Yohana 5
1 Baada ya haya, kulikuwa na Sikukuu ya Wayahudi, naye Isa akapanda kwenda Yerusalemu.
2 Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, palikuwa na bwawa moja lililoitwa Bethzatha kwa Kiebrania, ambalo lilikuwa limezungukwa na makumbi matano.
3 Hapa palikuwa na idadi kubwa ya wasiojiweza, yaani vipofu, viwete, na waliopooza [wakingojea maji yatibuliwe.
4 Kwa maana malaika alikuwa akishuka wakati fulani, akayatibua maji. Yule angekuwa wa kwanza kuingia ndani baada ya maji kutibuliwa alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao].
5 Mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa miaka thelathini na nane alikuwa hapo.
6 Isa alipomwona akiwa amelala hapo, na akijua amekuwa katika hali hiyo kwa muda mrefu, akamwambia, “Je, wataka kuponywa?”
7 Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kuniingiza bwawani maji yanapotibuliwa. Nami ninapotaka kutumbukia bwawani, mtu mwingine huingia kabla yangu.”
8 Isa akamwambia, “Inuka! Chukua mkeka wako na uende.”
9 Mara yule mtu akapona, akachukua mkeka wake, akaanza kutembea. Basi siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
10 Kwa hiyo viongozi wa Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato; si halali wewe kubeba mkeka wako.”
11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aliyeniponya aliniambia, ‘Chukua mkeka wako na uende.’ ”
12 Wakamuuliza, “Ni mtu gani huyo aliyekuambia uchukue mkeka wako uende?”
13 Basi yule mtu aliyeponywa hakufahamu ni nani aliyemponya, kwa sababu Isa alikuwa amepotea ndani ya umati ule wa watu waliokuwa hapo.
14 Baadaye Isa akamkuta yule mtu aliyemponya ndani ya Hekalu na kumwambia, “Tazama umeponywa. Usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo baya zaidi.”
15 Yule mtu akaenda, akawaambia wale viongozi wa Wayahudi kuwa ni Isa aliyemponya.
16 Kwa hiyo viongozi wa Wayahudi wakaanza kumsumbua Isa, kwa sababu alikuwa anafanya mambo kama hayo siku ya Sabato.
17 Isa akawajibu, “Baba yangu anafanya kazi yake daima hata siku hii ya leo, nami pia ninafanya kazi.”
18 Maneno haya yaliwaudhi sana viongozi wa Wayahudi. Wakajaribu kila njia wapate jinsi ya kumuua, kwani si kwamba alivunja Sabato tu, bali alikuwa akimwita Mungu Baba yake, hivyo kujifanya sawa na Mungu.
19 Isa akawaambia, “Amin, amin nawaambia, Mwana hawezi kufanya jambo lolote peke yake. Yeye aweza tu kufanya lile analomwona Baba yake akifanya, kwa maana lolote afanyalo Baba, Mwana pia hufanya vivyo hivyo.
20 Baba ampenda Mwana na kumwonesha yale ambayo yeye Baba mwenyewe anayafanya, naye atamwonesha kazi kuu kuliko hizi ili mpate kushangaa.
21 Hakika kama vile Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo Mwana huwapa uzima wale anaopenda.
22 Wala Baba hamhukumu mtu yeyote, lakini hukumu yote amempa Mwana,
23 ili wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Yeyote asiyemheshimu Mwana, hamheshimu Baba aliyemtuma.
24 “Amin, amin nawaambia, yeyote anayesikia maneno yangu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele, naye hatahukumiwa, bali amepita kutoka mautini na kuingia uzimani.
25 Amin, amin nawaambia, saa yaja, nayo saa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia watakuwa hai.
26 Kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake, vivyo hivyo amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake.
27 Naye amempa Mwanawe mamlaka ya kuhukumu kwa kuwa yeye ni Mwana wa Adamu.
28 “Msishangae kusikia haya, kwa maana saa inakuja ambapo wale walio makaburini wataisikia sauti yake,
29 nao watatoka makaburini. Wale waliotenda mema watafufuka wapate uzima, nao wale waliotenda maovu watafufuka ili wahukumiwe.
30 “Mimi siwezi kufanya jambo lolote peke yangu. Ninavyosikia ndivyo ninavyohukumu, nayo hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti kufanya mapenzi yangu mwenyewe, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
31 “Kama ningejishuhudia mimi mwenyewe, ushuhuda wangu si kweli.
32 Lakini yuko mwingine anishuhudiaye, na ninajua kwamba ushuhuda wake ni wa kweli.
33 “Mlituma wajumbe kwa Yahya, naye akaishuhudia kweli.
34 Si kwamba naukubali ushuhuda wa mwanadamu; la, bali ninalitaja hili ili ninyi mpate kuokolewa.
35 Yahya alikuwa taa iliyowaka na kutoa nuru, nanyi kwa muda mlichagua kuifurahia nuru yake.
36 “Ninao ushuhuda mkuu kuliko ule wa Yahya. Kazi ambazo Baba amenituma nizikamilishe, naam, kazi hizi ninazofanya, zinashuhudia kuwa Baba amenituma.
