Amosi 9
1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna yeyote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 Wajapojichimbia chini hadi kwenye vina vya Kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha.
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wanaoishi ndani yake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Mto Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya nchi: Mwenyezi Mungu ndilo jina lake.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Mwenyezi Mungu. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 “Hakika macho ya Bwana Mungu Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Mwenyezi Mungu.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 “Katika siku ile “Nitalisimamisha hema la Daudi lililoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Mwenyezi Mungu ambaye atafanya mambo haya.
13 “Siku zinakuja,” asema Mwenyezi Mungu, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani yake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatang’olewa tena kutoka nchi niliyowapa,” asema Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.
Marejeleo mtambuka
113
- 1Psa 68:21, Jhn 1:18, Hab 3:13, Amo 3:14, Rev 1:17, Isa 6:3–4, Isa 6:1, Ezk 9:2
- 2Psa 139:7–10, Jer 51:53, Oba 1:4, Luk 10:18, Isa 14:13–16, Jer 49:16, Ezk 28:13–16, Isa 2:19
- 3Jer 16:16, Job 34:22, Isa 27:1, Jer 23:23–24, Psa 139:9–11, Amo 1:2
- 4Lev 26:33, Jer 21:10, Jer 44:11, Lev 17:10, Deu 28:63–65, Ezk 5:12, Jer 39:16, Zec 13:8–9
- 5Amo 8:8, Psa 46:6, Isa 64:1, Rev 20:11, Mic 1:3–4, Hab 3:10, Psa 32:6, Hos 4:3
- 6Amo 5:8, Psa 104:3, Amo 4:13, Psa 104:13, Jer 5:22, Gen 2:1, Gen 7:11–19, Exo 3:14–15
- 7Jer 47:4, Deu 2:23, 2Ki 16:9, Amo 2:10, Amo 1:5, Jer 9:25–26, Isa 22:6, Hos 12:13
- 8Jer 30:11, Amo 9:4, Jer 44:27, Jer 5:10, Deu 4:31, Jol 2:32, Psa 11:4–6, Jer 33:24–26
- 9Luk 22:31, Deu 28:64, Isa 30:28, Lev 26:33
- 10Amo 6:3, Mat 13:49–50, Isa 33:14, Mat 3:10–12, Mat 13:41–42, Mal 4:1, Isa 56:12, Mal 3:15
- 11Act 15:15–17, Jer 33:14–16, Isa 16:5, Jer 23:5–6, Psa 80:12, Jer 46:26, Isa 63:11, Hos 3:5
- 12Isa 43:7, Isa 65:1, Act 15:17, Isa 63:19, Jer 14:9, Dan 9:18–19, Num 24:17–18, Isa 14:1–2
- 13Jol 3:18, Jhn 4:35, Lev 26:5, Isa 55:13, Isa 35:1–2, Ezk 36:35, Hos 2:21–23, Jol 3:20
- 14Isa 61:4, Jer 30:3, Jer 30:18, Ezk 28:26, Jer 31:28, Isa 65:21, Psa 53:6, Ezk 37:25–28
- 15Jer 24:6, Ezk 37:25, Isa 60:21, Ezk 34:28, Jol 3:20, Jer 32:41, Mic 4:4
Mada katika sura hii
33
Ashdod, Blindness, Caphtorim, Carmel, Church, Confidence, Death, Edomites, Egypt, Evaporation, Eye, Gentiles, God, Government, Hell, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Judgments, Kir, Meteorology and Celestial Phenomena, Nation, Philistines, Prophecy, Prophets, Quotations and Allusions, Readings, Select, Security, Serpent, Sieve, Sin, Suicide, Vision, Wicked (People)