1 Timotheo 6
1 Wale wote walio chini ya nira ya utumwa inawapasa kuwahesabu mabwana zao kuwa wanastahili heshima yote, ili jina la Mungu lisitukanwe wala mafundisho yetu.
2 Wale watumwa ambao wana mabwana waaminio, haiwapasi kupunguza heshima yao kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie hata vizuri zaidi, kwa sababu wale wanaonufaika na huduma yao ni waumini, ambao ni wapendwa wao. Fundisha mambo haya na uwahimize kuyafuata.
3 Ikiwa mtu yeyote atafundisha mafundisho mapotovu wala hakubaliani na mafundisho manyofu ya Bwana wetu Isa Al-Masihi na yale ya utauwa,
4 huyo anajivuna wala hajui kitu chochote. Yeye amejaa tamaa ya mabishano na ugomvi kuhusu maneno ambavyo matokeo yake ni wivu na mapigano, maneno ya ukorofi, shuku mbaya,
5 na kuzozana kusikokoma kati ya watu walioharibika akili zao, walioikosa kweli, na ambao hudhani kwamba utauwa ni njia ya kupata faida.
6 Lakini utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
7 Kwa kuwa hatukuja humu duniani na kitu chochote, wala hatuwezi kutoka humu na kitu.
8 Lakini kama tuna chakula na mavazi, tutaridhika navyo.
9 Lakini wale watu wanaotamani kuwa na mali kwa haraka huanguka kwenye majaribu, na wamenaswa na tamaa nyingi za kipumbavu zenye kudhuru, zinazowazamisha watu katika uharibifu na maangamizi.
10 Kwa maana kupenda fedha ndiyo shina moja la maovu ya kila namna. Baadhi ya watu wakitamani fedha, wameiacha imani na kujichoma wenyewe kwa maumivu mengi.
11 Lakini wewe, mtu wa Mungu, yakimbie mambo haya yote. Fuata haki, utauwa, imani, upendo, saburi na upole.
12 Pigana vile vita vizuri vya imani. Shika uzima wa milele ambao ndio ulioitiwa ulipokiri ule ukiri mzuri mbele ya mashahidi wengi.
13 Nakuagiza mbele za Mungu avipaye vitu vyote uhai, na mbele za Al-Masihi Isa, ambaye alipokuwa anashuhudia mbele ya Pontio Pilato alikiri ukiri mzuri,
14 uishike amri hii bila dosari wala lawama hadi kufunuliwa kwake Bwana wetu Isa Al-Masihi;
15 ambako Mungu atadhihirisha kwa wakati wake mwenyewe: Mungu ahimidiwaye, aliye peke yake Mtawala, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana,
16 yeye pekee aishiye milele, anayedumu katika nuru isiyoweza kukaribiwa, ambaye hakuna mwanadamu aliyemwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye milele. Amen.
17 Waagize wale ambao ni matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke tumaini lao katika mali ambayo si ya hakika, bali waweke tumaini lao katika Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie.
18 Waagize watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, pia wawe wakarimu na walio tayari kushiriki mali yao na wengine.
19 Kwa njia hii watajiwekea hazina kama msingi kwa ajili ya wakati ujao na hivyo watajipatia uzima, yaani ule uzima ambao ni wa kweli.
20 Timotheo, linda kile kilichowekwa amana kwako. Epuka majadiliano yasiyo ya utauwa na mabishano ambayo kwa uongo huitwa elimu,
21 ambayo wengine kwa kujidai kuwa nayo wameiacha imani. Neema iwe nanyi. Amen.
