Ezekieli 7
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kwa nchi ya Israeli: “ ‘Mwisho! Mwisho umekuja juu ya pembe nne za nchi!
3 Sasa mwisho umekuja juu yenu, nami nitamwaga hasira yangu dhidi yenu. Nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za kuchukiza.
4 Sitawaonea huruma wala kuwarehemu. Hakika nitawalipiza kwa ajili ya matendo yenu na desturi za machukizo miongoni mwenu. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’
5 “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Maafa! Maafa ambayo hayajasikiwa! Tazama, yanakuja!
6 Mwisho umewadia! Mwisho umewadia! Umejiinua wenyewe dhidi yenu. Tazama, umewadia!
7 Maangamizi yamekuja juu yenu, ninyi mnaoishi katika nchi. Wakati umewadia! Siku imekaribia! Kuna hofu kuu ya ghafula juu ya milima, wala si furaha.
8 Ninakaribia kumwaga ghadhabu yangu juu yenu na kumaliza hasira yangu dhidi yenu. Nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za machukizo.
9 Sitawaonea huruma wala kuwarehemu. Nitawalipiza kwa ajili ya matendo yenu na desturi za machukizo miongoni mwenu. “ ‘Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu ambaye huwapiga.
10 “ ‘Tazama, siku imefika! Tazama, imewadia! Maangamizi yamezuka ghafula, fimbo imechanua, nayo majivuno yamechipua!
11 Jeuri imeinuka kuwa fimbo ya kuadhibu waovu. Hakuna hata mmoja wa hao watu atakayeachwa, hata mmoja wa kundi hilo: hakuna utajiri wao utabaki, wala chochote cha thamani.
12 Wakati umewadia, siku imefika. Mnunuzi na asifurahi wala muuzaji asihuzunike, kwa maana ghadhabu iko juu ya kundi lote.
13 Muuzaji hatajipatia tena ardhi aliyoiuza wakati wote wawili wangali hai. Kwa kuwa maono kuhusu kundi lote hayatatanguka. Kwa sababu ya dhambi zao, hakuna hata mmoja atakayeokoa maisha yake.
14 “ ‘Wajapopiga tarumbeta na kuweka kila kitu tayari, hakuna hata mmoja atakayeenda vitani, kwa maana ghadhabu yangu iko juu ya kundi lote.
15 Nje ni upanga, ndani ni tauni na njaa. Walio shambani watakufa kwa upanga, nao waliomo mjini njaa na tauni vitawala.
16 Wote watakaopona na kutoroka watakuwa milimani, wakiomboleza kama hua wa mabondeni, kila mmoja kwa sababu ya dhambi zake.
17 Kila mkono utalegea na kila goti litakuwa dhaifu kama maji.
18 Watavaa gunia na kufunikwa na hofu. Nyuso zao zitafunikwa na aibu, na vichwa vyao vitanyolewa.
19 “ ‘Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itakuwa najisi. Fedha yao na dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Hawatashibisha njaa yao au kujaza tumbo zao kwa hiyo fedha wala dhahabu, kwa sababu imewaponza wajikwae dhambini.
20 Walijivunia vito vyao vizuri na kuvitumia kutengeneza sanamu za machukizo na vinyago vya upotovu. Kwa hiyo nitavifanya vitu hivyo kuwa najisi kwao.
21 Nitavitia vyote mikononi mwa wageni kuwa nyara na kuwa vitu vilivyotekwa mikononi mwa watu waovu wa dunia, nao watavinajisi.
22 Nitaugeuza uso wangu mbali nao, nao waovu wa dunia watapanajisi mahali pangu pa thamani. Wanyang’anyi watapaingia na kupanajisi.
23 “ ‘Andaa minyororo, kwa sababu nchi imejaa umwagaji wa damu na mji umejaa udhalimu.
24 Nitaleta taifa ovu kuliko yote kumiliki nyumba zao. Nitakomesha kiburi cha wenye nguvu na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.
25 Hofu ya ghafula itakapokuja, watatafuta amani, lakini haitapatikana.
26 Maafa juu ya maafa yatakuja, tetesi ya mabaya juu ya tetesi ya mabaya. Watajitahidi kupata maono kutoka kwa nabii; mafundisho ya sheria toka kwa kuhani yatapotea, vivyo hivyo shauri kutoka kwa wazee.
