Ayubu 7
1 “Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
2 Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
3 ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
4 Nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
5 Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
6 “Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
7 Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
8 Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
9 Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena.
10 Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
11 “Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
12 Je, mimi ni bahari, au yule mnyama mkubwa wa baharini, hata uniweke chini ya ulinzi?
13 Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
14 ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
15 hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
16 Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
17 “Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
18 kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
19 Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
20 Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
21 Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”
Referências cruzadas
139
- 1Job 14:5–6, Psa 39:4, Job 5:7, Job 14:13–14, Deu 15:18, Jhn 11:9–10, Ecc 8:8, Mat 20:1–15
- 2Lev 19:13, Deu 24:15, Mal 3:5, Jas 5:4, Jer 6:4, Psa 143:6, Psa 119:131
- 3Psa 6:6, Ecc 1:14, Job 29:2, Psa 39:5, Job 16:7
- 4Deu 28:67, Job 7:13–14, Psa 77:4, Psa 6:6, Psa 130:6, Job 30:17, Job 17:12, Isa 54:11
- 5Isa 14:11, Job 17:14, Job 2:7–8, Job 19:26, Ezk 20:43, Isa 1:6, Job 24:20, Isa 66:24
- 6Job 9:25, Job 17:15, Job 17:11, Job 16:22, Psa 103:15–16, 1Pe 1:24, Pro 14:32, Isa 40:6–7
- 7Jas 4:14, Psa 78:39, Psa 89:47, Jer 15:15, Job 10:21–22, Psa 74:18, Psa 89:50, Job 10:9
- 8Job 20:9, Psa 37:36, Job 8:18, Psa 90:8–9, Psa 39:11, Job 13:27, Job 14:3
- 9Job 30:15, Job 10:21, 2Sa 14:14, 2Sa 12:23, Psa 39:13, Job 16:22, Job 14:10–14, Job 37:11
- 10Job 8:18, Job 20:9, Psa 103:16, Job 27:23, Job 27:21
- 111Sa 1:10, Psa 40:9, Job 10:1, Isa 38:15, Job 6:26, Isa 38:17, Job 21:25, Job 13:13
- 12Job 7:17, Lam 3:7, Ezk 32:2–3, Job 38:6–11, Job 41:1–34
- 13Psa 6:6, Psa 77:4, Job 9:27–28, Job 7:3–4
- 14Gen 41:8, Gen 40:5–7, Dan 2:1, Mat 27:19, Jdg 7:13–14
- 15Mat 27:5, 2Sa 17:23
- 161Ki 19:4, Job 10:1, Job 9:21, Job 14:6, Jon 4:8, Psa 62:9, Job 10:20, Job 6:9
- 17Heb 2:6, Psa 8:4, Psa 144:3, Job 34:14–15, Job 7:12
- 181Pe 1:7, Jer 9:7, Isa 38:12–13, Gen 22:1, Isa 26:14, Job 14:3, Exo 20:5, Dan 12:10
- 19Job 9:18, Psa 13:1–3, Job 14:6, Rev 6:10, Psa 6:3, Psa 94:3
- 20Lam 3:12, Psa 36:6, Job 3:24, Job 7:11–12, Job 6:4, Psa 80:4, Job 31:33, Job 33:9
- 21Dan 12:2, Job 10:14, 1Jn 1:9, Isa 64:9, Lam 5:20–22, Ecc 12:7, Jhn 1:29, Job 13:23–24