Yohana 10
1 “Amin, amin nawaambia, yeye asiyeingia katika zizi la kondoo kupitia kwenye lango, lakini akwea kuingia ndani kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang’anyi.
2 Yeye anayeingia kupitia kwenye lango ndiye mchungaji wa kondoo.
3 Mlinzi humfungulia lango, na kondoo huisikia sauti yake. Yeye huwaita kondoo wake kwa majina yao na kuwatoa nje ya zizi.
4 Baada ya kuwatoa wote nje, yeye hutangulia mbele yao na kondoo humfuata, kwa kuwa wanaijua sauti yake.
5 Lakini kondoo hawatamfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti ya mgeni.”
6 Isa alitumia mfano huu, lakini wao hawakuelewa hayo aliyokuwa akiwaambia.
7 Kwa hiyo Isa akasema nao tena, akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
8 Wote walionitangulia ni wezi na wanyang’anyi, nao kondoo hawakuwasikia.
9 Mimi ndimi lango. Yeyote anayeingia zizini kupitia kwangu ataokoka. Ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
10 Mwizi huja ili aibe, aue na aangamize. Mimi nimekuja ili wapate uzima, kisha wawe nao tele.
11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
12 Mtu wa kuajiriwa sio mchungaji mwenye kondoo. Anapomwona mbwa-mwitu akija, yeye hukimbia na kuwaacha kondoo. Naye mbwa-mwitu hulishambulia kundi na kulitawanya.
13 Yeye hukimbia kwa sababu ameajiriwa wala hawajali kondoo.
14 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Ninawajua kondoo wangu, nao kondoo wangu wananijua.
15 Kama vile Baba anavyonijua mimi, nami ninavyomjua Baba, ndivyo nami ninautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
16 Ninao kondoo wengine ambao si wa zizi hili. Inanipasa kuwaleta, nao wataisikia sauti yangu; hivyo patakuwa na kundi moja na mchungaji mmoja.
17 Baba yangu ananipenda kwa kuwa ninautoa uhai wangu ili niupate tena.
18 Hakuna mtu aniondoleaye uhai wangu, bali ninautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa uhai wangu, na pia ninao uwezo wa kuutwaa tena. Amri hii nimepewa na Baba yangu.”
19 Waliposikia maneno haya, Wayahudi wakagawanyika.
20 Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
21 Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
22 Ikafika Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu. Ilikuwa majira ya baridi.
23 Naye Isa alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika Ukumbi wa Sulemani.
24 Wayahudi wakamkusanyikia, wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka hadi lini? Kama wewe ndiwe Al-Masihi, tuambie waziwazi.”
25 Isa akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
26 Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
27 Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata.
28 Nami ninawapa uzima wa milele; hawataangamia kamwe, wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu.
29 Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote, na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
30 Mimi na Baba yangu tu umoja.”
31 Kwa mara nyingine Wayahudi wakainua mawe ili wampige nayo,
32 lakini Isa akawaambia, “Nimewaonesha miujiza mingi mikubwa kutoka kwa Baba yangu. Ni kwa ipi kati ya hiyo miujiza mnataka kunipiga mawe?”
33 Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa sababu ya mambo mema uliyotenda, bali ni kwa kuwa umekufuru. Ingawa wewe ni mwanadamu, unajifanya kuwa Mungu.”
34 Isa akawajibu, “Je, haikuandikwa katika Torati yenu kwamba, ‘Nimesema kuwa ninyi ni “miungu” ’?
35 Kama aliwaita ‘miungu’ wale ambao neno la Mungu liliwafikia, nayo Maandiko hayawezi kutanguka,
36 je, mwawezaje kusema kwamba yule ambaye Baba amemweka wakfu na kumtuma ulimwenguni anakufuru, kwa sababu nilisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu’?
37 Ikiwa sifanyi kazi za Baba yangu, basi msiniamini.
38 Lakini ikiwa nazifanya kazi za Mungu, hata kama hamniamini mimi ziaminini hizo kazi, ili mpate kujua na kuelewa kwamba Baba yu ndani yangu, nami ni ndani yake.”
