Ezekieli 33
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, sema na watu wako uwaambie, ‘Nitakapoleta upanga dhidi ya nchi, nao watu wa nchi wakamchagua mmoja wa watu wao na kumfanya awe mlinzi wao,
3 naye auonapo upanga unakuja dhidi ya nchi na kupiga tarumbeta kuonya watu,
4 kama mtu yeyote asikiapo sauti ya tarumbeta hatakubali kuonywa, basi upanga ujapo na kuutoa uhai wake, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
5 Kwa kuwa alisikia sauti ya tarumbeta lakini hakukubali maonyo, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe. Kama angekubali maonyo, angejiokoa mwenyewe.
6 Lakini kama mlinzi akiona upanga unakuja na asipige tarumbeta kuonya watu na upanga ukija na kutoa uhai wa mmoja wao, yule mtu ataondolewa kwa sababu ya dhambi yake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwa mlinzi huyo.’
7 “Mwanadamu, nimekufanya wewe kuwa mlinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo na uwape maonyo kutoka kwangu.
8 Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Ewe mtu mwovu, hakika utakufa,’ nawe hukusema neno la kumwonya ili atoke katika njia zake, yule mtu mwovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini mimi nitaitaka damu yake mkononi mwako.
9 Lakini kama utamwonya huyo mtu mwovu aache njia zake mbaya naye hafanyi hivyo, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini utakuwa umejiokoa mwenyewe.
10 “Mwanadamu, sema na nyumba ya Israeli uwaambie, ‘Hili ndilo mnalosema: “Makosa yetu na dhambi zetu zimetulemea, nasi tunadhoofika kwa sababu ya hayo. Tutawezaje basi kuishi?” ’
11 Waambie, ‘Hakika kama mimi niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, sifurahii kifo cha watu waovu, bali kwamba wageuke kutoka njia zao mbaya wapate kuishi. Geukeni! Geukeni kutoka njia zenu mbaya! Kwa nini mkafe, ee nyumba ya Israeli?’
12 “Kwa hiyo, mwanadamu, waambie watu wako, ‘Haki ya mtu mwenye haki haitamwokoa wakati anapoacha kutii, wala uovu wa mtu mwovu hautamsababisha yeye kuanguka anapotubu na kuacha uovu. Mtu mwenye haki akitenda dhambi, hataishi kwa sababu ya uadilifu wake wa awali.’
13 Nikimwambia mtu mwenye haki kwamba hakika ataishi, lakini akategemea hiyo haki yake na kutenda uovu, hakuna tendo lolote la haki alilotenda litakalokumbukwa; atakufa kwa ajili ya uovu alioutenda.
14 Nami nikimwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ kisha akageuka kutoka dhambi yake na kufanya lile lililo haki na sawa,
15 kama akirudisha kile alichochukua rehani kwa ajili ya deni, akarudisha alichoiba na kufuata amri zile ziletazo uzima, wala hafanyi uovu, hakika ataishi, hatakufa.
16 Hakuna dhambi yoyote aliyoitenda itakayokumbukwa juu yake. Ametenda lile lililo haki na sawa, hakika ataishi.
17 “Lakini watu wako wanasema, ‘Njia ya Bwana si sawa.’ Lakini ni njia zao ambazo si sawa.
18 Kama mtu mwenye haki akigeuka kutoka uadilifu wake na kufanya uovu, atakufa kwa ajili ya huo uovu.
19 Naye mtu mwovu akigeuka kutoka uovu wake na kufanya lile lililo haki na sawa, kwa kufanya hivyo ataishi.
20 Lakini, ee nyumba ya Israeli, unasema, ‘Njia ya Bwana si sawa.’ Lakini nitamhukumu kila mmoja wenu sawasawa na njia zake mwenyewe.”
21 Mwaka wa kumi na mbili wa uhamisho wetu, mwezi wa kumi, siku ya tano, mtu aliyekuwa ametoroka kutoka Yerusalemu akanijia na kusema, “Mji wa Yerusalemu umeanguka!”
22 Basi jioni kabla mtu huyo hajaja, mkono wa Mwenyezi Mungu ulikuwa juu yangu, naye alifungua kinywa changu kabla ya mtu yule aliyenijia asubuhi hajafika. Basi kinywa changu kilifunguliwa na sikuweza tena kunyamaza.
