Ayubu 9
1 Kisha Ayubu akajibu:
2 “Naam, najua hili ni kweli. Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
3 Ingawa mtu angetaka kushindana naye, hangeweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.
4 Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. Ni nani aliyempinga naye akawa salama?
5 Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.
6 Aitikisa dunia kutoka mahali pake na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.
7 Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; naye huizima mianga ya nyota.
8 Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
9 Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, na Orioni, Kilimia, na makundi ya nyota za kusini.
10 Hutenda maajabu yasiyopimika, miujiza isiyoweza kuhesabiwa.
11 Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; apitapo mbele yangu, simtambui.
12 Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’
13 Mungu hataizuia hasira yake; hata jeshi kubwa la Rahabu lenye nguvu linajikunyata miguuni pake.
14 “Ni vipi basi mimi nitaweza kubishana naye? Nawezaje kupata maneno ya kuhojiana naye?
15 Ingawa sikuwa na hatia, sikuweza kumjibu; ningeweza tu kumsihi Mhukumu wangu anihurumie.
16 Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.
17 Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.
18 Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.
19 Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?
20 Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.
21 “Ingawa mimi sina kosa, haileti tofauti katika nafsi yangu; nauchukia uhai wangu.
22 Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’
23 Wakati wa pigo liletapo kifo cha ghafula, yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa.
24 Nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, yeye huwafunga macho mahakimu wake. Kama si yeye, basi ni nani?
25 “Siku zangu zapita mbio kuliko mkimbiaji; zinapita upesi bila kuona furaha hata kidogo.
26 Zinapita upesi kama mashua ya mafunjo, mfano wa tai ayashukiaye mawindo kwa ghafula.
27 Nikisema, ‘Nitayasahau malalamiko yangu, nitabadili sura ya uso wangu na kutabasamu,’
28 bado ninahofia mateso yangu yote, kwa kuwa ninajua hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Kwa kuwa nimeonekana mwenye hatia, kwa nini basi nitaabishwe bure?
30 Hata kama ningejiosha kwa sabuni na kutakasa mikono yangu kwa magadi,
31 wewe ungenitupa kwenye shimo la utelezi kiasi kwamba hata nguo zangu zingenichukia sana.
32 “Yeye si mwanadamu kama mimi ili niweze kumjibu, ili tuweze kushindana naye mahakamani.
33 Laiti pangekuwa na mtu wa kutupatanisha, aweke mkono wake juu yetu sote wawili,
34 mtu wa kuondoa fimbo ya Mungu juu yangu, ili utisho wake usiendelee kunitia hofu.
35 Ndipo ningenena naye, bila kumwogopa, lakini kama ilivyo kwangu sasa, sitaweza.
Referências cruzadas
243
- 2Job 4:17, Psa 143:2, Rom 3:20, Job 25:4, Job 14:3–4, Job 32:2, Job 33:9, 1Ki 8:46
- 3Job 10:2, Job 40:2, Psa 19:12, 1Jn 1:8, Job 9:20, Psa 40:12, Job 31:35–37, Rom 9:20
