1 Yohana 1
1 Tunawajulisha lile lililokuwako tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
2 Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu.
3 Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Isa Al-Masihi.
4 Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
5 Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
6 Tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
7 Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Isa, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
8 Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
9 Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutokana na udhalimu wote.
10 Tukisema hatujatenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.
Referências cruzadas
80
- 1Act 4:20, Jhn 20:27, 1Jn 4:14, Jhn 1:1–18, Luk 24:39, Jhn 5:26, Jhn 8:58, 2Pe 1:16–18
- 2Jhn 1:4, 1Jn 5:20, 1Ti 3:16, Jhn 17:3, 1Jn 3:8, Jhn 14:6, Tit 1:2, 1Jn 3:5
- 31Co 1:9, Jhn 17:3, Jhn 17:21, Act 4:20, Php 2:1, 2Co 13:14, 1Jn 1:7, Heb 3:14
- 4Jhn 15:11, Jhn 16:24, 2Jn 1:12, 2Co 1:24, Hab 3:17–18, Jhn 3:29, Eph 3:19, Php 1:25–26
- 5Jhn 8:12, Jas 1:17, Isa 60:19, Psa 27:1, Jhn 1:9, Jhn 1:4, Rev 22:5, Jhn 12:35–36
- 61Jn 4:20, 1Jn 2:4, Jhn 3:19–21, Jhn 8:12, Pro 4:18–19, Pro 2:13, 1Jn 1:10, Jhn 12:35
- 7Eph 5:8, Rom 13:12, Rev 1:5, Eph 1:7, Rev 7:14, 1Jn 2:9–10, Heb 9:14, 1Co 6:11
- 8Rom 3:23, Ecc 7:20, Jas 3:2, Isa 53:6, 1Jn 2:4, 1Jn 1:10, Pro 20:9, Job 15:14
- 9Psa 32:5, Pro 28:13, Jer 33:8, Psa 51:2–5, 1Jn 1:7, Ezk 36:25, Heb 10:23, 1Ti 1:15
- 101Jn 1:8, 1Jn 5:10, 1Jn 2:4, Psa 130:3, 2Jn 1:2, 1Jn 2:14, Job 24:25, Col 3:16
Temas neste capítulo
35
Ablution, Atonement, Blessing, Blindness, Blood, Cleanliness, Communion, Confession, Darkness, Depravity of Man, Fellowship, God, Gospel, Holiness, Hypocrisy, Jesus, the Christ, Joy, Judgment, Life, Light, Penitent, Repentance, Reprobacy, Righteous, Salvation, Sanctification, Satan, Sin, Sinlessness, Testimony, Truth, Unbelief, Walking, Wicked (People), Word of God