23 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
24 “Mwanadamu, watu wanaoishi katika magofu hayo katika nchi ya Israeli wanasema hivi, ‘Ibrahimu alikuwa mtu mmoja tu, hata hivyo akaimiliki nchi. Lakini sisi ni wengi, hakika tumepewa nchi kuwa milki yetu.’
25 Kwa hiyo waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa kuwa mnakula nyama ikiwa na damu, na kuinulia sanamu zenu macho na kumwaga damu, je, mtaimiliki nchi?
26 Mnategemea panga zenu, mnafanya mambo ya machukizo na kila mmoja wenu humnajisi mke wa jirani yake. Je, mtaimiliki nchi?’
27 “Waambie hivi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Hakika kama niishivyo, wale waliobaki katika magofu wataanguka kwa upanga, wale walio nje mashambani nitawatoa wararuliwe na wanyama pori, nao wale walio katika ngome na kwenye mapango watakufa kwa tauni.
28 Nitaifanya nchi ukiwa, na kiburi cha nguvu zake kitafikia mwisho, nayo milima ya Israeli itakuwa ukiwa ili mtu yeyote asipite huko.
29 Kisha watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapokuwa nimeifanya nchi ukiwa kwa sababu ya mambo yote ya machukizo waliyotenda.’
30 “Kwako wewe, mwanadamu, watu wako wanaongea habari zako wakiwa karibu na kuta na kwenye milango ya nyumba, wakiambiana kila mmoja na mwenzake, ‘Njooni msikie ujumbe ule unaotoka kwa Mwenyezi Mungu.’
31 Watu wangu wanakujia, kama wafanyavyo, nao wanaketi mbele yako kama watu wangu na kusikiliza maneno yako, lakini hawayatendi. Kwa maana udanganyifu u katika midomo yao, lakini mioyo yao ina tamaa ya faida isiyo halali.
32 Naam, mbele yao umekuwa tu kama yeye aimbaye nyimbo za mapenzi kwa sauti nzuri za kuvutia na kupiga vyombo kwa ustadi, kwa kuwa wanasikia maneno yako lakini hawayatendi.
33 “Mambo haya yote yatakapotimia, kwa kuwa hakika yatatokea, ndipo watajua kuwa nabii amekuwa miongoni mwao.”
Références croisées
230
- 2Ezk 33:30, Ezk 14:17, Ezk 33:17, Ezk 3:11, Ezk 3:27, Jer 15:2–3, Zec 13:7, Isa 62:6
- 3Hos 8:1, Neh 4:20, Jer 4:5, Jol 2:1, Isa 58:1, Neh 4:18, Jer 6:1, Ezk 33:8–9
- 4Ezk 18:13, Act 18:6, Jer 6:17, Ezk 33:9, 2Ch 25:16, Zec 1:2–4, Ezk 33:5, Act 20:26
- 5Heb 11:7, Exo 9:19–21, Jhn 8:39, Isa 51:2, 2Ki 6:10, Act 2:37–41, Heb 2:1–3, Psa 95:7
- 6Ezk 3:18–20, Ezk 33:8–9, Gen 42:22, 2Sa 4:11, Ezk 18:20, Gen 9:5, Ezk 34:10, Ezk 18:24
- 7Jer 26:2, Ezk 3:17–21, Ezk 2:7–8, Heb 13:17, Act 5:20, Jer 1:17, Isa 62:6, 1Th 4:1–2
- 8Act 20:26–27, Ezk 33:6, Ezk 33:14, Ezk 18:4, Gen 3:4, Ezk 18:20, Isa 3:11, Ezk 18:18
- 9Ezk 3:19, Act 20:26, Pro 15:10, Ezk 3:21, 1Th 4:3–8, Luk 12:47, Eph 5:3–6, Php 3:18–19
