Yohana 20
1 Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa bado giza, Mariamu Magdalene alienda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
2 Hivyo akakimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Isa alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
3 Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara moja kuelekea kaburini.
4 Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 Akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani, lakini hakuingia.
6 Ndipo Simoni Petro akaja akimfuata nyuma, akaingia ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini,
7 na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Isa. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
8 Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini akaingia ndani, akaona, na akaamini.
9 (Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Isa afufuke kutoka kwa wafu.)
10 Kisha hao wanafunzi wakaondoka, wakarudi nyumbani mwao.
11 Lakini Mariamu Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama kuchungulia mle kaburini,
12 naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Isa ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
13 Wakamuuliza Mariamu, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu, na sijui walikomweka.”
14 Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Isa amesimama, lakini hakumtambua.
15 Isa akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Mariamu, akidhani alikuwa anaongea na mtunza bustani, akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nioneshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Isa akamwita, “Mariamu!” Ndipo Mariamu akamgeukia Isa na kusema naye kwa Kiebrania, “Raboni!” (maana yake “Mwalimu”).
17 Isa akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’ ”
18 Kwa hiyo Mariamu Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Isa, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Isa alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
19 Ilipokuwa jioni ya siku hiyo hiyo ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi. Naye Isa akawatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
20 Baada ya kusema haya, akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana Isa.
21 Isa akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi.”
22 Alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu wa Mungu.
23 Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa; na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
24 Lakini Tomaso (aliyeitwa Didimasi), mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Isa alipokuja.
25 Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana Isa.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari, na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
26 Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Isa akaja, milango ikiwa imefungwa, na kusimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi.”
27 Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
28 Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Isa akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
30 Isa alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
31 Lakini hii imeandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Isa ndiye Al-Masihi, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.
ข้ออ้างอิงโยง
199
- 1Mrk 16:9, Mat 27:60, Luk 24:1–10, Mrk 15:46, Jhn 19:25, Rev 1:10, Jhn 20:18–19, Jhn 20:26
- 2Jhn 13:23, Jhn 20:13, Jhn 21:24, Jhn 19:26, Jhn 21:20, Jhn 21:7, Mat 27:63–64, Jhn 20:15
- 3Luk 24:12
- 42Sa 18:23, 1Co 9:24
- 5Jhn 19:40, Jhn 11:44, Jhn 20:11
- 6Luk 22:31–32, Mat 16:15–16, Jhn 21:15–17, Jhn 18:25–27, Jhn 6:67–69, Jhn 21:7, Jhn 18:17
- 7Jhn 11:44
- 8Jhn 20:25, Jhn 1:50, Jhn 20:4, Jhn 20:29
- 9Psa 16:10, Isa 25:8, Isa 53:10–12, Luk 24:44–46, Isa 26:19, 1Co 15:4, Luk 24:26, Hos 13:14
- 10Jhn 16:32, Jhn 7:53
- 11Jhn 20:5
- 12Luk 24:3–7, Rev 3:4, Dan 7:9, Mrk 16:5–6, Rev 7:14, Luk 24:22–23, 2Ch 5:12, Mat 17:2
- 13Jhn 20:15, Jhn 16:20–22, Jhn 2:4, 1Sa 1:8, Psa 43:3–5, Jhn 14:27–28, Act 21:13, Jhn 20:2
- 14Luk 24:16, Sng 3:3–4, Mat 28:9, Jhn 21:4, Mrk 16:9, Jhn 8:59, Luk 24:31, Mrk 16:12
- 15Jhn 18:7, Jhn 20:13, Sng 3:2, Jhn 1:38, Jhn 18:4, Mrk 16:6, Mat 28:5, 1Sa 1:16
- 16Jhn 10:3, Jhn 1:38, Sng 2:8–17, Sng 3:4, 1Sa 3:10, Luk 10:41, Sng 5:2, Gen 45:12
- 17Jhn 16:28, Eph 4:8–10, 1Pe 1:3, Gal 4:6–7, Jhn 17:11, Eph 1:17–23, Psa 68:18, Heb 2:11–13
- 18Luk 24:10, Mat 28:10, Mrk 16:10–13, Luk 24:22–23, Jhn 20:1
- 19Jhn 20:26, Jhn 14:27, Luk 24:36–49, Jhn 20:21, 2Th 3:16, Jhn 7:13, Eph 2:14, Mrk 16:14
- 20Jhn 16:22, Jhn 20:27, Luk 24:39–41, 1Jn 1:1, Jhn 16:20, Jhn 19:34, Isa 25:8–9, Mat 28:8
- 21Jhn 17:18–19, Mat 28:18–20, Jhn 13:20, Jhn 3:17, Mrk 16:15–18, Act 1:8, Luk 24:47–49, Mat 10:16
- 22Job 33:4, Gen 2:7, Act 8:15, Jhn 7:39, Act 2:38, Ezk 37:9, Psa 33:6, Act 19:2
- 23Mat 18:18, Mat 16:19, Mrk 2:5–10, Act 13:38–39, Act 10:43, 2Co 2:6–10, Act 2:38, 1Ti 1:20
- 24Jhn 11:16, Heb 10:25, Jhn 6:66–67, Jhn 21:2, Jhn 14:5
- 25Jhn 6:30, Mrk 16:11, Heb 3:18–4:2, Heb 3:12, Psa 78:32, Luk 24:34–41, Psa 78:11–22, Job 9:16
- 26Jhn 20:19, Isa 54:10, Isa 26:12, Mat 17:1, Luk 9:28, Jhn 14:27, Jhn 20:21, Isa 27:5
- 27Jhn 20:25, Psa 103:13–14, 1Jn 1:1–2, Jhn 20:20, Luk 24:40, Psa 78:38, 1Ti 1:14–16, Mat 17:17
- 28Jhn 1:1, Isa 9:6, 1Ti 3:16, Isa 7:14, Mat 14:33, Jhn 5:23, Isa 25:9, Act 7:59–60
- 291Pe 1:8, 2Co 5:7, Heb 11:1, Heb 11:27, Luk 1:45, Jhn 4:48, Jhn 20:8, Heb 11:39
- 30Jhn 21:25, Rom 15:4, 1Jn 5:13, 2Ti 3:15–17, Luk 1:3–4, Jhn 2:11, 2Pe 3:1–2, 1Co 10:11
- 31Act 10:43, Jhn 3:15–16, 1Jn 5:1, 1Jn 4:15, Jhn 3:36, 1Jn 5:20, 1Jn 5:10–13, Jhn 6:40
ข้อความคู่ขนาน
1
- The Empty TombMat 28:1–8, Mrk 16:1–8, Luk 24:1–12, Jhn 20:1–10
Topics in this chapter
37
Angel (A Spirit), Apostles, Art, Backsliders, Burial, Church, Court, Faith, Fraternity, Friendship, God, Holy Spirit, Jesus, the Christ, John, Life, Linen, Love, Mary, Minister, Christian, Miracles, Peace, Persecution, Peter, Rabbi, Salutations, Salvation, Sin, Skepticism, Spear, Thomas, Trinity, Trouble, Unbelief, Vicegerency, Weeping, Women, Word of God