Yohana 18
1 Isa alipomaliza kuomba, akaondoka na wanafunzi wake, wakavuka Bonde la Kidroni. Upande wa pili palikuwa na bustani; yeye na wanafunzi wake wakaingia humo.
2 Basi Yuda, aliyemsaliti, alipafahamu mahali hapo, kwani Isa alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara.
3 Hivyo Yuda akaja kwenye bustani akiongoza kikosi cha askari Warumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha.
4 Isa, akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao, akawauliza, “Mnamtafuta nani?”
5 Wao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.” Isa akawajibu, “Mimi ndiye.” (Yuda, aliyemsaliti, alikuwa amesimama pamoja nao.)
6 Isa alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini!
7 Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Isa Al-Nasiri.”
8 Isa akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”
9 Hii ilikuwa ili litimie lile neno alilosema, “Sikumpoteza hata mmoja miongoni mwa wale ulionipa.”
10 Simoni Petro, aliyekuwa na upanga, akaufuta na kumkata sikio la kuume mtumishi wa kuhani mkuu. (Mtumishi huyo aliitwa Malko.)
11 Isa akamwambia Petro, “Rudisha upanga wako kwenye ala yake. Je, hainipasi kukinywea kikombe alichonipa Baba?”
12 Hivyo wale askari, wakiwa na jemadari wao na maafisa wa Wayahudi, wakamkamata Isa na kumfunga.
13 Kwanza wakampeleka kwa Anasi, mkwewe Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka ule.
14 Kayafa ndiye alikuwa amewashauri viongozi wa Wayahudi kwamba imempasa mtu mmoja kufa kwa ajili ya watu.
15 Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walikuwa wakimfuata Isa. Huyu mwanafunzi mwingine alikuwa anafahamika kwa kuhani mkuu, hivyo aliingia uani kwa kuhani mkuu pamoja na Isa.
16 Lakini Petro alisimama nje karibu na lango. Ndipo yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akazungumza na msichana aliyekuwa analinda lango, akamruhusu Petro aingie ndani.
17 Yule msichana akamuuliza Petro, “Je, wewe pia si mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?” Petro akajibu, “Sio mimi.”
18 Wale watumishi na askari walikuwa wamesimama wakiota moto wa makaa kwa sababu palikuwa na baridi, Petro naye alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
19 Wakati huo kuhani mkuu akawa anamuuliza Isa kuhusu wanafunzi wake na mafundisho yake.
20 Isa akamjibu, “Nimekuwa nikizungumza waziwazi mbele ya watu wote. Siku zote nimefundisha katika masinagogi na Hekaluni, mahali Wayahudi wote hukusanyika. Sikusema jambo lolote kwa siri.
21 Mbona unaniuliza mimi maswali? Waulize wale waliosikia yale niliyowaambia. Wanajua niliyoyasema.”
22 Alipomaliza kusema hayo, mmoja wa askari aliyekuwa amesimama karibu naye akampiga Isa kofi usoni. Kisha akasema, “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu kuhani mkuu?”
23 Isa akamjibu akasema, “Kama nimesema jambo baya, shuhudia huo ubaya niliousema. Lakini kama nimesema yaliyo kweli, mbona umenipiga?”
24 Ndipo Anasi akampeleka Isa kwa kuhani mkuu Kayafa, akiwa bado amefungwa.
25 Wakati huo Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Baadhi ya watu waliokuwepo wakamuuliza, “Je, wewe si mmoja wa wanafunzi wake?” Petro akakana, akasema, “Sio mimi.”
26 Mmoja wa watumishi wa kuhani mkuu, ndugu yake yule mtu ambaye Petro alikuwa amemkata sikio, akamuuliza, “Je, mimi sikukuona kule bustanini ukiwa na Isa?”
27 Kwa mara nyingine tena Petro akakana, naye jogoo akawika wakati huo huo.
28 Ndipo viongozi wa Wayahudi wakamchukua Isa kutoka kwa Kayafa na kumpeleka kwenye jumba la kifalme la mtawala Mrumi. Wakati huo ilikuwa ni alfajiri. Ili kuepuka kuwa najisi kwa taratibu za ibada, Wayahudi hawakuingia ndani ya jumba kwa sababu walitaka kushiriki katika Pasaka.
