Yohana 16
1 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
2 Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
3 Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
4 Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 “Sasa mimi ninaenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unaenda wapi?’
6 Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
7 Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; lakini nikienda nitamtuma kwenu.
8 Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;
10 kwa habari ya haki, kwa sababu ninaenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
12 “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
13 Atakapokuja huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonesha mambo yajayo.
14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.”
16 Isa akaendelea kusema, “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninaenda kwa Baba’?”
18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
19 Isa akatambua kuwa walitaka kumuuliza kuhusu hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
20 Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 Mwanamke anapokuwa na uchungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini baada ya mtoto kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha yake ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
22 Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
23 Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
24 Hadi sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
26 Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni; sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
29 Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
30 Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
31 Isa akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
32 Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani mwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
33 “Nimewaambia mambo haya ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”
ข้ออ้างอิงโยง
237
- 11Pe 2:8, Mat 13:21, Mat 26:31–33, Jhn 15:18–27, Mat 24:10, Jhn 16:4, Rom 14:21, Mat 13:57
- 2Jhn 9:22, Act 26:9–11, Rom 10:2–3, Mat 10:28, Act 22:3–4, Jhn 12:42, Rev 6:9, Act 22:19–23
- 3Jhn 15:21, Jhn 17:25, 2Th 2:10–12, Jhn 8:19, Jhn 8:55, 2Th 1:8, 1Jn 3:1, Jhn 17:3
- 4Jhn 14:29, Mrk 13:23, Jhn 17:12–13, Jhn 13:19, Mat 9:15, Act 9:16, Mat 24:25, 2Pe 1:14
- 5Jhn 13:36, Jhn 7:33, Jhn 16:28, Jhn 17:4, Eph 4:7–11, Heb 1:3, Jhn 16:10, Jhn 14:4–6
- 6Jhn 16:20–22, Luk 24:17, Jhn 20:11–15, Jhn 14:1, Jhn 14:27–28, Luk 22:45
- 7Jhn 14:26, Jhn 14:16–17, Jhn 15:26, Act 2:33, Luk 24:49, Act 1:4–5, Jhn 7:39, Rom 8:28
- 8Act 2:37, Jud 1:15, Zec 12:10, Act 16:29–30, 1Co 14:24, Jhn 8:9, Jhn 8:46
- 9Jhn 15:22–25, Jhn 12:47–48, Jhn 8:23–24, Heb 3:12, Mrk 16:16, Act 2:22–38, Jhn 8:42–47, Act 3:14–19
- 102Co 5:21, 1Pe 3:18, Rom 10:3–4, Act 3:14, Jer 23:5–6, Php 3:7–9, 1Ti 3:16, 1Co 1:30
- 11Jhn 12:31, 1Jn 3:8, Heb 2:14, Col 2:15, Jhn 14:30, 2Co 4:4, Rev 12:7–10, Rev 20:10–15
- 12Mrk 4:33, Jhn 15:15, 1Co 3:1–2, Act 1:3, Heb 5:11–14, Jhn 14:30
- 13Jhn 14:26, 1Co 2:10–13, Jhn 14:17, Jhn 15:26, 1Jn 2:27, 1Jn 2:20, Act 2:17–18, Jhn 12:49
- 141Jn 4:13–14, 2Co 3:14–18, Jhn 15:26, Rev 19:10, 1Co 12:3, 1Pe 1:10–12, 1Jn 3:23–4:3, Gal 5:5
- 15Jhn 17:10, Mat 11:27, Jhn 3:35, Luk 10:22, Col 1:19, Mat 28:18, Jhn 13:3, Jhn 10:29–30
- 16Jhn 7:33, Jhn 16:22, Act 10:40–41, Jhn 16:28, Jhn 14:18–24, Act 1:3, Heb 12:2, Jhn 13:3
- 17Jhn 16:16, Mrk 9:32, Jhn 16:5, Jhn 16:19, Jhn 14:5, Luk 18:34, Jhn 12:16, Mrk 9:10
- 18Luk 24:25, Mat 16:9–11, Heb 5:12
- 19Jhn 16:30, Jhn 16:16, Jhn 14:19, Jhn 13:33, Jhn 7:33, Jhn 2:24–25, Rev 2:23, Mat 9:4
- 20Jas 1:2, Mat 5:4, Rev 7:14–17, Psa 126:5–6, Mrk 16:10, Jer 31:25, 2Co 6:10, 1Pe 1:6–8
- 21Psa 113:9, Isa 13:8, Jer 30:6–7, 1Th 5:3, Isa 26:16–18, Hos 13:13–14, Rev 12:2–5, Mic 4:10
- 221Pe 1:8, Act 13:52, Jhn 16:6, 2Th 2:16, Isa 25:9, Act 16:25, Psa 146:2, 1Pe 4:13–14
- 23Jhn 15:7, Jhn 14:13–14, Mat 21:22, Isa 65:24, 1Jn 5:14–16, Mat 7:7, Jhn 16:26, Jhn 14:20
- 24Mat 7:7–8, Jas 4:2–3, Jhn 15:11, Jhn 16:23, 2Th 2:16–17, 1Jn 1:3–4, 2Jn 1:12, Eph 1:16–17
- 25Jhn 16:12, Jhn 16:28–29, Jhn 10:6, Mrk 4:13, Mat 13:34–35, Psa 49:4, Mat 13:10–11, Psa 78:2
- 26Rom 8:34, Jhn 17:24, Jhn 17:9, Jhn 17:19, Jhn 14:16, Jhn 16:23
- 27Jhn 14:21, Jhn 14:23, Jhn 17:23, Jhn 8:42, 1Jn 4:19, Jhn 21:15–17, 2Co 5:14, Jhn 17:25–26
- 28Jhn 13:1, Jhn 13:3, Jhn 8:14, Jhn 17:5, Jhn 14:28, Jhn 16:5, Act 1:9–11, Jhn 17:11
- 29Jhn 16:25
- 30Jhn 21:17, Jhn 16:17, Heb 4:13, Jhn 17:8, Jhn 5:20, Jhn 16:27–28
- 31Luk 9:44–45, Jhn 13:38
- 32Zec 13:7, Mat 26:31, Jhn 8:29, Mrk 14:27, Jhn 8:16, Mat 26:56, Isa 50:6–9, Mrk 14:50
- 33Jhn 14:27, 1Jn 5:4, 2Th 3:16, 1Jn 4:4, Php 4:7, Jhn 14:1, 2Ti 3:12, 1Pe 5:9
Topics in this chapter
32
Afflictions and Adversities, Apostles, Blindness, Church, Conscience, Conviction, Faith, Gifts From God, God, Holy Spirit, Ignorance, Jesus, the Christ, Joy, Love, Neophytes, Peace, Persecution, Power, Prayer, Righteous, Satan, Symbols and Similitudes, Synagogue, Temptation, Tribulation, Trinity, Trouble, Truth, Unbelief, War, Wisdom, Zeal, Religious