Marko 13
1 Isa alipokuwa akitoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”
2 Ndipo Isa akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”
3 Isa alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani,
4 “Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”
5 Isa akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye.
6 Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi.
7 Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.
8 Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa uchungu.
9 “Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao.
10 Nayo Injili lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote.
11 Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu wa Mungu.
12 “Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.
13 Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
14 “Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walio Yudea wakimbilie milimani.
15 Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote.
16 Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
17 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
18 Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi.
19 Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwa tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, hadi leo, na wala haitakuwa tena kamwe.
20 “Kama Mwenyezi Mungu hangefupisha siku hizo, kamwe hakuna mtu yeyote angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo.
21 Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Al-Masihi huyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki.
22 Kwa maana watatokea masihi wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule.
23 Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.
24 “Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki, “ ‘jua litatiwa giza nao mwezi hautatoa nuru yake;
25 nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’
26 “Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.
27 Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.
28 “Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
29 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
30 Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
32 “Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.
33 Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia.
34 Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.
35 “Basi kesheni, kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko,
36 akija ghafula asije akawakuta mmelala.
37 Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”
Cross-references
248
- 1Mat 24:1–51, Ezk 11:22–23, Ezk 7:20–22, Ezk 8:6, Ezk 10:19, Ezk 10:4, Mal 3:1–2, Luk 21:5–36
- 2Luk 21:6, Mat 24:2, Mic 3:12, 1Ki 9:7–8, Jer 26:18, Luk 19:41–44, 2Ch 7:20–21, Act 6:14
- 3Mat 21:1, Mrk 4:34, Mrk 10:35, Mat 17:1, Mat 13:10, Mrk 5:37, Mrk 14:33, Mrk 1:16–19
- 4Act 1:6–7, Mat 24:3, Jhn 21:21–22, Dan 12:6, Luk 21:7, Dan 12:8
- 5Col 2:8, Eph 5:6, Jer 29:8, Mat 24:4–5, 1Co 15:33, Luk 21:8, 2Th 2:3, Rev 20:7–8
- 6Mrk 13:22, Jhn 5:43, 1Jn 4:1, Mat 24:11, Mat 24:23–24, Mat 24:5, Jer 14:14, Act 5:36–39
- 7Luk 21:9–11, Jhn 14:27, Mat 24:6–7, Psa 27:3, Psa 112:7, Act 17:3, Isa 8:12, Pro 3:25
- 8Mat 24:8, Psa 48:6, 1Th 5:3, Hag 2:22, Isa 37:3, Mic 4:9–10, Zec 14:13, Jer 22:23
- 9Mat 10:17–18, Jhn 16:2, Php 1:29, 1Co 4:9–13, Mrk 13:5, Mat 24:9–10, Act 12:1–3, Mat 23:34–37
- 10Mat 24:14, Col 1:23, Rom 10:18, Mrk 16:15, Col 1:6, Rev 14:6, Mat 28:18–19, Rom 15:19
- 11Luk 21:14–15, Luk 12:11–12, Mat 10:19–21, Act 6:10, 1Co 2:13, 1Pe 1:12, 2Sa 23:2, Isa 50:4
- 12Mat 10:21, Luk 12:52–53, Mic 7:4–6, Mat 24:10, Ezk 38:21, Luk 21:16
- 13Mat 10:22, Jhn 15:18–19, Mat 24:13, Luk 6:22, Gal 6:9, Rom 2:7, Mat 5:11–12, Jhn 15:21
- 14Dan 12:11, Dan 9:27, Dan 11:31, Mat 24:15–28, Luk 21:20–24, Dan 8:13, 1Co 14:20, Rev 13:18
- 15Heb 11:7, Luk 17:31–33, Php 3:7–8, Mat 24:16–18, Pro 6:4–5, Act 27:18–19, Gen 19:15–17, Job 2:4
- 17Luk 23:29, Lam 4:10, Deu 28:56–57, Luk 21:23, Hos 13:16, Lam 2:19–20, Mat 24:19–21, Hos 9:14
- 19Dan 12:1, Mat 24:21, Jol 2:2, Dan 9:26, Luk 21:22–24, Lam 1:12, Mrk 10:6, Dan 9:12
- 20Mat 24:22, Zec 13:8–9, Isa 65:8–9, Rom 11:28–32, Rom 11:23–24, Isa 1:9, Rom 11:5–7, Isa 6:13
- 21Mat 24:23–25, Luk 21:8, Mat 24:5, Deu 13:1–3, Luk 17:23–24, Jhn 5:43
- 22Mat 24:24, 2Th 2:8–14, Mrk 13:6, Mat 7:15, 1Jn 2:26, Jhn 10:27–28, 1Jn 2:19, Rev 13:13–14
- 232Pe 3:17, Luk 21:8, Mrk 13:5, Jhn 14:29, Isa 44:7–8, Mrk 13:9, Luk 21:34, Mat 7:15
- 24Isa 13:10, Act 2:19–20, Mat 24:29–31, Rev 6:12–14, Jol 2:30–31, Jol 3:15, Amo 5:20, 2Pe 3:10
- 25Isa 34:4, Rev 6:13
- 26Rev 1:7, Mat 16:27, Mat 24:30, Mrk 14:62, Mat 25:31, Mrk 8:38, Dan 7:9–14, Act 1:11
- 27Zec 2:6, Mat 24:31, Deu 30:4, 2Th 2:1, Rev 7:1–3, Luk 16:22, Mrk 13:20, Mat 13:41
- 28Luk 21:29–31, Mat 24:32–33
- 29Jas 5:9, 1Pe 4:17–18, Heb 10:25–37, Ezk 12:25–28, Ezk 7:10–12
- 30Mat 24:34, Luk 21:32, Mat 16:28, Mrk 9:1, Mat 23:36
- 31Isa 40:8, Isa 51:6, Mat 24:35, Luk 21:33, Mat 5:18, Psa 102:25–27, Heb 1:10–12, Psa 19:7
- 32Mat 24:36–42, Act 1:7, Mat 25:13, Rev 3:3, 1Th 5:1–2, Mrk 13:26–27, Mat 25:6, 2Pe 3:10
- 33Luk 12:40, Rom 13:11–12, Eph 6:18, Rev 16:15, Luk 21:34–36, 1Pe 4:7, Mat 25:13, 1Pe 5:8
- 34Jhn 10:3, Mat 25:14–30, Luk 12:36–40, Mat 24:45–47, Ezk 3:17–21, Ezk 33:2–9, 1Co 15:58, Act 20:29–31
- 35Mrk 13:33, Mat 24:42, Mat 24:44, Mrk 14:30, Mrk 6:48
- 361Th 5:6–7, Rom 13:11–14, Luk 21:34, Mrk 14:40, Mat 24:48–51, Mat 25:5, Mrk 14:37, Isa 56:10
- 37Luk 12:41–46, Mrk 13:33, Mrk 13:35
Parallel passages
1
- Signs of the End of the AgeMat 24:1–8, Mrk 13:1–8, Luk 21:5–11
Topics in this chapter
44
Andrew, Angel (A Spirit), Antichrist, Astronomy, Beating, Blessing, Children, Cock Crowing, Commandments, Darkness, Decision, Earth, Earthquakes, Eclipse, God, Gospel, Holy Spirit, Israel, Prophecies Concerning, James, Jerusalem, Jesus, the Christ, Judgment, Martyrdom, Minister, Christian, Missions, Moon, Olives, Mount of, Persecution, Perseverance, Peter, Power, Predestination, Reward, Righteous, Sign, Stars, Stones, Summer, Sun, Temple, Temptation, War, Watchfulness, Word of God