39 Ndipo wakajaribu kumkamata kwa mara nyingine, lakini akaponyoka kutoka mikononi mwao.
40 Isa akaenda tena ng’ambo ya Yordani hadi mahali Yahya alikuwa akibatiza hapo awali, naye akakaa huko.
41 Watu wengi wakamjia, nao wakawa wakisema, “Yahya hakufanya muujiza wowote, lakini kila jambo alilosema kumhusu huyu mtu ni kweli.”
42 Nao watu wengi wakamwamini Isa huko.
ข้ออ้างอิงโยง
305
- 1Mat 7:15, 1Jn 4:1, Jhn 10:8–10, Rom 16:18, Heb 5:4, 2Pe 2:1, Zec 11:16–17, 2Pe 2:3
- 2Act 20:28, Jhn 10:14, 1Pe 5:4, Psa 23:1, Isa 40:11, Ecc 12:11, Jhn 10:9, 1Ti 4:14
- 3Ezk 34:11–16, 2Ti 2:19, Jhn 10:4, Rev 3:20, Jhn 10:14, Psa 78:52–53, Jhn 10:16, Jhn 10:26–27
- 4Deu 1:30, Jhn 10:16, Jhn 12:26, Jhn 10:8, Jhn 18:37, 1Co 11:1, 1Pe 2:21, 1Pe 5:3
- 51Jn 4:5–6, Col 2:6–10, Mrk 4:24, Rev 2:2, 1Pe 2:1–3, Pro 19:27, Eph 4:11–15, 2Ti 3:5–7
- 6Isa 56:11, Psa 82:5, Pro 28:5, Dan 12:10, Mat 13:51, Psa 106:7, Jhn 16:25, Isa 6:9–10
- 7Jhn 14:6, Eph 2:18, Jhn 10:1, Jhn 10:9, Ezk 34:31, Psa 79:13, Heb 10:19–22, Psa 100:3
- 8Ezk 34:2, Jer 23:1, Jhn 10:1, Jhn 10:27, Isa 56:10–12, Ezk 22:25–28, Act 5:36, Zec 11:4–9
- 9Jhn 14:6, Eph 2:18, Jhn 10:7, Jhn 10:1, Rom 5:1–2, Psa 100:3–4, Psa 95:7, Psa 23:1–6
- 10Luk 19:10, Jhn 6:51, Jhn 12:47, Jhn 3:17, Jhn 6:33, 1Ti 1:15, Mat 20:28, Jhn 10:1
- 11Psa 23:1, Jhn 10:14–15, Jhn 15:13, Rev 7:17, Isa 40:11, 1Pe 2:24–25, 1Jn 3:16, Heb 13:20
- 122Pe 2:3, Act 20:29, Zec 11:16–17, Ezk 34:2–6, Mat 10:16, 1Pe 5:2, 2Ti 4:10, Mat 7:15
- 13Php 2:20, Jhn 12:6, Act 18:17
- 14Jhn 10:27, 2Ti 2:19, Jhn 10:11, Eph 1:17, 1Jn 5:20, Jhn 17:3, 2Ti 1:12, Psa 1:6
- 15Gal 1:4, Jhn 10:11, Isa 53:10, Mat 11:27, 1Jn 2:2, 1Pe 3:18, Zec 13:7, Jhn 10:17–18
- 16Isa 56:8, Jhn 11:52, 1Pe 2:25, Ezk 34:23, Eph 2:13–18, Ezk 37:24, 1Pe 2:10, Jhn 6:37
- 17Jhn 10:18, Jhn 10:15, Jhn 10:11, Heb 2:9, Jhn 17:4–5, Isa 53:7–12, Jhn 15:9–10, Isa 42:1
- 18Tit 2:14, Heb 2:9, Jhn 10:17, Jhn 2:19–21, Jhn 14:31, Isa 53:10–12, Heb 5:6–9, Jhn 6:38
- 191Co 3:3, Jhn 9:16, Jhn 7:40–43, Act 14:4, Act 23:7–10, Luk 12:51–53, 1Co 11:18, Mat 10:34–35
- 20Jhn 7:20, Mrk 3:21, Jhn 8:52, Jhn 8:47–48, Isa 53:8, Mat 10:25, Act 26:24, Jhn 7:46–52
