Yohana 1
1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, naye huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3 Vitu vyote viliumbwa kupitia kwake, na hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa pasipo yeye.
4 Ndani yake kulikuwa na uzima, nao huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5 Nuru hung’aa gizani nalo giza halikuishinda.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yahya.
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9 Nuru halisi inayomwangazia kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni, na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
12 Bali wote waliompokea, yaani wale walioliamini jina lake, aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu.
13 Hawa hawakuzaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali wamezaliwa kwa mapenzi ya Mungu.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 Yahya alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.’ ”
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Musa, lakini neema na kweli zimekuja kupitia Isa Al-Masihi.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba, ndiye ambaye amemdhihirisha.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yahya wakati viongozi wa Wayahudi waliwatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
20 Yahya alikiri waziwazi pasipo kuficha, akasema, “Mimi si Al-Masihi.”
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani, basi? Je, wewe ni Ilya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Mwenyezi Mungu.’ ”
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo,
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Al-Masihi, wala si Ilya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
26 Yahya akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini kati yenu yupo mtu msiyemjua.
27 Yeye anakuja baada yangu, nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ng’ambo ya Yordani, mahali Yahya alipokuwa akibatiza.
29 Siku iliyofuata, Yahya alimwona Isa akimjia, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.’
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
32 Kisha Yahya akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho Mtakatifu wa Mungu akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho Mtakatifu wa Mungu akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho wa Mungu.’
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
35 Siku iliyofuata, Yahya alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
36 Alipomwona Isa akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yahya akisema haya, wakamfuata Isa.
38 Isa akageuka, akawaona wakimfuata, akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Mwalimu, unaishi wapi?”
39 Isa akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
40 Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yahya alisema na kumfuata Isa.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masihi” (yaani Al-Masihi).
42 Naye akamleta kwa Isa. Isa akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
43 Siku iliyofuata Isa aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
44 Filipo alikuwa raia wa Bethsaida, mji walikotoka Andrea na Petro.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Musa aliandika habari zake katika Torati, na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani Isa Al-Nasiri, mwana wa Yusufu.”
46 Nathanaeli akauliza, “Nasiri! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nasiri?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
47 Isa alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake, akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Isa akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
49 Nathanaeli akamwambia, “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
50 Isa akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu kuliko hilo.”
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
ข้ออ้างอิงโยง
348
- 1Gen 1:1, Jhn 17:5, Rev 19:13, Col 1:17, Jhn 1:14, 1Jn 1:1–2, Rev 22:13, Jhn 1:2
- 3Col 1:16–17, 1Co 8:6, Rev 4:11, Psa 33:6, Gen 1:26, Jhn 1:10, Heb 1:2–3, Isa 45:18
- 4Jhn 8:12, Jhn 12:46, Jhn 5:26, 1Jn 1:5–7, Jhn 9:5, Luk 1:78–79, Jhn 11:25, Isa 42:6–7
- 5Jhn 3:19–20, Jhn 12:36–40, 1Co 2:14, Job 24:13–17, Jhn 1:10, Rom 1:28, Pro 1:29–30, Pro 1:22