- 4Job 36:5, Rom 11:33, Eph 3:20, Exo 14:17–18, Pro 29:1, Eph 3:10, Jud 1:24–25, Job 9:19
- 5Mat 27:51, Luk 21:11, Rev 11:13, Rev 16:18–20, Hab 3:10, Hab 3:6, Rev 6:14, Psa 68:8
- 6Psa 75:3, Heb 12:26, Hag 2:6, Isa 2:21, Job 26:11, Job 38:4–7, Isa 2:19, Hag 2:21
- 7Isa 13:10, Amo 8:9, Luk 21:25–26, Mat 24:29, Amo 4:13, Job 37:7, Job 38:19–20, Ezk 32:7–8
- 8Isa 44:24, Psa 104:2–3, Isa 40:22, Job 37:18, Zec 12:1, Mat 14:25–30, Psa 33:6, Jer 10:11
- 9Amo 5:8, Gen 1:16, Job 38:31–41, Psa 147:4, Act 28:13, Psa 104:13, Psa 104:3, Job 37:9
- 10Job 5:9, Psa 72:18, Rom 11:33, Eph 3:20, Psa 136:4, Dan 4:2–3, Ecc 3:11, Isa 40:26–28
- 11Job 23:8–9, Job 35:14, Psa 77:19, 1Ti 6:16
- 12Isa 45:9, Job 11:10, Job 23:13, Rom 11:34, Dan 4:35, Job 34:29, Jer 18:6, Job 33:13
- 13Psa 89:10, Job 26:12, Isa 51:9, Isa 30:7, Jas 4:6–7, Isa 31:2–3, Job 40:9–11
- 14Job 33:5, 1Ki 8:27, Job 23:4, Job 23:7, Job 4:19, Job 25:6, Job 9:3, Job 11:4–5
- 15Job 10:15, Job 8:5, Job 22:27, 1Pe 2:23, Job 5:8, Job 10:2, Job 23:7, Dan 9:18
- 16Exo 6:9, Psa 116:1–2, Jdg 6:13, Act 12:14–16, Psa 66:18–20, Psa 18:6, Psa 126:1, Job 29:24
- 17Job 16:14, Job 2:3, Job 34:6, Jhn 15:25, Ezk 13:13, Jer 23:19, Mat 12:20, Psa 83:15
- 18Job 7:19, Lam 3:15, Lam 3:18–19, Heb 12:11, Psa 88:7, Psa 39:13, Psa 88:15–18, Lam 3:3
- 19Job 9:32–33, Job 9:4, 1Co 1:25, Psa 62:11, Mat 6:13, Job 40:9–10, Job 36:17–19, Job 31:35
- 20Job 34:35, Php 3:12–15, Psa 143:2, Job 9:2, Job 4:17, Psa 130:3, Job 15:5–6, Job 32:1–2
- 21Psa 139:23–24, Job 1:1, Pro 28:26, Job 7:21, 1Co 4:4, 1Jn 3:20, Jer 17:9–10, Job 7:15–16
- 22Ecc 9:1–3, Ezk 21:3–4, Luk 13:2–4, Job 10:8
- 23Job 24:12, Heb 11:36–37, Job 8:20, Job 4:7, 2Sa 14:15, Psa 44:22, Job 2:7, Job 1:13–19
- 24Job 10:3, Psa 73:3–7, Jer 12:1–2, 2Sa 15:30, Job 21:7–15, Est 7:8, Job 32:2, Dan 5:18–21
- 25Jas 4:14, Job 7:6–7, Psa 90:9–10, Psa 39:5, Psa 39:11, Psa 89:47, Est 8:14
- 26Hab 1:8, Isa 18:2, Jer 4:13, Job 39:27–30, 2Sa 1:23, Lam 4:19, Pro 23:5
- 27Job 7:13, Jer 8:18, Psa 77:2–3, Job 7:11
- 28Psa 119:120, Job 3:25, Job 14:16, Psa 130:3, Job 10:14, Psa 88:15–16, Job 21:6, Job 7:21
- 29Job 10:7, Psa 37:33, Job 21:16–17, Jer 2:35, Psa 73:13, Job 10:2, Job 22:5–30, Job 21:27
- 30Jer 2:22, Psa 26:6, 1Jn 1:8, Isa 1:16–18, Pro 28:13, Jer 4:14, Job 31:7, Rom 10:3
- 31Isa 59:6, Php 3:8–9, Isa 64:6, Job 15:6, Job 9:20
- 32Rom 9:20, Ecc 6:10, Isa 45:9, Psa 143:2, Num 23:19, Job 23:3–7, Job 13:18–23, Job 35:5–7
- 331Sa 2:25, Job 9:19, 1Jn 2:1–2, Psa 106:23, 1Ki 3:16–28
- 34Psa 39:10, Job 13:11, Job 33:7, Job 31:23, Job 13:20–22, Job 37:1, Psa 90:11, Job 29:2–25
Temas neste capítulo
36
Afflictions and Adversities, Arcturus, Astronomy, Blasphemy, Constellations, Daysman, Depravity of Man, Doubting, Eagle, Earth, Earthquakes, God, Heart, Heaven, Humility, Impenitence, Intercession, Jesus, the Christ, Job, Life, Meteorology and Celestial Phenomena, Mountain, Murmuring, Orion, Perfection, Philosophy, Pleiades, Post, Power, Repentance, Satan, Scourging, Self-Condemnation, Sin, Snow, Stars