Marko 16
1 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalene, Mariamu mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Isa.
2 Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walienda kaburini.
3 Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka ingilio la kaburi?”
4 Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
5 Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
6 Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Isa, Mnasiri, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Mtamwona huko kama alivyowaambia.’ ”
8 Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa. Isa amtokea Mariamu Magdalene (Mathayo 28:9-10; Yohana 20:11-18) [
9 Isa alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, aliyekuwa amemtoa pepo wachafu saba.
10 Mariamu akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Isa, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
11 Lakini waliposikia kwamba Isa yu hai na kwamba Mariamu alikuwa amemwona, hawakusadiki.
12 Baadaye Isa akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
13 Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
14 Baadaye Isa akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
15 Akawaambia, “Nendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
19 Baada ya Bwana Isa kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
20 Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana Isa akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]
Cross-references
131
- 1Luk 23:56–24:12, Mat 28:1–10, Jhn 20:1–10, Mrk 15:40, Jhn 19:25, Mrk 14:3, 2Ch 16:14, Mrk 14:8
- 2Jhn 20:1, Luk 24:1, Mat 28:1
- 3Mrk 15:46–47, Mat 27:60–66
- 4Mat 28:2–4, Luk 24:2, Jhn 20:1
- 5Jhn 20:11–12, Mat 28:3, Jhn 20:8, Luk 24:3–5, Luk 1:29–30, Mrk 6:49–50, Mrk 9:15, Luk 1:12
- 6Rev 1:17–18, Luk 24:46, 1Co 15:3–7, Mat 28:4–7, Jhn 2:19–22, Act 4:10, Act 2:22–23, Pro 8:17
- 7Mrk 14:28, Mat 26:32, Mat 28:10, Mat 28:7, Mat 28:16–17, Jhn 21:1, 1Co 15:5, Mrk 14:50
- 8Luk 24:22–24, Mat 28:8, Luk 24:37, Luk 24:9–11, Mrk 16:5–6, 2Ki 4:29, Luk 10:4
- 9Luk 8:2, Jhn 20:14–19, Jhn 20:12, Mrk 15:47, Luk 24:10, Mat 27:56, Mrk 15:40
- 10Jhn 20:18, Jhn 16:6, Mrk 14:72, Mat 9:15, Luk 24:17, Mat 24:30, Jhn 16:20–22
- 11Luk 24:11, Mrk 16:13–14, Luk 24:23–35, Mrk 9:19, Exo 6:9, Job 9:16
- 12Luk 24:13–32, Mrk 16:14, Jhn 21:14, Jhn 21:1
- 13Jhn 20:25, Luk 24:33–35, Jhn 20:8, Luk 16:31
- 141Co 15:5, Luk 24:36–43, Heb 3:7–8, Mrk 8:17–18, Rev 3:19, Jhn 20:27, Psa 95:8–11, Mrk 16:11–13
- 15Mat 28:19, Mrk 13:10, Act 1:8, Luk 24:47–48, Psa 96:3, Jhn 15:16, 1Jn 4:14, Jhn 20:21
- 16Jhn 11:25–26, Jhn 3:36, Rom 10:9–14, Jhn 3:18–19, Jhn 3:15–16, Act 2:38, Jhn 5:24, Jhn 8:24
- 17Act 5:16, 1Co 12:28, Luk 10:17, Act 8:7, Jhn 14:12, 1Co 12:10, Act 10:46, Act 19:6
- 18Luk 10:19, Jas 5:14–15, Act 28:3–6, Act 19:12, Act 4:30, Act 28:8–9, Mrk 5:23, Act 3:16
- 191Pe 3:22, Heb 1:3, Heb 12:2, Rom 8:34, Psa 110:1, Act 2:33, Heb 8:1, Col 3:1
- 201Co 2:4–5, Act 14:3, Rom 15:19, Heb 2:4, Act 8:4–6, Act 5:12, Act 2:1–28, 1Co 3:6–9
Parallel passages
1
- The Empty TombMat 28:1–8, Mrk 16:1–8, Luk 24:1–12, Jhn 20:1–10
Topics in this chapter
40
Angel (A Spirit), Anointing, Apostles, Ascension, Baptism, Burial, Charism, Demons, Disease, Doubting, Embalming, Faith, Galilee, God, Gospel, Hand, Heart, Heaven, James, Jesus, the Christ, Language, Love, Mary, Miracles, Missions, Persecution, Peter, Power, Rising, Sabbath, Salome, Salvation, Serpent, Spices, Stones, Translation, Unbelief, Wicked (People), Women, Zeal, Religious