Ayubu 5
1 “Itana, ukitaka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwa udongo, wala ubaya hauchipui kutoka ardhini.
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zinavyoruka kuelekea juu.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeweka shauri langu mbele zake.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale wanaoomboleza huinuliwa wakawa salama.
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humkanya; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Utayacheka maangamizi na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama pori watakuwa na amani nawe.
24 Utajua kwamba hema lako li salama; utahesabu mali yako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Utajua kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yanapokusanywa kwa wakati wake.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Referências cruzadas
200
- 1Job 15:15, Job 4:18, Job 15:8–10, Isa 41:21–23, Isa 41:1, Heb 12:1, Eph 1:1, Deu 33:2–3
- 2Ecc 7:9, Psa 92:6, Pro 12:16, Psa 75:4, Rom 2:8, Psa 107:17, Job 18:4, 1Sa 18:8–9
- 3Psa 73:18–20, Psa 92:7, Psa 69:25, Job 24:18, Psa 73:3–9, Act 1:20, Jer 12:1–3, Job 27:8
- 4Psa 127:5, Psa 119:155, Job 18:16–19, Job 10:7, Psa 7:2, Job 27:14, Exo 20:5, Job 8:4
- 5Lam 2:16, Hos 8:7, Jer 51:44, Jer 51:34, Job 18:8–10, Jdg 6:3–6, 2Ch 33:11, Jdg 6:11
- 6Isa 45:7, 1Sa 6:9, Psa 90:7, Job 34:29, Lam 3:38, Amo 3:6, Hos 10:4, Deu 32:27
- 7Job 14:1, Gen 3:17–19, Ecc 5:15–17, 1Co 10:13, Ecc 2:22, Ecc 1:8, Psa 90:8–9
- 8Psa 50:15, Psa 37:5, Job 22:21, 2Ch 33:12–13, 1Pe 4:19, 2Ti 1:12, Job 22:27, Job 8:5
- 9Psa 40:5, Job 9:10, Psa 86:10, Psa 72:18, Job 11:7–9, Job 37:5, Rom 11:33, Isa 40:28
- 10Jer 5:24, Act 14:17, Jer 14:22, Psa 65:9–11, Psa 147:8, Job 28:26, Jer 10:13, Job 38:26–28
- 11Psa 113:7, Luk 1:52–53, Luk 6:21, 1Sa 2:7–8, Psa 107:41, Deu 33:27, Jas 4:6–10, Psa 91:14
- 12Psa 33:10–11, Psa 21:11, Isa 8:10, Pro 21:30, Psa 37:17, Isa 37:36, Act 12:11, Neh 4:15
- 13Psa 9:15–16, 1Co 3:19, Luk 1:51, Psa 7:15–16, 1Co 1:19–20, Est 9:25, Psa 18:26, Psa 35:7–8
- 14Job 12:25, Deu 28:29, Isa 59:10, Pro 4:19, Amo 8:9
- 15Psa 35:10, Psa 140:12, Psa 109:31, Job 4:10, Psa 10:17, Psa 72:4, Psa 107:41, Psa 10:14
- 16Psa 107:42, 1Sa 2:8–9, Psa 63:11, Isa 14:32, Exo 11:7, Rom 3:19, Zec 9:12, Psa 9:18
- 17Jas 1:12, Psa 94:12, Pro 3:11–12, Rev 3:19, Jas 5:11, Heb 12:5–11, Jer 31:18
- 18Hos 6:1, Deu 32:39, Psa 147:3, Isa 30:26, 1Sa 2:6
- 19Psa 34:19, 1Co 10:13, Psa 91:3–10, Pro 24:16, 2Pe 2:9, 2Co 1:8
- 20Psa 33:19, Hos 13:14, Psa 37:19, Gen 45:7, Pro 10:3, 1Ki 17:6, Hab 3:17, Psa 27:3
- 21Psa 31:20, Psa 91:5–7, Pro 12:18, Psa 55:21, Jer 18:18, Psa 57:4, Isa 54:17, Jas 3:5–8
- 22Ezk 34:25, Isa 35:9, Psa 91:13, Hos 2:18, Isa 65:25
- 23Lev 26:6, Dan 6:22, Psa 91:12–13, Isa 11:6–9, Hos 2:18, Ezk 14:15–16, Rom 8:38–39
- 24Psa 121:7–8, Psa 91:10, Job 8:6, Isa 4:5–6, Deu 28:6, Job 18:6, Job 18:21, Psa 107:4
- 25Psa 112:2, Psa 72:16, Deu 28:4, Job 42:13–16, Gen 15:5, Lev 26:9, Psa 128:3–6, Psa 127:3–5
- 26Pro 9:11, Job 42:16–17, Psa 91:16, Gen 15:15, Pro 10:27, Gen 25:8
- 27Psa 111:2, Pro 9:12, Job 32:11–12, Pro 2:3–5, Deu 10:13, Job 15:17, Job 12:2, Job 15:9–10
Temas neste capítulo
31
Afflictions and Adversities, Anger, Blessing, Chastisement, Children, Eliphaz, Envy, Faith, Famine, Fear, God, Happiness, Holiness, Humility, Job, Longevity, Old Age, Peace, Philosophy, Poor, Power, Presumption, Quotations and Allusions, Resignation, Righteous, Scourging, Seekers, Sin, Slander, Wicked (People), Wisdom