Références croisées
166
- 11Pe 2:17–20, Eph 6:5–8, Tit 2:8–10, Tit 2:5, 1Co 7:21–22, Rom 2:24, Col 3:22–25, Mal 1:6
- 2Col 4:1, 1Ti 4:11, Gen 16:4–5, Mat 25:40, Col 1:4, 1Pe 5:1, 2Th 1:3, Jol 2:28
- 31Ti 1:3, 1Ti 1:10, Rom 16:17, Tit 1:9, 2Ti 4:3, 1Th 4:8, 1Ti 1:6, 2Ti 1:13
- 42Ti 2:23, 2Ti 3:4, 1Ti 3:6, 2Ti 2:14, Jud 1:10, 2Pe 2:12, Jud 1:16, 1Ti 1:7
- 52Ti 3:5, 2Pe 2:3, Tit 1:11, 2Ti 3:8, Tit 1:15–16, Rom 16:17–18, 1Ti 6:6, Mat 12:33
- 6Heb 13:5, 1Ti 6:8, Pro 16:8, Php 4:11–13, Luk 12:31–32, Php 1:21, Pro 15:16, 1Ti 4:8
- 7Job 1:21, Psa 49:17, Luk 12:20–21, Ecc 5:15–16, Pro 27:24, Luk 16:22–23
- 8Heb 13:5–6, Mat 6:11, Mat 6:25–33, Pro 30:8–9, Gen 28:20, Deu 2:7, Ecc 3:12–13, Pro 27:23–27
- 91Jn 2:15–17, Pro 15:27, Pro 28:20–22, 1Ti 3:7, Act 8:20, Mrk 4:19, 2Pe 2:3, Eph 4:22
- 10Pro 1:19, 1Ti 6:9, Psa 32:10, Pro 1:31, Tit 1:11, Mic 3:11, Isa 56:11, Jud 1:11
- 112Ti 2:22, 1Ti 4:12, 2Ti 3:17, Heb 12:14, 2Pe 1:5–7, Php 4:8–9, 1Co 10:14, Psa 34:14
- 121Pe 5:10, 1Ti 1:18, 1Co 9:25–26, 2Ti 4:7, Eph 6:10–18, Php 3:12–14, Rev 3:3, 1Ti 6:13
- 13Jhn 18:36–37, Mat 27:11, 1Ti 5:21, Rev 3:14, Rev 1:5, Jhn 5:21, 1Ti 6:12, Act 17:25
- 142Pe 3:14, 1Pe 1:7, 1Th 5:23, Php 1:10, Tit 2:13, Heb 9:28, Jud 1:24, 2Th 2:8
- 15Rev 19:16, Rev 17:14, 1Ti 1:17, Psa 47:2, Jer 10:10, 1Ti 1:11, Dan 2:44–47, Jer 46:18
- 161Ti 1:17, Jhn 1:18, 1Jn 1:5, Col 1:15, Psa 90:2, Jhn 6:46, Isa 57:15, Psa 104:2
- 17Pro 11:28, Act 14:17, Mat 19:23, Jas 1:9–10, Pro 27:24, 1Ti 4:10, Jer 9:23–24, Jer 17:7–8
- 18Heb 13:16, 1Jn 3:17, Psa 37:3, Rom 12:8, Tit 2:14, Luk 12:21, Pro 11:24–25, Tit 3:8
- 19Mat 6:19–21, 1Ti 6:12, 2Ti 2:19, Luk 16:9, 1Pe 1:4, Pro 31:25, Gal 6:8–9, Php 3:14
- 20Col 2:8, 2Ti 2:16, 2Ti 1:12–14, Col 2:18, Rom 3:2, 2Ti 3:14–16, 1Ti 6:14, 2Th 2:15
- 212Ti 2:18, Rom 16:20, Rom 16:23, 1Ti 1:19, Tit 3:15, Col 4:18, 1Ti 1:6, Rom 1:7
Thèmes dans ce chapitre
59
Agency, Alms, Avarice, Backsliders, Benedictions, Beneficence, Church, Commandments, Company, Confidence, Contentment, Covetousness, Death, Decision, Doctrines, Envy, Faith, Fellowship, Fight of Faith, Gifts From God, God, Gospel, Holiness, House, Immortality, Influence, Jesus, the Christ, Liberality, Life, Light, Love, Lust, Meekness, Minister, Christian, Money, Obedience, Patience, Philosophy, Pilate, Pontius, Power, Preaching, Pride, Quickening, Railing, Responsibility, Rich, the, Riches, Science, Servant, Strife, Temptation, Testimony, Timothy, Truth, Vanity, War, Wisdom, Word of God, Works