29 Hivyo Pilato akatoka nje walikokuwa, akawauliza, “Mmeleta mashtaka gani kumhusu mtu huyu?”
30 Wao wakamjibu, “Kama huyu mtu hakuwa mhalifu, tusingemleta kwako.”
31 Pilato akawaambia, “Basi mchukueni ninyi mkamhukumu kwa kufuata sheria zenu.” Wayahudi wakamjibu, “Sisi haturuhusiwi kutoa hukumu ya kifo kwa mtu yeyote.”
32 Walisema hivyo ili yale maneno aliyosema Isa kuhusu kifo atakachokufa yapate kutimia.
33 Kwa hiyo Pilato akaingia ndani ya jumba la kifalme, akamwita Isa, akamuuliza, “Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?”
34 Isa akamjibu, “Je, unauliza swali hili kutokana na mawazo yako mwenyewe, au uliambiwa na watu kunihusu?”
35 Pilato akamjibu, “Je, mimi ni Myahudi? Taifa lako mwenyewe na viongozi wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Umefanya kosa gani?”
36 Isa akajibu, “Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, wafuasi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa viongozi wa Wayahudi. Lakini kama ilivyo, ufalme wangu hautoki hapa ulimwenguni.”
37 Pilato akamuuliza, “Kwa hiyo wewe ni mfalme?” Isa akajibu, “Wewe wasema kwamba mimi ni mfalme. Kwa kusudi hili nilizaliwa, na kwa ajili ya hili nilikuja ulimwenguni: ili niishuhudie kweli. Mtu yeyote aliye wa kweli husikia sauti yangu.”
38 Pilato akamuuliza Isa, “Kweli ni nini?” Baada ya kusema haya Pilato akaenda nje tena, akawaambia wale viongozi wa Wayahudi waliomshtaki Isa, “Sioni msingi wowote wa kumshtaki mtu huyu.
39 Lakini ninyi mna desturi yenu kwamba wakati wa Pasaka nimwachie huru mfungwa mmoja mnayemtaka. Je, mnataka niwafungulie huyu ‘mfalme wa Wayahudi’?”
40 Wao wakapiga kelele, wakajibu, “Si huyu mtu, bali tufungulie Baraba!” Yule Baraba alikuwa mnyang’anyi.
ข้ออ้างอิงโยง
242
- 12Sa 15:23, Mrk 14:32, Mat 26:36, Luk 22:39–40, Jhn 18:26, 2Ki 23:6, 2Ki 23:12, 2Ch 30:14
- 2Luk 22:39, Luk 21:37, Mrk 11:11–12
- 3Jhn 18:12, Luk 22:47–53, Psa 22:12, Psa 3:1–2, Act 1:16, Mat 26:47–56, Jhn 13:2, Jhn 13:27–30
- 4Jhn 13:1, Jhn 18:7, Act 2:28, Psa 27:3, Act 20:22–23, Mat 17:22–23, Pro 28:1, Jhn 19:28
- 5Mat 21:11, Jhn 1:46, Mat 2:23, Jhn 19:19, Jer 8:12, Isa 3:9
- 6Psa 27:2, Psa 70:2–3, 2Ki 1:9–15, Act 4:29–30, Luk 9:54–56, Psa 40:14, Psa 129:5
- 7Jhn 18:4
- 8Jhn 10:28, Jhn 13:1, 2Co 12:9, 1Co 10:13, Mat 26:56, 1Pe 5:7, Isa 53:6, Eph 5:25
- 9Jhn 17:12
- 10Mrk 14:47, Mat 26:51–54, Luk 22:49–51, Jhn 18:26, Luk 22:33, Mrk 14:30
- 11Mat 20:22, Mat 26:39, Jhn 20:17, Jhn 12:27–28, Jhn 15:10, Heb 12:2, Mrk 14:35–36, Luk 22:42
- 12Mat 26:57, Jhn 18:3, Act 22:24–28, Mrk 15:1, Mrk 14:53, Act 21:37, Jdg 16:21, Luk 22:54
- 13Jhn 18:24, Mat 26:3, Jhn 11:51, Mat 26:57, Luk 3:2, Act 4:6
- 14Jhn 11:49–52
- 15Mrk 14:54, Luk 22:54, Mat 26:58–68, Mat 26:3
- 16Mat 26:69, Mrk 14:66–68, Luk 22:55–57
