1 Wafalme 21
1 Baada ya hayo, pakawa na tukio lililohusisha shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli. Shamba hilo lilikuwa Yezreeli, karibu na jumba la kifalme la Ahabu, mfalme wa Samaria.
2 Ahabu akamwambia Nabothi, “Nipe shamba lako la mizabibu liwe langu, nilime bustani ya mboga kwa kuwa liko karibu na jumba langu. Nitakupa shamba jingine la mizabibu lililo zuri zaidi, au kama utapenda, nitakulipa kulingana na thamani ya shamba lako.”
3 Lakini Nabothi akamjibu, “Mwenyezi Mungu na apishe mbali kukupa wewe urithi wa baba zangu.”
4 Basi Ahabu akaenda nyumbani kwa uchungu na hasira kwa sababu Nabothi Myezreeli alikuwa amemwambia, “Sitakupa urithi wa baba zangu.” Akajinyoosha juu ya kitanda akisononeka, na akakataa kula.
5 Yezebeli mke wake akaingia na akamuuliza, “Kwa nini unahuzunika hivi? Kwa nini huli chakula?”
6 Akamjibu, “Kwa sababu nilimwambia Nabothi Myezreeli, ‘Niuzie shamba lako la mizabibu, au ukipenda, nitakupa shamba jingine la mizabibu badala yake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’ ”
7 Yezebeli mke wake akamuuliza, “Hivi ndivyo unavyofanya, nawe ni mfalme wa Israeli yote? Inuka na ule! Changamka. Nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.”
8 Kwa hiyo akaandika barua kwa jina la Ahabu, akaweka muhuri wa Ahabu juu ya hizo barua; kisha akazituma kwa wazee na kwa watu wenye vyeo walioishi na Nabothi katika mji wake.
9 Katika barua hizo aliandika: “Tangazeni siku ya watu kufunga, na mkamketishe Nabothi mbele ya watu.
10 Waketisheni walaghai wawili mkabala naye, nao washuhudie dhidi yake kuwa amemlaani Mungu na mfalme pia. Kisha mtoeni nje na kumpiga kwa mawe hadi afe.”
11 Hivyo wazee na watu wenye vyeo walioishi katika mji wa Nabothi wakafanya kama Yezebeli alivyoelekeza katika barua alizowaandikia.
12 Wakatangaza mfungo na kumketisha Nabothi mbele ya watu.
13 Kisha walaghai wawili wakaja wakaketi mkabala naye; nao wakaleta mashtaka dhidi ya Nabothi mbele ya watu, wakisema, “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme pia.” Kwa hiyo wakamtoa nje na kumpiga kwa mawe hadi akafa.
14 Kisha wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, kusema, “Nabothi amepigwa mawe na amekufa.”
15 Mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa mawe na amekufa, akamwambia Ahabu, “Amka na umiliki lile shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli, ambalo alikataa kukuuzia. Hayuko hai tena, bali amekufa.”
16 Ahabu aliposikia Nabothi amekufa, akainuka, kisha akashuka kwenda kulimiliki shamba la mizabibu la Nabothi.
17 Kisha neno la Mwenyezi Mungu likamjia Ilya Mtishbi, kusema:
18 “Shuka ukakutane na Ahabu mfalme wa Israeli, anayetawala Samaria. Sasa yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ambalo ameenda kulimiliki.
19 Umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu: Je, hujamuua mtu na kuitwaa mali yake?’ Kisha umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi Mungu: Mahali mbwa walipoiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako pia; naam, yako wewe!’ ”
20 Ahabu akamwambia Ilya, “Kwa hiyo umenipata, wewe adui yangu!” Akajibu, “Ndiyo, nimekupata. Kwa sababu umejiuza mwenyewe kwa kufanya uovu mbele za macho ya Mwenyezi Mungu.
21 ‘Nitaleta maafa juu yako. Nitaangamiza uzao wako na kukatilia mbali kila mwanaume wa jamaa ya Ahabu katika Israeli, awe mtumwa au mtu huru.
22 Nitaifanya nyumba yako kuwa kama ile ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa sababu umenighadhibisha kwa kusababisha Israeli kutenda dhambi.’
23 “Pia Mwenyezi Mungu anasema kumhusu Yezebeli: ‘Mbwa watamla Yezebeli karibu na ukuta wa Yezreeli.’
24 “Mbwa watawala wale wa nyumba ya Ahabu watakaofia mjini, nao wale watakaofia mashambani wataliwa na ndege wa angani.”
25 (Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni pa Mwenyezi Mungu, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.
26 Alitenda uovu sana kwa kuzifuata sanamu, kama Waamori ambao Mwenyezi Mungu aliowafukuza mbele ya Israeli.)
27 Ahabu aliposikia maneno haya, akararua nguo zake, akavaa gunia na kufunga. Akalala na kujifunika gunia na kwenda kwa unyenyekevu.
28 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu lilipomjia Ilya Mtishbi kusema,
29 “Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele zangu? Kwa kuwa amejishusha mwenyewe, sitaleta maafa haya wakati akiwa hai, lakini nitayaleta juu ya nyumba yake katika siku za mwanawe.”
