Ayubu 1
1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
2 Alikuwa na wana saba na binti watatu,
3 naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu maarufu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
4 Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika dada zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
5 Kipindi cha karamu kilipomalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
6 Siku moja wana wa Mungu walienda kujionesha mbele za Mwenyezi Mungu. Shetani naye akaja pamoja nao.
7 Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Mwenyezi Mungu, “Natoka kuzunguka duniani, nikitembea huku na huko.”
8 Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
9 Shetani akamjibu Mwenyezi Mungu, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
10 Je, wewe hukumzingira pande zote, yeye na watu wa nyumbani mwake, pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki, na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
11 Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
12 Mwenyezi Mungu akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Mwenyezi Mungu.
13 Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
14 akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
15 Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, mimi peke yangu ndiye niliyenusurika kukuletea habari!”
16 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, mimi peke yangu ndiye niliyenusurika kukuletea habari!”
17 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, mimi peke yangu ndiye niliyenusurika kukuletea habari.”
18 Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako wa kiume na wa kike walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
19 ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, mimi peke yangu ndiye niliyenusurika kukuletea habari!”
20 Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akasujudu na kuabudu,
21 akasema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Mwenyezi Mungu alinipa, naye Mwenyezi Mungu ameviondoa; jina la Mwenyezi Mungu litukuzwe.”
22 Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.
Referências cruzadas
158
- 1Jas 5:11, Ezk 14:14, Ezk 14:20, Job 28:28, Job 2:3, Gen 6:9, Job 1:8, Job 23:11–12
- 2Job 42:13, Psa 127:3–5, Job 13:13, Est 5:11, Psa 107:38, Psa 128:3
- 3Job 29:25, Job 42:12, Jdg 6:3, Pro 10:22, Num 23:7, 1Ki 4:30, Gen 12:16, Gen 12:5
- 4Heb 13:1, Psa 133:1
- 5Job 42:8, Gen 8:20, 1Sa 16:5, Job 8:4, Gen 35:2–3, Eph 6:18, 1Ki 21:13, 1Ki 21:10
- 6Job 2:1, Job 38:7, Zec 3:1, Rev 12:9–10, 1Ki 22:19, Gen 6:4, 1Ch 21:1, Mat 18:10
- 71Pe 5:8, Mat 12:43, Job 2:2, Rev 12:12–17, Rev 12:9, Rev 20:8, 2Ki 5:25, Zec 6:7
- 8Job 2:3, Job 1:1, Num 12:7–8, 2Ki 23:25, Pro 8:13, Job 8:20, Isa 1:16, Psa 84:11
- 91Ti 4:8, Mat 16:26, 1Ti 6:6, Job 1:21, Job 21:14–15, Job 2:10, Mal 1:10
- 10Psa 34:7, Zec 2:5, 1Pe 1:5, Deu 28:2–6, Pro 10:22, Zec 2:8, Job 31:25, Psa 107:38
- 11Job 2:5, Job 19:21, Rev 16:11, Mal 3:13–14, Rev 16:21, Rev 16:9, Job 2:9, Job 4:5
- 12Luk 22:31–32, Jhn 3:35–36, 2Co 12:7, 1Co 10:13, Jhn 19:11, Isa 27:8, Job 2:4–7, Luk 8:32–33
- 13Luk 21:34, Pro 27:1, Luk 12:19–20, Job 1:4, Luk 17:27–29, Ecc 9:12
- 141Sa 4:17, Jer 51:31, 2Sa 15:13
- 15Gen 10:7, Job 6:19, Job 1:16–17, Job 1:19, Psa 72:10, Gen 25:3, Jol 3:8, Gen 10:28
- 162Ki 1:12, Gen 19:24, 1Ki 18:38, Lev 10:2, Amo 7:4, Num 11:1–3, Lev 9:24, 2Ki 1:10
- 17Gen 11:28, Hab 1:6, Isa 23:13, Gen 11:31, 2Sa 1:3, Job 1:15
- 18Job 1:4, Job 1:13, Job 23:2, Job 19:9–10, Psa 34:19, Job 6:2–3, Jer 51:31, Amo 4:6–11
- 19Jer 4:11–12, Eph 2:2, Luk 13:1–5, 1Ki 20:30, Gen 42:36, Act 28:4, Gen 37:32–33, 2Sa 18:33
- 201Pe 5:6, 2Sa 12:16–20, Gen 37:29, Gen 37:34, Ezr 9:3, Deu 9:18, Mat 26:39, 2Ch 7:3
- 21Ecc 5:15, 1Ti 6:7, 1Th 5:18, Jas 1:17, Job 2:10, Psa 49:17, Ecc 12:7, Eph 5:20
- 22Jas 1:12, Job 2:10, 1Pe 1:7, Rom 9:20, Jas 1:4, Job 40:4–8, Job 34:18–19, Job 34:10
Temas neste capítulo
40
Accusation, False, Afflictions and Adversities, Amusements and Worldly Pleasures, Armies, Bereavement, Blessing, Camel, Children, Death, Dissipation, Dress, Faith, Faithfulness, Falsehood, Family, Fear, God, Hedge, Intercession, Job, Mantle, Meteorology and Celestial Phenomena, Motive, Mourning, Obedience, Parents, Patience, Perfection, Persecution, Plow, Prayer, Rending, Resignation, Rich, the, Sabeans, Satan, Sin, Temptation, Uz, Worship