, 2Ki 9:11
- 30Psa 119:18, Jhn 12:37, Isa 29:18, Jhn 3:10, Isa 29:14, Mat 11:5, Luk 7:22, 2Co 4:6
- 31Pro 15:29, Isa 1:15, Pro 28:9, Mic 3:4, Psa 145:19, Pro 1:28–29, Zec 7:13, Psa 34:15–16
- 32Isa 64:4, Job 20:4, Luk 1:70, Rev 16:18
- 33Jhn 9:16, Jhn 3:2, Act 5:38–39
- 34Jhn 9:22, Jhn 9:2, Isa 66:5, Gen 19:9, Job 25:4, Psa 51:5, Luk 18:17, Luk 6:22
- 35Jhn 20:31, 1Jn 5:13, Rom 10:20, 1Jn 4:15, Jhn 10:36, Psa 27:10, Jhn 1:34, Act 9:20
- 36Rom 10:14, Jhn 1:38, Sng 5:9, Mat 11:3, Pro 30:3–4
- 37Jhn 4:26, Psa 25:8–9, Jhn 7:17, Jhn 14:21–23, Psa 25:14, Mat 11:25, Mat 13:11–12, Act 10:31–33
- 38Mat 14:33, Mat 28:9, Jhn 20:28, Psa 2:12, Rev 5:9–14, Mat 28:17, Luk 24:52, Psa 45:11
- 39Jhn 3:19, Jhn 12:46, Act 26:18, Jhn 8:12, 1Jn 2:11, Luk 4:18, Jhn 12:40–41, Luk 1:79
- 40Rev 3:17, Mat 15:12–14, Rom 2:19–22, Jhn 9:34, Jhn 7:47–52, Luk 11:39–54, Mat 23:16–28
- 41Isa 5:21, Jhn 15:22–24, Luk 18:14, 1Jn 1:8–10, Pro 26:12, Heb 10:26, Jer 2:35, Luk 12:47
Topics in this chapter
39
Afflictions and Adversities, Alms, Beggars, Bigotry, Blindness, Church, Clay, Confession, Contingencies, Converts, Cowardice, Death, Diligence, Faith, Heredity, Hypocrisy, Jesus, the Christ, Judgment, Light, Miracles, Night, Obedience, Opinion, Public, Persecution, Pool, Prayer, Rabbi, Responsibility, Righteous, Sabbath, Salvation, Self-Righteousness, Siloam, Sin, Synagogue, Testimony, Wicked (People), Wisdom, Zeal, Religious