37 Naye Baba mwenyewe ameshuhudia juu yangu. Hamjapata kamwe kuisikia sauti yake wala kuona umbo lake,
38 wala hamna neno lake ndani yenu, kwa sababu hamkumwamini yeye aliyetumwa naye.
39 Ninyi mnachunguza Maandiko mkidhani ya kuwa ndani yake mna uzima wa milele. Maandiko haya ndio yanayonishuhudia mimi.
40 Lakini mnakataa kuja kwangu ili mpate uzima.
41 “Mimi sikubali kutukuzwa na wanadamu,
42 lakini mimi ninawafahamu. Ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu.
43 Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, nanyi hamnipokei. Lakini mtu mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea.
44 Mnawezaje kuamini ikiwa mnapeana utukufu ninyi kwa ninyi, lakini hamfanyi bidii kupata utukufu unaotoka kwa Mungu?
45 “Lakini msidhani kuwa mimi nitawashtaki mbele za Baba. Mshtaki wenu ni Musa, ambaye mmemwekea tumaini lenu.
46 Kama mngemwamini Musa, mngeniamini na mimi, kwa maana aliandika habari zangu.
47 Lakini ikiwa hamwamini aliyoandika Musa, mtaaminije ninayoyasema?”
ข้ออ้างอิงโยง
331
- 1Deu 16:16, Exo 23:14–17, Lev 23:2–4, Exo 34:23, Jhn 2:13
- 2Neh 3:1, Neh 12:39, Neh 3:32, Isa 22:11, Jhn 19:13, Isa 22:9, Jhn 20:16, Jhn 19:17
- 3Mrk 3:1–4, Mat 15:30, Luk 7:22, Zec 11:17, Lam 3:26, Jas 5:7, Pro 8:34, Rom 8:25
- 5Act 3:2, Luk 8:43, Mrk 9:21, Luk 13:16, Act 14:8, Act 9:33, Jhn 5:14, Jhn 9:1
- 6Luk 18:41, Heb 4:15, Heb 4:13, Isa 65:1, Jhn 21:17, Psa 142:3, Jer 13:27
- 7Psa 72:12, Deu 32:36, 1Co 9:24, Psa 142:4, 2Co 1:8–10, Rom 5:6, Jhn 5:3
- 8Luk 5:24, Mat 9:6, Mrk 2:11, Act 9:34
- 9Act 3:7–8, Jhn 9:14, Mrk 3:2–4, Mat 12:10–13, Mrk 1:31, Mrk 5:29, Mrk 1:42, Mrk 10:52
- 10Jer 17:21, Luk 6:2, Jhn 9:16, Mrk 3:4, Luk 13:14, Mrk 2:24, Neh 13:15–21, Mat 12:2–8
- 11Mrk 2:9–11, Jhn 9:16
- 12Mat 21:23, Jdg 6:29, Rom 10:2, 1Sa 14:38
- 13Luk 4:30, Luk 24:31, Jhn 14:9, Jhn 8:59
- 14Jhn 8:11, Lev 26:23–24, Psa 118:18, Mat 12:45, Neh 9:28, Psa 107:20–22, Rev 2:21–23, Isa 38:20
- 15Jhn 4:29, Jhn 9:11–12, Jhn 9:25, Mrk 1:45, Jhn 1:19, Jhn 9:34, Jhn 9:15, Jhn 5:12
- 16Jhn 10:39, Act 9:4–5, Luk 6:11, Jhn 15:20, Jhn 7:25, Jhn 5:13, Mat 12:13, Jhn 7:19–20
- 17Jhn 9:4, Jhn 14:10, 1Co 12:6, Col 1:16, Heb 1:3, Gen 2:1–2, Isa 40:26, Act 17:28
- 18Jhn 10:30, Jhn 10:33, Jhn 19:7, Jhn 8:58, Jhn 5:23, Jhn 14:23, Rev 22:1, Jhn 8:54
- 19Jhn 12:49, Jhn 8:28, Jhn 14:10, Jhn 10:18, Jhn 5:28–30, Rom 8:11, Jhn 14:16–23, Luk 21:15
- 20Jhn 3:35, Mat 3:17, Pro 8:22–31, Jhn 15:15, 2Pe 1:17, Jhn 17:26, Jhn 12:45–47, Jhn 5:29
- 21Rom 8:11, Deu 32:39, Jhn 11:25, Act 26:8, Luk 7:14–15, Jhn 17:2, Luk 8:54–55, Jhn 11:43–44
- 22Jhn 5:27, Act 17:31, Mat 28:18, 2Co 5:10, Act 10:42, Jhn 9:39, 2Ti 4:1, Rom 2:16