27 Mfalme ataomboleza, mwana wa mfalme atavikwa kukata tamaa, nayo mikono ya watu wa nchi itatetemeka. Nitawaadhibu kulingana na matendo yao, na kwa kanuni zao wenyewe nitawahukumu. “ ‘Ndipo watajua kwamba Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
Marejeleo mtambuka
191
- 2Amo 8:2, Amo 8:10, Ezk 7:3, 1Pe 4:7, Ezk 11:13, Lam 4:18, Ezk 7:5–6, Lam 1:9
- 3Ezk 18:30, Ezk 5:13, Ezk 33:20, Ezk 7:8–9, Ezk 16:38, Ezk 7:27, Ezk 6:12–13, Rev 20:12–13
- 4Ezk 6:7, Ezk 5:11, Ezk 11:21, Ezk 6:14, Ezk 9:10, Hos 9:7, Hos 12:2, Ezk 16:43
- 5Ezk 5:9, Nam 1:9, 2Ki 21:12–13, Amo 3:2, Dan 9:12, Mat 24:21
- 6Zec 13:7, Jer 44:27, Ezk 7:3, Ezk 7:10, Ezk 21:25, Ezk 39:8, 2Pe 2:5
- 7Isa 22:5, Gen 19:15, Ezk 12:28, Ezk 7:12, Ezk 12:23–25, Gen 19:24, Jer 20:7, Isa 17:14
- 8Ezk 14:19, Ezk 9:8, Ezk 20:21, Isa 42:25, Ezk 20:8, Nam 1:6, Ezk 20:33, Psa 79:6
- 9Rev 20:13, Isa 9:13, Gal 6:7, Mic 6:9
- 10Isa 10:5, Jas 4:6, 1Th 5:3, Pro 16:18, Ezk 7:6, Pro 14:3, Psa 89:32, Isa 28:1
- 11Zep 1:18, Isa 59:6–8, Ezk 7:23, Jer 16:5–6, Mic 3:3, Isa 5:7, Psa 78:64, Jer 25:33
- 12Isa 5:13–14, 1Co 7:29–31, Ezk 6:11–12, Jas 5:8–9, Ezk 7:10, Isa 24:1–2, Ezk 7:5–7, Jer 32:7–8
- 13Lev 25:24–28, Ecc 8:8, Lev 25:31, Psa 52:7, Ezk 33:26–27, Ezk 13:22, Job 15:25
- 14Jer 4:5, Jer 51:27, Jer 6:1, Isa 24:1–7, Jer 6:11, Jer 12:12, Jer 7:20, Ezk 7:11–12
- 15Ezk 5:12, Jer 14:18, Lam 1:20, Jer 15:2–3, Deu 32:23–25, Ezk 6:12
- 16Isa 59:11, Isa 38:14, Ezr 9:15, Zec 12:10–14, Isa 37:31, Ezk 36:31, Ezk 6:8–9, Jer 50:4–5
- 17Ezk 21:7, Heb 12:12, Ezk 22:14, Jer 6:24, Isa 13:7–8
- 18Isa 15:2–3, Amo 8:10, Job 21:6, Ezk 27:31, Isa 3:24, Rev 6:15–17, Jer 3:25, Gen 15:12
- 19Zep 1:18, Pro 11:4, Ezk 14:7, Luk 12:19–20, Isa 2:20, Mat 16:26, Ezk 14:3–4, Ecc 5:10
- 20Ezk 24:21, Jer 7:30, Ezk 9:7, Ezk 8:7–10, Isa 64:11, Ezk 8:15–16, Hag 2:3, Psa 87:2–3
- 212Ki 24:13, Psa 74:2–8, 2Ch 36:18–19, Jer 52:13–23, 2Ki 25:13–16, Psa 79:1, 2Ki 25:9
- 22Jer 18:17, Psa 74:18–23, Psa 74:10–11, Psa 35:22, Ezk 39:23–24, Psa 10:11
- 23Jer 27:2, Ezk 9:9, Hos 4:2, 2Ki 21:16, Ezk 11:6, Jer 22:17, Ezk 8:17, 2Ki 24:4
- 24Ezk 28:7, Ezk 21:31, Ezk 33:28, Psa 106:41, Hab 1:6–10, Jer 6:12, Psa 83:12, Isa 5:14
- 25Lam 4:17–18, Isa 59:8–12, Isa 57:21, Jer 8:15–16, Ezk 13:16, Mic 1:12, Ezk 13:10
- 26Jer 4:20, Mic 3:6, Ezk 14:1, Psa 74:9, Jer 21:2, Lam 2:9, Ezk 20:1–3, Jer 18:18
- 27Ezk 18:30, Ezk 7:4–8, Rom 2:5–10, Isa 3:11, Jas 2:13, Ezk 17:15–21, Jol 3:17, Psa 9:16