Marko 14
1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa Torati walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Isa kwa hila na kumuua.
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
3 Isa alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Isa.
4 Baadhi ya watu waliokuwa pale walikasirika na wakasemezana, “Upotevu huu wote wa manukato ni wa nini?
5 Manukato haya yangeuzwa kwa zaidi ya dinari mia tatu, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
6 Lakini Isa akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Isa kwao.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Isa wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
15 Atawaonesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Isa alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
17 Ilipofika jioni, Isa akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
18 Walipoketi mezani wakila, Isa akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi, Bwana?”
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
22 Walipokuwa wanakula, Isa akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu.”
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
27 Isa akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “ ‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
30 Isa akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Isa akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
43 Isa alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa Torati, na wazee.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
45 Mara Yuda akamjia Isa na kusema, “Mwalimu.” Akambusu.
46 Wale watu wakamkamata Isa, wakamweka chini ya ulinzi.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
48 Kisha Isa akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang’anyi?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
51 Kijana mmoja, aliyekuwa amevaa nguo ya kitani pekee, alikuwa akimfuata Isa. Walipomkamata,
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
53 Wakampeleka Isa kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa Torati wote wakakusanyika pamoja.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Isa ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’ ”
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Isa, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
61 Lakini Isa akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Al-Masihi, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
62 Isa akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
63 Kuhani mkuu akayararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
64 Ninyi mmesikia alivyokufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini uani, tazama akaja mmoja wa wajakazi wa kuhani mkuu.
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Isa, Mnasiri.”
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
69 Yule mjakazi alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Isa alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
Marejeleo mtambuka
447
- 1Exo 12:6–20, Luk 22:1–2, Jhn 13:1, Deu 16:1–8, Lev 23:5–7, Act 4:25–28, Mat 12:14, Psa 64:2–6
- 2Pro 21:30, Mrk 11:18, Jhn 12:19, Pro 19:21, Mrk 11:32, Luk 20:6, Mat 26:5, Jhn 7:40
- 3Luk 7:37–39, Jhn 12:1–8, Jhn 11:2, Mat 26:6–13, Sng 4:13–14