- 6Mal 3:1, Jhn 3:28, Isa 40:3–5, Luk 1:76, Act 13:24, Jhn 1:33, Mat 11:10, Mrk 1:1–8
- 7Act 19:4, Jhn 1:32–34, Jhn 1:36, Jhn 5:33–35, Jhn 1:12, Jhn 1:9, Jhn 3:26–36, Jhn 1:26–27
- 8Jhn 1:20, Jhn 3:28, Act 19:4
- 9Jhn 12:46, Jhn 1:4, 1Jn 2:8, Isa 49:6, 1Th 5:4–7, Jhn 1:7, 1Jn 5:20, Jhn 6:32
- 10Jhn 17:25, 1Jn 3:1, 1Co 2:8, 1Co 1:21, Mat 11:27, Heb 11:3, Act 17:24–27, Jhn 1:18
- 11Luk 19:14, Isa 53:2–3, Jhn 3:32, Act 7:51–52, Luk 20:13–15, Mat 15:24, Rom 15:8, Act 3:25–26
- 12Gal 3:26, Rom 8:14, 1Jn 3:1, 2Co 6:17–18, Gal 4:6, Jhn 3:18, Mat 10:40, 1Jn 5:12–13
- 13Jas 1:18, 1Jn 3:9, 1Pe 1:23, 1Pe 1:3, Jhn 3:5–8, 1Jn 5:4, 1Jn 2:28–29, 1Jn 4:7
- 141Jn 4:9, 1Ti 3:16, Gal 4:4, Jhn 1:1, Isa 40:5, Heb 1:3, 1Jn 1:1–2, Php 2:6–8
- 15Mat 3:11, Col 1:17, Luk 3:16, Jhn 1:29–34, Jhn 1:1–2, Jhn 3:26–36, Jhn 5:33–36, Mat 3:13–17
- 16Col 1:19, Rom 5:2, Eph 2:5–10, Eph 4:7–13, Col 2:9–10, Eph 3:19, Eph 1:23, Rom 5:17
- 17Rom 6:14, Jhn 14:6, Rom 5:20–21, Rom 3:19–26, Jhn 1:14, Heb 9:22, Jhn 8:32, Jhn 7:19
- 18Col 1:15, Jhn 6:46, Mat 11:27, Luk 10:22, 1Jn 4:12, 1Ti 6:16, 1Jn 4:9, 1Jn 4:20
- 19Luk 3:15–18, Jhn 10:24, Act 19:4, Act 13:25, Jhn 5:33–36, Mat 21:23–32, Jhn 2:18
- 20Mat 3:11–12, Mrk 1:7–8, Luk 3:15–17, Jhn 3:28–36
- 21Deu 18:15–18, Mal 4:5, Mat 11:14, Jhn 1:25, Luk 1:17, Mat 17:10–12, Mat 16:14, Jhn 7:40
- 23Isa 40:3–5, Mrk 1:3, Mat 3:3, Luk 3:4–6, Luk 1:76–79, Luk 1:16–17, Jhn 3:28
- 24Luk 11:39–44, Mat 23:13–15, Luk 11:53, Luk 7:30, Luk 16:14, Jhn 3:1–2, Act 23:8, Php 3:5–6
- 25Deu 18:18, Deu 18:15, Jhn 1:20–22, Mat 21:23, Act 5:28, Act 4:5–7, Dan 9:24–26
- 26Jhn 1:10–11, Luk 3:16, Act 1:5, Mrk 1:8, Mat 3:11, Jhn 8:19, Act 11:16, 1Jn 3:1
- 27Luk 3:16, Mrk 1:7, Mat 3:11, Jhn 1:30, Jhn 1:15, Act 19:4
- 28Jhn 10:40, Jhn 3:23, Jdg 7:24, Jhn 3:26
- 29Isa 53:7, 1Jn 2:2, 1Jn 3:5, 1Pe 1:19, 2Co 5:21, 1Pe 2:24, Isa 53:11, Heb 1:3
- 30Jhn 1:15, Jhn 1:27, Luk 3:16
- 31Mal 3:1, Luk 1:17, Jhn 1:33, Jhn 1:7, Luk 3:3–4, Mal 4:2–5, Mrk 1:3–5, Mat 3:6
- 32Luk 3:22, Mrk 1:10, Mat 3:16, Jhn 1:7, Jhn 5:32
- 33Act 1:5, Mat 3:11, Luk 3:16, Tit 3:5–6, Act 10:44–47, Jhn 3:34, Mrk 1:7–8, Act 19:2–6
- 34Psa 2:7, Jhn 1:49, Mat 4:3, 1Jn 5:20, Psa 89:26–27, Rev 2:18, Jhn 20:31, Rom 1:4
- 35Mal 3:16, Jhn 3:25–26
- 36Jhn 1:29, 1Pe 1:19–20, Isa 65:1–2, Heb 12:2, Isa 45:22
- 37Rom 10:17, Rev 22:17, Jhn 1:43, Zec 8:21, Jhn 4:39–42, Eph 4:29, Pro 15:23
- 38Jhn 18:7, Jhn 3:2, Jhn 1:49, Pro 8:34, Psa 27:4, Jhn 18:4, Jhn 12:21, Jhn 3:26
- 39Luk 24:29, Mat 11:28–30, Jhn 6:37, Jhn 4:40, Jhn 1:46, Pro 8:17, Rev 3:20, Jhn 14:22–23
- 40Mrk 1:16–20, Mat 4:18–22, Jhn 1:40–42, Luk 5:2–11, Mat 10:2, Jhn 6:8, Act 1:13
- 41Jhn 4:25, Jhn 1:45, Isa 2:3–5, Act 13:32–33, Psa 89:20, Act 10:38, Jhn 1:36–37, Luk 2:17
- 42Jhn 21:15–17, 1Co 3:22, 1Co 15:5, 1Co 1:12, Mat 16:17–18, Gal 2:9, 1Co 9:5, Mat 10:2
- 43Isa 65:1, Jhn 14:8, Mat 9:9, Mat 4:18–21, Jhn 12:21, 1Jn 4:19, Jhn 6:5, Php 3:12
- 44Jhn 12:21, Mat 11:21, Mat 10:3, Luk 9:10, Mrk 8:22, Luk 10:13, Mrk 3:18, Mrk 6:45
- 45Deu 18:18–22, Mic 5:2, Luk 24:27, Mat 2:23, Luk 24:44, Isa 7:14, Isa 9:6, Jhn 5:45–46
- 46Jhn 7:52, Jhn 7:41–42, Jhn 4:29, 1Th 5:21, Luk 12:57
- 47Rev 14:5, Psa 32:2, Psa 73:1, Jhn 8:39, Rom 9:4, Rom 9:6, Rom 2:28–29, Jhn 8:31
- 48Isa 65:24, Jhn 2:25, Psa 139:1–2, Mat 6:6, Rev 2:18–19, Gen 32:24–30, 1Co 14:25, 1Co 4:5
- 49Zep 3:15, Zec 9:9, Mat 27:42, Luk 19:38, Jhn 12:13–15, Mat 2:2, Mat 21:5, Jhn 1:34
- 50Jhn 20:29, Jhn 11:40, Luk 1:45, Mat 25:29
- 51Gen 28:12, Act 7:56, Luk 22:43, Mat 16:27–28, Mrk 1:10, Luk 2:13, Act 10:11, Mrk 14:62
Topics in this chapter
62
Adoption, Andrew, Angel (A Spirit), Apostles, Atonement, Baptism, Bethabara, Bethsaida, Blessing, Blindness, Character, Confession, Converts, Daily Offering, Darkness, Decision, Depravity of Man, Dove, Turtle, Earth, Elijah, Faith, Glory, God, Gospel, Holiness, Holy Spirit, Humility, Ingratitude, Integrity, Jesus, the Christ, John, Jonas, Lamb of God, Law, Light, Minister, Christian, Nathanael, Nazareth, Obedience, Offerings, Perfection, Peter, Philip, Power, Priest, Prophets, Proverbs, Quotations and Allusions, Rabbi, Regeneration, Salvation, Sincerity, Symbols and Similitudes, Trinity, Truth, Types, Unbelief, Uncharitableness, Vision, Wisdom, Word, Zeal, Religious