- 231Jn 2:23, Luk 10:16, Mat 11:27, 2Jn 1:9, Jhn 15:23–24, Jer 17:5–7, Luk 12:8–9, 1Th 3:11–13
- 24Jhn 3:36, Jhn 6:40, 1Jn 5:11–13, Jhn 3:18, Rom 8:1, Jhn 11:26, Jhn 6:47, Jhn 3:16
- 25Jhn 5:28, Eph 5:14, Eph 2:5, Jhn 4:23, Jhn 8:47, Col 2:13, Rom 6:4, Rev 3:1
- 26Jhn 1:4, Jhn 11:26, Jhn 14:6, Exo 3:14, Jhn 17:2–3, 1Co 15:45, 1Ti 1:17, Jer 10:10
- 27Act 10:42, Jhn 5:22, Act 17:31, 1Pe 3:22, 1Co 15:25, Dan 7:13–14, Psa 110:6, Eph 1:20–23
- 28Rev 20:12, 1Th 4:14–17, Isa 26:19, Jhn 11:24–25, Job 19:25–26, 1Co 15:42–54, 1Co 15:22, Jhn 6:39–40
- 29Dan 12:2–3, Rom 2:6–10, Act 24:15, Mat 25:31–46, Luk 14:14, Gal 6:8–10, 1Ti 6:18, Heb 13:16
- 30Jhn 6:38, Jhn 5:19, Jhn 4:34, Jhn 14:10, Mat 26:39, Jhn 8:28, Psa 40:7–8, Jhn 8:15–16
- 31Pro 27:2, Jhn 8:54, Rev 3:14, Jhn 8:13–14
- 321Jn 5:6–9, Jhn 1:33, Jhn 12:50, Jhn 12:28–30, Jhn 5:36–37, Mat 17:5, Jhn 8:17–18, Mat 3:17
- 33Jhn 1:29–34, Jhn 3:26–36, Jhn 1:6–8, Jhn 1:15–27
- 34Jhn 20:31, 1Jn 5:9, Luk 19:41–42, 1Ti 4:16, 1Ti 2:3–4, Rom 10:1, 1Co 9:22, Jhn 5:41
- 352Pe 1:19, Jhn 1:7–8, Mat 11:11, Mat 3:5–7, Luk 1:76–77, Mrk 6:20, Mat 13:20–21, Mat 21:26
- 36Jhn 10:25, Jhn 10:37–38, Jhn 15:24, Jhn 2:23, Jhn 9:30–33, 1Jn 5:9, Jhn 3:2, Act 2:22
- 37Jhn 8:18, Mat 3:17, Jhn 1:18, 1Ti 1:17, 1Ti 6:16, 1Jn 4:20, 1Jn 4:12, Exo 20:19
- 381Jn 2:14, Jhn 12:44–48, Deu 6:6–9, Isa 53:1–3, Jas 1:21–22, Pro 7:1–2, Jhn 1:11, Jhn 8:37
- 39Luk 24:27, Luk 24:44, 2Pe 1:19–21, Act 26:22–23, Pro 8:33–34, Mat 22:29, 2Ti 3:14–17, Isa 34:16
- 40Jhn 3:19, Jhn 1:11, Psa 81:11, Jhn 6:37, Isa 50:2, Isa 49:7, Mat 23:37, Jhn 7:37–38
- 41Jhn 7:18, 1Th 2:6, Jhn 8:50, Jhn 5:34, Jhn 8:54, Jhn 5:44, Jhn 6:15, 1Pe 2:21
- 421Jn 4:20, 1Jn 3:17, Rom 8:7, Jhn 2:25, 1Jn 2:15, Jhn 8:47, Rev 2:23, Heb 4:12–13
- 43Mat 24:5, Jhn 10:25, Jhn 17:4–6, Heb 5:4–5, Jhn 6:38, Mat 24:24, Jhn 8:28–29, Jhn 12:28
- 44Jhn 12:43, Rom 2:29, Php 2:3, Mat 23:5, Rom 8:7–8, 1Pe 1:7, 1Sa 2:30, Rom 2:10
- 45Gal 3:10, Rom 3:19–20, Rom 2:12, 2Co 3:7–11, Rom 10:5–10, Jhn 9:28–29, Jhn 7:19, Mat 19:7–8
- 46Deu 18:15, Deu 18:18–19, Jhn 1:45, Luk 24:27, Num 24:17–18, Gen 49:10, Act 26:22, Gen 22:18
- 47Luk 16:31, Luk 16:29
Topics in this chapter
48
Ambition, Angel (A Spirit), Bethesda, Bigotry, Confidence, Death, Faith, Feasts, God, Godlessness, Heaven, Hebrew, Holiness, Immortality, Instability, Jerusalem, Jesus, the Christ, John, Judgment, Justification, Law, Life, Light, Love, Minister, Christian, Miracles, Obedience, Persecution, Power, Punishment, Quickening, Regeneration, Resurrection, Righteous, Sabbath, Salvation, Sheep Gate, Sheep Market, Sin, Slander, Temple, Truth, Unbelief, Voice, Wicked (People), Will, Word of God, Worldliness