- 17Mat 26:69–70, Mrk 14:66–68, Jhn 18:16, Luk 22:56–57, Jhn 18:25, Luk 22:54, Jhn 21:15, Mat 26:33
- 18Mrk 14:54, Jhn 18:25, Luk 22:55–56, Mrk 14:67, Gen 49:6, Jhn 21:9, Eph 5:11–12, Psa 26:4–10
- 19Luk 20:20, Mat 26:59–68, Mrk 14:55–65, Luk 11:53–54, Luk 22:63–71
- 20Isa 48:16, Jhn 7:26, Mat 4:23, Luk 21:37, Luk 4:15, Mat 9:35, Jhn 7:4, Isa 45:19
- 21Mrk 14:55–59, Act 24:12–13, Luk 22:67, Mat 26:59–60, Act 24:18–20
- 22Luk 22:63–64, Mrk 14:65, Jhn 19:3, Isa 50:5–7, Mat 26:67–68, Job 16:10, Act 23:2–5, Mic 5:1
- 231Pe 2:20–23, 2Co 10:1, Mat 5:39, Act 23:2–5
- 24Jhn 18:13, Mat 26:57
- 25Mrk 14:67–72, Jhn 18:17–18, Gen 18:15, Pro 29:25, Mat 26:71–75, Luk 22:58–62, Mrk 14:37–38, Mat 26:69
- 26Jhn 18:1, Jhn 18:10, Luk 22:59–60, Mat 26:73, Mrk 14:70–71, Pro 12:19
- 27Jhn 13:38, Luk 22:60–62, Mrk 14:71–72, Mat 26:34, Mrk 14:68, Mat 26:74–75, Mrk 14:30, Luk 22:34
- 28Jhn 18:33, Jhn 19:9, Mrk 15:1–5, Mat 27:27, Jhn 19:14, Act 3:13, Mat 27:1–10, Isa 1:10–15
- 29Mat 27:23, Mrk 15:2–5, Mat 27:11–14, Luk 23:2–3, Act 23:28–30, Act 25:16
- 30Luk 20:19–26, Mrk 15:3, Act 3:13, Mrk 10:33, Luk 23:2–5, Luk 24:7, Jhn 19:12
- 31Jhn 19:6–7, Jhn 19:15, Ezk 21:26–27, Act 25:18–20, Hos 3:4–5, Gen 49:10
- 32Mat 26:2, Mat 20:19, Jhn 3:14, Jhn 12:32–33, Luk 18:32–33, Deu 21:23, Jhn 8:28, Mrk 10:33
- 33Luk 23:3–4, Zec 9:9, Act 2:34–36, Mrk 15:2, Luk 19:38–40, Mat 27:11, Jhn 19:12, Jhn 19:3
- 35Jhn 18:28, Act 23:29, Act 3:13, Ezr 4:12, Jhn 19:6, Act 25:19–20, Jhn 19:11, Act 22:22–24
- 36Luk 17:20–21, Col 1:12–14, Jhn 6:15, Rom 14:17, Dan 2:44, Dan 7:14, Zec 9:9, 1Ti 6:13
- 37Jhn 8:47, 1Jn 4:6, Jhn 8:14, Jhn 10:26–27, 1Jn 3:19, Jhn 14:6, Isa 55:4, Jhn 7:17
- 38Jhn 19:4, Luk 23:4, Jhn 19:6, Act 17:32, Mat 27:18–19, Act 24:25–26, Luk 23:14–16, Mrk 15:14
- 39Mat 27:15–18, Luk 23:16–23, Mrk 15:6–14, Mat 27:20–23
- 40Mrk 15:7, Luk 23:18–19, Mat 27:16, Mrk 15:15, Mat 27:26, Luk 23:25, Act 3:13–14
ข้อความคู่ขนาน
3
- The Arrest of JesusMat 26:47–56, Mrk 14:43–52, Luk 22:47–53, Jhn 18:1–11
- Peter's DenialMat 26:69–75, Mrk 14:66–72, Luk 22:54–62, Jhn 18:15–27
- Jesus before PilateMat 27:11–26, Mrk 15:1–15, Luk 23:1–25, Jhn 18:28–40
Topics in this chapter
52
Accusation, False, Afflictions and Adversities, Annas, Arrest, Barabbas, Caiaphas, Captain, Church, Court, Cowardice, Cup, Defilement, Demagogism, Doorkeepers, Faith, Falsehood, Gethsemane, Gospel, Hypocrisy, Indictments, Jerusalem, Jesus, the Christ, John, Judas (Jude), Kidron, Kingdom of Heaven, Lantern, Love, Malchus, Malice, Minister, Christian, Opinion, Public, Passover, Persecution, Peter, Pilate, Pontius, Pleading, Politics, Pretorium, Priest, Prisoners, Prophecy, Resignation, Salvation, Slander, Sword, Synagogue, Temple, Traitor, Truth, Wisdom, Women