- 4Jhn 12:4–5, Mat 26:8–9, Ecc 4:4, Ecc 5:4–8, Mal 1:12–13
- 5Jhn 13:29, Mat 20:11, Jud 1:16, Luk 15:2, Exo 16:7–8, Psa 106:25, Deu 1:27, 1Co 10:10
- 6Tit 3:14, Mat 26:10, Heb 10:24, Heb 13:21, Act 9:36, Tit 2:14, Tit 2:7, Eph 2:10
- 7Deu 15:11, Mat 26:11, Jas 2:14–16, 1Jn 3:16–19, Jhn 17:11, Jhn 12:7–8, Jhn 16:28, Jhn 16:5
- 82Co 8:12, Jhn 12:7, 2Ch 31:20–21, Mrk 15:42–16:1, Luk 23:53–24:3, 2Co 8:1–3, 2Ch 34:19–33, 1Ch 29:1–17
- 9Mrk 16:15, Mat 26:12–13, Mat 24:14, Psa 112:6–9, Zec 6:14, Num 31:54
- 10Luk 22:3–6, Jhn 13:2, Mat 26:14–16, Psa 41:9, Jhn 13:30, Psa 55:12–14, Jhn 6:70–71, Mat 10:4
- 111Ti 6:10, Hos 7:3, Jud 1:11, Luk 22:5–6, Pro 28:21–22, 2Ki 5:26, 2Pe 2:14–15, Mat 26:15
- 12Exo 12:6, Lev 23:5–6, 1Co 5:7–8, Mat 26:17–19, Num 28:16–18, Exo 12:8, Exo 12:18, Gal 4:4
- 13Mat 26:18–19, Luk 22:10–13, Heb 5:9, Jhn 15:14, Mat 8:9, Mrk 11:2–3, Heb 4:13, Luk 19:30–33
- 14Rev 3:20, Jhn 11:28, Jhn 13:13, Mrk 10:17, Mrk 11:3
- 15Act 1:13, Pro 21:1–2, Act 20:8, Psa 110:3, Jhn 2:24–25, Jhn 21:17, Pro 16:1, 2Ch 6:30
- 16Jhn 16:4, Luk 22:13, Luk 22:35
- 17Luk 22:14, Mat 26:20–24, Luk 22:21–23, Jhn 13:21–26
- 18Psa 41:9, Jhn 6:47, Jhn 6:70, Mrk 9:1, Mat 5:18, Mat 6:2, Jhn 3:3, Jhn 5:19
- 19Jhn 13:22, Luk 22:21–23, Mat 26:22
- 20Jhn 13:26, Mrk 14:43, Mat 26:23, Luk 22:47, Mat 26:47, Jhn 6:71
- 21Isa 53:1–12, Mat 26:24–25, Dan 9:24, Zec 13:7, Mat 18:6–7, Act 4:27, Jhn 19:28, Dan 9:26
- 22Mat 26:26–29, Mrk 14:24, 1Co 10:16–17, 1Co 11:23–29, Luk 24:30, Luk 22:18–20, Jhn 6:48–58, Mrk 6:41
- 23Mrk 14:22, Mat 26:27, 1Co 10:16, Luk 22:17, Rom 14:6
- 24Exo 24:8, Zec 9:11, Rev 7:9–17, Heb 9:15–23, Mrk 10:45, Heb 13:20–21, Rev 5:8–10, 1Co 10:16
- 25Mat 26:29, Psa 104:15, Amo 9:13–14, Zec 9:17, Luk 22:16–18, Jol 3:18, Luk 22:29–30
- 26Mat 26:30, Luk 22:39
- 27Zec 13:7, Jhn 16:32, Mat 26:31, Jhn 16:1, 2Ti 4:16, Luk 22:31–32
- 28Mat 28:16, Mrk 16:7, Mat 28:7, Mat 28:10, Mat 26:32, 1Co 15:4–6, Mat 16:21, Jhn 21:1
- 29Luk 22:33–34, Jhn 13:36–38, Mat 26:33–35, Jhn 21:15
- 30Mrk 14:66–72, Jhn 13:38, 1Co 10:12, Mat 26:69–75, Gen 1:8, Luk 22:34, Jhn 18:17, Luk 22:54–62
- 31Jhn 13:37, Exo 19:8, Jer 17:9, Deu 5:27–29, Pro 16:18, Jer 10:23, Pro 18:24, Pro 29:23
- 32Mrk 14:39, Psa 18:5–6, Mrk 14:36, Luk 22:39–46, Mat 26:36–46, Psa 109:4, Psa 88:1–3, Jhn 18:1–11
- 33Luk 22:44, Heb 5:7, Mrk 1:16–19, Mrk 5:37, Psa 88:14–16, Psa 38:11, Psa 69:1–3, Mrk 9:2
- 34Jhn 12:27, Mrk 13:35–37, 1Pe 5:8, Eph 6:18–19, Lam 1:12, 1Pe 4:7, Mrk 14:37–38, Isa 53:3–4
- 35Mrk 14:41, Deu 9:18, Act 10:25–26, Mat 26:39, Heb 5:7, Gen 17:3, 2Ch 7:3, Rev 4:10
- 36Gal 4:6, Rom 8:15–16, Jhn 5:30, Heb 5:7–8, Jhn 12:27, Php 2:8, Mrk 10:27, Jhn 6:38–39
- 37Mat 26:40, Mrk 14:29–31, Mrk 14:40–41, 2Sa 16:17, Heb 12:3, Luk 9:31–32, Luk 22:45–46, Mat 25:5
- 38Mat 26:41, Mat 24:42, Luk 21:36, Rom 7:18–25, Luk 22:40, Rev 3:2–3, Luk 22:46, Gal 5:17
- 39Mat 26:42–44, 2Co 12:8, Mat 6:7, Luk 18:1
- 40Mrk 9:33–34, Rom 3:19, Gen 44:16
- 41Mrk 9:31, Mrk 14:35, Jhn 17:1, 1Ki 22:15, Mrk 14:10, Jhn 7:30, Mrk 14:18, Jhn 12:27
- 42Mat 26:46, Jhn 18:1–2
- 43Luk 22:47–53, Jhn 18:3–11, Mat 26:47–56, Psa 22:11–13, Psa 2:1–2, Act 1:16, Psa 3:1–2
- 44Mat 26:48–50, Pro 27:6, Exo 12:13, Psa 55:20–21
- 45Mal 1:6, Jhn 20:16, Mrk 12:14, Mat 23:7–10, Jhn 13:13–14, Luk 6:46, Isa 1:3