- 21Exo 4:11, Isa 35:5–6, Mat 11:5, Psa 94:9, Exo 8:19, Psa 146:8, Jhn 9:32–33, Mat 4:24
- 23Act 3:11, Act 5:12
- 24Jhn 1:19, Luk 22:67–70, 1Ki 18:21, Jhn 8:53, Mat 11:3, Jhn 8:25, Luk 3:15, Jhn 16:25
- 25Jhn 10:38, Jhn 8:58, Jhn 14:11, Heb 2:3, Jhn 5:17–43, Jhn 3:2, Jhn 20:30, Jhn 12:37
- 26Jhn 8:47, 2Co 4:3–4, Jhn 10:27, Jhn 12:37–40, Rom 11:7–8, Jhn 6:65, Jhn 6:44–45, Jhn 10:4
- 27Jhn 10:16, Jhn 10:14, 1Co 8:3, Rev 3:20, Jhn 10:3–4, Heb 3:7, Jhn 5:25, Jhn 8:12
- 28Jhn 6:39–40, Jhn 6:37, Jhn 3:15–16, Heb 7:25, Jhn 18:9, Rom 8:29, Isa 54:17, Php 1:6
- 29Jhn 6:37, Jhn 17:9, Jhn 17:2, Jhn 14:28, Jhn 17:6, Mal 1:14, Jhn 17:11, Exo 18:11
- 30Jhn 1:1–2, Jhn 14:9, Jhn 17:21–23, Jhn 5:23, Jhn 8:58, Mat 11:27, Mat 28:19, Jhn 5:17
- 31Jhn 8:59, Jhn 5:18, Exo 17:4, 1Sa 30:6, Jhn 11:8, Act 7:52, Mat 23:35, Mat 21:35
- 32Psa 109:4–5, Ecc 4:4, 2Ch 24:20–22, Jhn 5:19–20, Mat 11:5, Jhn 10:37, Act 10:38, Psa 35:12
- 33Jhn 5:18, Jhn 10:30, Lev 24:16, Php 2:6, Rom 13:1, Psa 82:6, 1Ki 21:10, Lev 24:14
- 34Psa 82:6–7, Exo 7:1, Psa 82:1, Exo 4:16, Psa 138:1
- 35Mat 24:35, Rom 13:1, Gen 15:1, Luk 24:44–46, Luk 16:17, Jhn 19:36–37, Act 1:16, Mat 26:53–56
- 36Jhn 3:17, Jhn 5:17–18, Jer 1:5, Jhn 10:30–33, Jhn 20:28, Jhn 6:27, Jhn 20:31, Jhn 9:35–37
- 37Jhn 15:24, Jhn 10:25, Mat 11:20–24, Jhn 10:32, Jhn 12:37–40, Jhn 14:10, Jhn 5:31
- 38Jhn 10:30, Jhn 14:20, Jhn 10:25, Jhn 14:9–11, Act 2:22, Jhn 3:2, Jhn 17:21–23, Jhn 5:36
- 39Jhn 7:30, Jhn 8:59, Jhn 7:44, Luk 4:29–30, Jhn 10:31
- 40Jhn 1:28, Jhn 11:54, Jhn 7:1, Jhn 3:26
- 41Jhn 1:33–34, Jhn 1:29–30, Jhn 2:11, Mat 3:11–12, Mat 14:2, Jhn 1:27, Luk 12:1, Jhn 3:26–36
- 42Jhn 4:41, Jhn 12:42, Jhn 4:39, Jhn 2:23, Jhn 11:45, Jhn 7:31, Jhn 8:30
Topics in this chapter
43
Apostles, Baptism, Bethabara, Character, Church, Demons, Employee, Faith, Falsehood, Feasts, Gentiles, God, Heaven, Immortality, Insanity, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, John, Life, Minister, Christian, Obedience, Penitent, Persecution, Perseverance, Power, Quotations and Allusions, Regeneration, Reprobacy, Righteous, Salvation, Sheep, Shepherd, Slander, Solomon's Porch, Strife, Suffering, Temple, Theft and Thieves, Unbelief, Wisdom, Wolf, Word of God, Works