Ayubu 35
1 Ndipo Elihu akasema:
2 “Je, unadhani hili ni haki? Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’
3 Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata, na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’
4 “Ningependa nikujibu wewe na rafiki zako walio nawe.
5 Tazama juu mbinguni ukaone; yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.
6 Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu? Kama dhambi zako zikiwa nyingi, hilo linamfanyia nini Mungu?
7 Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini, au yeye anapokea nini mkononi kwako?
8 Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe, nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.
9 “Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.
10 Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu, yeye anifanyaye niimbe usiku,
11 yeye atufundishaye sisi zaidi ya wanyama wa nchi, na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’
12 Yeye hajibu wakati watu waliapo kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
13 Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili; Mwenyezi hayazingatii.
14 Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza wewe usemapo humwoni, tena kwamba kesi yako iko mbele zake na wewe lazima umngojee,
15 pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu wala haangalii uovu hata kidogo?
16 Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana; anaongea maneno mengi bila maarifa.”
Referências cruzadas
99
- 2Mat 12:36–37, Job 9:17, Job 27:2–6, Job 40:8, Job 16:17, Job 10:7, Job 34:5, Job 19:6–7
- 3Job 34:9, Mal 3:14, Job 21:15, Job 9:30–31, Job 31:2, Job 9:21–22, Job 10:15, Psa 73:13
- 4Job 34:8, Pro 13:20
- 5Job 22:12, Isa 55:9, Nam 1:3, Isa 40:22–23, Job 25:5–6, Job 36:26–37:5, Gen 15:5, Job 37:16
- 6Jer 7:19, Pro 8:36, Pro 9:12
- 7Job 22:2–3, Psa 16:2, Luk 17:10, Rom 11:35, Pro 9:12, 1Ch 29:14
- 8Heb 11:7, Ezk 22:30, Gen 18:24–33, Gen 19:29, Ecc 9:18, Jos 7:1–5, Psa 106:23, Jos 22:20
- 9Exo 2:23, Job 34:28, Exo 3:7, Psa 12:5, Psa 56:1–2, Psa 10:15, Neh 5:1–5, Job 40:9
- 10Psa 42:8, Act 16:25, Psa 149:5, Psa 77:6, Isa 51:13, 1Pe 4:19, Job 36:13, Ecc 12:1
- 11Psa 94:12, Job 32:8, Job 36:22, Gen 1:26, Gen 2:7
- 12Pro 1:28, Jhn 9:31, Psa 123:3–4, Psa 73:6–8, Psa 18:41, Isa 14:14–17
- 13Pro 15:29, Jer 11:11, Jas 4:3, Isa 1:15, Pro 15:8, Ecc 5:1–3, Hos 8:2–3, Amo 5:22
- 14Job 9:11, Job 23:3, Job 19:7, Psa 62:8, Job 23:8–10, Psa 77:5–10, Rom 8:33–34, Psa 97:2
- 15Psa 89:32, Num 20:12, Job 9:14, Job 13:15, Luk 1:20, Job 30:15–31, Psa 88:11–16, Heb 12:11–12
- 16Job 38:2, Job 34:35–37, Job 33:8–12, Job 3:1, Job 33:2