- 46Jdg 16:21, Lam 4:20, Jhn 18:12, Act 2:23
- 47Jhn 18:10–11, Mat 26:51–54, Luk 22:49–51
- 48Luk 22:52–53, 1Sa 26:18, 1Sa 24:14–15, Mat 26:55
- 49Jhn 18:20, Jhn 8:2, Mat 26:54, Mrk 12:35, Luk 24:44–45, Luk 22:37, Dan 9:24–26, Mat 1:22
- 50Mrk 14:27, Jhn 16:32, 2Ti 4:16, Psa 88:18, Psa 38:11, Psa 88:7–8, Jhn 18:8, Job 19:13–14
- 52Mrk 13:14–16, Gen 39:12
- 53Mat 26:57–68, Jhn 18:12–14, Luk 22:54–62, Isa 53:7, Jhn 18:19–24, Mrk 15:1, Mat 26:3, Act 4:5–6
- 54Jhn 18:18, Mat 26:3, Jhn 18:25, Jhn 18:15–16, Mrk 14:67–68, Mrk 14:29–31, Mrk 14:38, 1Ki 19:9
- 55Act 24:1–13, Mat 5:22, 1Pe 3:16–18, Mat 26:59–60, Dan 6:4, 1Ki 21:13, Psa 35:11, Psa 27:12
- 57Mat 26:60–61, Act 6:13–14, Mat 27:40, Mrk 15:29, Jer 26:8–9, Jer 26:18, Jhn 2:18–21
- 58Jhn 2:19, Heb 9:11, 2Co 5:1, Mrk 15:29, Act 7:48, Heb 9:24, Dan 2:34, Dan 2:45
- 60Mat 26:62–63, Mrk 15:3–5, Jhn 19:9–10
- 61Mat 26:63–64, Mrk 15:2, Isa 53:7, Jhn 19:7, Jhn 10:30–31, Luk 22:67–71, Jhn 10:36, 1Pe 2:23
- 62Dan 7:13–14, Psa 110:1, Heb 1:3, Mrk 13:26, Mat 24:30, Luk 22:69, Mat 26:64, Heb 12:2
- 63Mat 26:65, Num 14:6, Isa 36:22–37:1, Lev 21:10, Jer 36:23–24, Act 14:13–14
- 64Lev 24:16, Jhn 19:7, Jhn 10:31–33, Jhn 5:18, Jhn 8:58–59, 1Ki 21:9–13, Mat 26:65–66, Luk 22:71
- 65Mat 26:67–68, Act 23:2, Isa 50:6, Jhn 19:3, Luk 22:63–64, Num 12:14, Job 30:10, Isa 52:14
- 66Mrk 14:54, Mat 26:69–75, Jhn 18:15–18, Jhn 18:25–27, Mat 26:58, Luk 22:55–62
- 67Mrk 14:54, Jhn 19:19, Act 10:38, Mat 2:23, Jhn 1:45–49, Mrk 1:24, Mrk 10:47, Mat 21:11
- 68Mrk 14:29–31, 2Ti 2:12–13, Jhn 13:36–38, Mrk 14:72, Mat 26:71–72
- 69Jhn 18:17, Jhn 18:25, Gal 6:1, Luk 22:58, Mrk 14:38
- 70Luk 22:59–60, Mat 26:73–74, Mrk 14:68, Act 2:7, Jhn 18:26–27, Jdg 12:6
- 71Jer 17:9, 2Ki 8:12–15, 1Co 10:12, 2Ki 10:32
- 72Mrk 14:30, Mrk 14:68, Ezk 7:16, Jer 31:18–20, 2Co 7:10, Mat 26:74–75, Psa 119:59–60, Ezk 16:63
Vifungu sambamba
5
- The Anointing at BethanyMat 26:6–13, Mrk 14:3–9, Jhn 12:1–8
- The Last SupperMat 26:26–30, Mrk 14:22–26, Luk 22:14–23
- The Agony in GethsemaneMat 26:36–46, Mrk 14:32–42, Luk 22:39–46
- The Arrest of JesusMat 26:47–56, Mrk 14:43–52, Luk 22:47–53, Jhn 18:1–11
- Peter's DenialMat 26:69–75, Mrk 14:66–72, Luk 22:54–62, Jhn 18:15–27
Mada katika sura hii
94
Abba, Accusation, False, Afflictions and Adversities, Alabaster, Anointing, Apostasy, Apostles, Arrest, Assault and Battery, Backsliders, Betrayal, Blasphemy, Blood, Box, Bribery, Chiding, Church, Cock Crowing, Confidence, Conscience, Court, Covetousness, Cowardice, Craftiness, Cup, Deception, Eucharist (the Lord's Supper), Falsehood, False Teachers, Frugality, Galilee, Gethsemane, God, Government, House, Indictments, James, Jesus, the Christ, John, Judas (Jude), Judgment, Leprosy, Malchus, Man, Mary, Master, Millennium, Mocking, Money, Music, Oath, Ointment, Olives, Mount of, Passover, Penny, Perjury, Persecution, Peter, Poor, Praise, Prayer, Predestination, Presumption, Priest, Prisoners, Prophecy, Quotations and Allusions, Rabbi, Repentance, Resignation, Scribe (S), Self-Examination, Servant, Sheep, Shepherd, Silver, Simon, Slander, Song, Sorrow, Spikenard, Staves (Long Poles), Submission, Symbols and Similitudes, Temple, Temptation, Testament, Traitor, Weeping, Wicked (People), Will, Wine, Women, Zeal, Religious