- 10Isa 49:14, Ezk 37:11, Lev 26:39, Ezk 24:23, Ezk 4:17, Jer 2:25, Psa 130:7, Isa 51:20
- 111Ti 2:4, Ezk 18:23, 2Pe 3:9, Isa 55:6–7, Act 3:19, Pro 8:36, Ezk 18:30–32, Jer 3:22
- 122Ch 7:14, Ezk 33:18–19, Rom 3:25, Ezk 33:2, 1Ki 8:48–50, 1Jn 2:1, Mat 21:28–31, Ezk 18:24–32
- 13Ezk 18:24, Heb 10:38, Ezk 18:4, Luk 18:9–14, Ezk 3:20, 2Pe 2:20–22, 1Jn 2:19, Rom 10:3
- 14Ezk 18:27, Hos 14:1, Ezk 33:8, Isa 55:7, Jer 18:7–8, Mic 6:8, Pro 28:13, Luk 13:3–5
- 15Ezk 20:11, Luk 19:8, Exo 22:1–4, Psa 119:93, Ezk 18:7, Lev 18:5, Lev 6:2–5, Ezk 20:13
- 16Isa 43:25, Ezk 18:22, Mic 7:18–19, Isa 44:22, Isa 1:18, Rom 5:16, 1Jn 2:1–3, Rom 5:21
- 17Ezk 18:29, Ezk 18:25, Mat 25:24–26, Job 35:2, Job 40:8, Luk 19:21–22, Ezk 33:20
- 18Ezk 33:12–13, Heb 10:38, 2Pe 2:20–22, Ezk 18:26–27, Ezk 3:20
- 19Ezk 18:27–28, Ezk 33:14
- 20Mat 16:27, Ezk 18:25, Rev 22:12, Ezk 33:17, Psa 62:12, Ezk 18:29–30, Rev 20:12–15, Jhn 5:29
- 21Ezk 1:2, Ezk 32:1, Jer 52:4–14, 2Ch 36:17–21, Ezk 24:26–27, 2Ki 24:4–7, 2Ki 25:4, Jer 39:1–8
- 22Ezk 1:3, Ezk 24:26–27, Ezk 3:26–27, Ezk 37:1, Ezk 3:22, Ezk 40:1, Luk 1:64
- 24Isa 51:2, Ezk 33:27, Act 7:5, Ezk 36:4, Luk 3:8, Jer 40:7, Jer 39:10, Rom 4:12
- 25Jer 7:9–10, Deu 12:16, Gen 9:4, Ezk 18:6, Ezk 22:6, Ezk 22:27, Lev 3:17, Jer 44:15–19
- 26Zep 3:3, Mic 2:1–2, Gen 27:40, Lev 20:13, Lev 18:25–30, Deu 29:18–23, Deu 4:25–26, Rev 21:27
- 271Sa 13:6, Jer 42:22, Ezk 39:4, Jer 15:2–4, Isa 2:19, 1Sa 24:3, Jer 44:12, 1Sa 22:1
- 28Ezk 7:24, Mic 7:13, Ezk 24:21, Jer 44:22, Ezk 6:14, Jer 44:6, Jer 44:2, Ezk 30:6–7
- 29Ezk 6:7, Ezk 8:6–15, Psa 83:17–18, Jer 5:1–9, Zep 3:1–4, Ezk 23:49, 2Ch 36:14–17, Ezk 6:11
- 30Isa 29:13, Isa 58:2, Mat 22:16–17, Mat 15:8, Jer 23:35, Jer 42:20, Jer 11:18–19, Jer 18:18
- 31Mat 13:22, Psa 78:36–37, Jas 1:22–24, Isa 29:13, Luk 11:28, Jas 2:14–16, Luk 6:48–49, Jer 44:16
- 32Mrk 6:20, Jhn 5:35, Mrk 4:16–17
- 33Jer 28:9, Ezk 2:5, 1Sa 3:19–20, 2Ki 5:8, Ezk 33:29, Luk 10:11
Thèmes dans ce chapitre
51
Abraham, Adultery, Affections, Apostasy, Armies, Backsliders, Blasphemy, Blood, Cave, Condescension of God, Contingencies, Conviction, Covetousness, Death, Ezekiel, God, Harp, Hearers, Hypocrisy, Ignorance, Impenitence, Infidelity, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Judgment, Judgments, Minister, Christian, Music, Obedience, Opportunity, Pawn, Penitent, Prophecy, Prophets, Remorse, Repentance, Responsibility, Restitution, Righteousness, Robbery, Scoffing, Self-Righteousness, Sin, Supererogation, Surety (Guarantee), Symbols and Similitudes, Trumpet, War, Watchman, Wicked (People), Works