Ayubu 40
1 Mwenyezi Mungu akamwambia Ayubu:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Mwenyezi Mungu:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Ndipo Mwenyezi Mungu akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe unaweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ng’ombe.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama pori wote hucheza karibu naye.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Mto unapofurika, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Referências cruzadas
112
- 1Job 38:1, Job 40:6
- 21Co 2:16, Isa 40:14, Rom 11:34–36, Job 33:13, Isa 45:9–11, Isa 50:8, Rom 9:19–23, Mat 20:11
- 4Pro 30:32, Job 29:9, Job 21:5, Job 42:6, Gen 18:27, Ezr 9:6, Jdg 18:19, Mic 7:16
- 5Psa 62:11, Job 33:14, Job 9:15, Job 9:3, Job 34:31–32, Rom 3:19, Jer 31:18–19, 2Ki 6:10
- 6Job 38:1, Heb 12:18–20, 2Pe 3:10–12, Psa 50:3–4
- 7Job 38:3, Job 42:4, Job 23:3–4, Job 13:22
- 8Rom 3:4, Job 32:2, Isa 28:18, Isa 14:27, Psa 51:4, Job 34:5–6, Job 10:3, Job 35:2–3
- 9Psa 89:13, Job 37:4–5, Psa 29:3, Job 9:4, 1Co 10:22, Exo 15:6, Job 23:6, Job 33:12–13
- 10Psa 93:1, Psa 149:4, Isa 59:17, 2Pe 1:16–17, Psa 104:1–2, Psa 21:5, Psa 90:16–17, Exo 28:2
- 11Dan 4:37, Isa 2:11–12, Isa 2:17, Nam 1:6, Act 12:22–23, Dan 5:20–23, Rom 2:8–9, Isa 10:12–19
- 12Isa 63:3, Mal 4:3, Zec 10:5, Psa 60:12, 1Sa 2:7, Isa 10:6, Pro 15:25, Job 36:20
- 13Isa 2:10, Est 7:8, Job 14:13, Job 36:13, Psa 49:14, Jhn 11:44
- 14Rom 5:6, Psa 44:6, Isa 40:29, Psa 44:3, Eph 2:4–9
- 15Gen 1:24–26, Psa 104:14, Job 40:20, Job 39:8
- 17Job 41:23
- 18Job 7:12, Isa 48:4
- 19Job 41:33, Isa 27:1, Psa 104:24, Psa 7:12, Job 26:13
- 20Psa 104:26, Psa 104:14, Psa 147:8–9, Job 40:15
- 21Isa 19:6–7, Isa 35:7
- 22Isa 15:7, Ezk 17:5, Lev 23:40
- 23Gen 13:10, Psa 55:8, Jos 3:15, Isa 37:25, Isa 28:16
- 24Job 41:1–2