Références croisées
187
- 1Jos 19:18, Jdg 6:33, 2Ch 28:22, 1Ki 18:45–46, Hos 1:4–5, 1Sa 29:1, Jer 5:3, Isa 9:13
- 21Sa 8:14, Jas 1:14–15, 1Ti 6:9, Gen 16:6, Ecc 2:5, 1Sa 8:6, Hab 2:9–11, Sng 4:15
- 3Num 36:7, Lev 25:23, Ezk 46:18, Gal 6:14, Gen 44:7, Job 27:5, Rom 3:6, Gen 44:17
- 41Ki 20:43, Jas 1:14, Isa 57:20–21, Gen 4:5–8, 1Ki 21:3, Hab 2:9–12, Eph 4:27, 2Sa 13:4
- 5Neh 2:2, 1Ki 18:4, 1Ki 19:2, 2Sa 13:4, Gen 3:6, Est 4:5, 1Ki 21:25, 1Ki 16:31
- 6Est 6:12, Jas 4:2–7, 1Ti 6:9–10, Pro 14:30, Est 5:9–14, 1Ki 21:2–4
- 71Sa 8:14, Pro 30:31, Mic 2:1–2, Ecc 8:4, 1Sa 8:4, 1Ki 21:15–16, Mic 7:3, 2Sa 13:4
- 82Sa 11:14–15, Est 8:8–13, Ezr 4:11, 2Ki 10:11, Deu 21:1–9, Ezr 4:7–8, Deu 16:18–19, Neh 6:5
- 9Luk 20:47, Mat 23:13, Mat 2:8, Isa 58:4, Jhn 18:28, Gen 34:13–17
- 10Exo 22:28, Act 6:11, Lev 24:15–16, Deu 19:15, Deu 13:13, Jdg 19:22, Mat 26:59–66, Act 6:13
- 111Sa 23:20, Exo 1:17, Lev 19:15, Mat 2:12, Mat 2:16, Hos 5:11, Mic 6:16, Pro 29:12
- 12Isa 58:4, 1Ki 21:8–10
- 132Ki 9:26, Exo 20:16, Deu 21:21, Isa 8:21, Deu 13:10, Pro 25:18, Pro 19:5, Act 24:5
- 142Sa 11:14–24, Ecc 8:14, Ecc 5:8
- 15Pro 1:10–16, 1Ki 21:7, Pro 4:17
- 162Sa 1:13–16, Rom 1:32, 2Pe 2:15, Isa 33:15, 2Sa 23:15–17, Psa 50:18, 2Sa 11:25–27, Oba 1:12–14
- 17Psa 9:12, 2Ki 5:26, 2Ki 1:15–16, Isa 26:21
- 182Ch 22:9, 1Ki 13:32
- 191Ki 22:38, 2Sa 12:9, Mat 7:2, Est 7:10, Psa 9:16, Mic 3:1–4, 2Ki 9:25–26, Hab 2:9
- 20Rom 7:14, 2Ki 17:17, 1Ki 21:25, 1Ki 18:17, Isa 52:3, Rev 11:10, 1Ki 22:8, Isa 50:1
- 211Ki 14:10, 2Ki 10:1–7, 2Ki 14:26, 1Sa 25:22, Exo 20:5–6, 2Ki 10:17, 2Ki 10:30, 1Sa 25:34
- 221Ki 16:3, 1Ki 14:16, 1Ki 16:11, 1Ki 12:30, 1Ki 15:34, 1Ki 15:29–30, 1Ki 16:26
- 232Ki 9:10, 2Ki 9:30–37, 1Ki 21:25
- 241Ki 16:4, 1Ki 14:11, Jer 15:3, Isa 14:19, Rev 19:18, Ezk 32:4–5, Ezk 39:18–20
- 25Pro 22:14, 1Ki 21:20, 1Ki 16:30–33, Ecc 7:26, 1Ki 21:7, Rom 6:19, Act 14:2, 2Ki 17:17
- 262Ki 21:11, Gen 15:16, Lev 18:25–30, Ezk 18:12, Lev 20:22–23, 1Ki 15:12, Ezr 9:11–14, Jer 16:18
- 272Ki 6:30, Gen 37:34, 2Sa 3:31, 2Sa 12:16–17, Isa 58:5–8, Jol 1:13, Job 16:15, 2Ki 18:37
- 292Pe 3:9, Mic 7:18, 2Ki 9:25–26, Psa 86:15, 2Ki 9:33–10:7, 2Ki 10:11, Psa 18:44, Ezk 33:10–11
Thèmes dans ce chapitre
47
Accusation, False, Afflictions and Adversities, Ahab, Amorites, Anger, Baasha, Blasphemy, Character, Children, Confiscation, Conspiracy, Covetousness, Dishonesty, Dog (Sodomite?), Elijah, Falsehood, False Teachers, Fasting, Forgery, Government, Grape, Homicide, Humility, Indictments, Inheritance, Jezebel, Jezreel, Judge, Judgments, King, Money, Naboth, Palace, Perjury, Property, Prophecy, Punishment, Repentance, Reproof, Rulers, Seal, Slander, Stoning, Usurpation, Wicked (People), Wife, Women