Marko 12
1 Isa akaanza kusema nao kwa mifano, akawaambia: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, na ndani yake akachimba shimo la shinikizo la kukamulia zabibu, na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha shamba hilo la mizabibu kwa wakulima fulani, kisha akasafiri hadi nchi nyingine.
2 Wakati wa mavuno ulipofika, mwenye shamba akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili kuchukua sehemu yake ya mavuno ya shamba la mizabibu kutoka kwa hao wapangaji.
3 Lakini wale wakulima walimkamata yule mtumishi, wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
4 Kisha yule mwenye shamba akamtuma mtumishi mwingine kwao; nao wale wakulima wakampiga kichwani na kumfanyia mambo ya aibu.
5 Kisha akamtuma mtumishi mwingine, naye huyo wakamuua. Akawatuma wengine wengi; baadhi yao wakawapiga, na wengine wakawaua.
6 “Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
7 “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’
8 Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
9 “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.
10 Je, hamjasoma andiko hili: “ ‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni;
11 Mwenyezi Mungu ndiye alitenda jambo hili, nalo ni la kushangaza machoni petu’?”
12 Walipotambua kuwa amesema mfano huo kwa ajili yao, wakataka kumkamata, lakini wakaogopa umati ule wa watu. Wakamwacha, wakaenda zao.
13 Baadaye wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherode ili wamtege Isa katika maneno yake.
14 Wakamjia, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu. Wewe huyumbishwi na wanadamu, kwa kuwa huna upendeleo. Lakini wewe huifundisha njia ya Mungu katika kweli. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?
15 Je, tulipe kodi au tusilipe?” Lakini Isa alijua unafiki wao. Akawauliza, “Mbona mnajaribu kunitega? Nileteeni hiyo dinari niione.”
16 Wakamletea hiyo sarafu. Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?” Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.”
17 Ndipo Isa akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.” Nao wakamstaajabia sana.
18 Kisha Masadukayo, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Isa,
19 wakasema, “Mwalimu, Musa alituandikia kuwa kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
20 Basi kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa bila kuacha mtoto yeyote.
21 Wa pili akamwoa yule mjane, lakini naye akafa bila kuacha mtoto yeyote. Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa tatu.
22 Hakuna hata mmoja wa hao ndugu saba aliyeacha mtoto. Hatimaye yule mwanamke naye akafa.
23 Basi, wakati wa ufufuo yeye atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
24 Isa akawajibu, “Je, hampotei kwa sababu hamfahamu Maandiko wala uweza wa Mungu?
25 Wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
26 Basi kuhusu wafu kufufuliwa, je hamjasoma katika Kitabu cha Musa jinsi Mungu alivyosema na Musa kutoka kile kichaka akisema, ‘Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo’?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Kwa hiyo mmekosea kabisa.”
28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Isa amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
29 Isa akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
30 Mpende Mwenyezi Mungu, Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
32 Yule mwalimu wa Torati akamwambia Isa, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
33 Kumpenda Mungu kwa moyo wako wote, na kwa ufahamu wako wote, na kwa nguvu zako zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
34 Isa alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe huko mbali na ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
35 Isa alipokuwa akifundisha Hekaluni, akauliza, “Imekuwaje walimu wa Torati wanasema kwamba Al-Masihi ni Mwana wa Daudi?
36 Kwa maana Daudi mwenyewe, akinena kwa kuongozwa na Roho wa Mungu, alisema: “ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.” ’
37 Kwa hiyo Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana.’ Awezaje basi yeye kuwa mwanawe?” Umati ule wote wa watu wakamsikiliza kwa furaha.
38 Alipokuwa akifundisha, Isa alisema, “Jihadharini na walimu wa Torati. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.
39 Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu.
40 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
41 Kisha Isa akaketi mkabala na sehemu ambapo sadaka zilikuwa zinawekwa na kuangalia umati wa watu wakiweka fedha zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu. Matajiri wengi wakaweka kiasi kikubwa cha fedha.
42 Lakini mjane mmoja maskini akaja na kuweka sarafu mbili ndogo za shaba zenye thamani ya senti mbili.
43 Isa akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka katika sanduku la hazina zaidi ya watu wengine wote.
44 Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali yao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake, akaweka kila kitu alichokuwa nacho, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
Cross-references
262
- 1Isa 5:1–4, Mrk 13:34, Sng 8:11–12, Mrk 4:2, Rom 11:17–24, Mat 25:14, Psa 80:8–16, Mrk 4:33–34
- 2Jhn 15:1–8, Luk 12:48, Jer 25:4–5, Jdg 6:8–10, Psa 1:3, 2Ch 36:15, Zec 1:3–6, Mic 7:1
- 31Th 2:15, Act 7:52, Heb 11:36–37, Jer 26:20–24, Jer 29:26, Neh 9:26, 2Ch 36:16, 1Ki 18:13
- 5Mat 22:6, Neh 9:30, Mat 5:12, Luk 6:22–23, Mrk 9:13, Mat 21:35–36, Jer 7:25–28, Luk 6:36
- 6Mat 3:17, Heb 1:1–2, Jhn 1:34, Gen 22:2, Mat 26:63, Mat 17:5, Mat 1:23, Heb 1:6
- 7Mrk 12:12, Act 13:27–28, Mat 2:3–13, Act 5:28, Isa 49:7, Mat 2:16, Gen 37:20, Isa 53:7–8
- 8Mat 21:39, Mat 21:33, Luk 20:15, Heb 13:11–13
- 9Rom 10:20–11:12, Mat 21:43, Luk 19:27, Rom 9:30–33, Mat 8:11–13, Mal 1:11, Mat 23:34–38, Act 13:46–48
- 10Psa 118:22–23, Isa 28:16, 1Pe 2:7–8, Luk 20:17–18, Mat 21:42, Act 4:11–12, Eph 2:20–22, Rom 9:33
- 11Psa 118:23, Act 3:12–16, Hab 1:5, Act 2:32–36, Act 2:12, 1Ti 3:16, Act 13:40–41, Col 1:27
- 12Mrk 11:18, Jhn 7:44, Mrk 11:32, Jhn 7:30, Jhn 7:25, Mat 22:22, Luk 20:19, 1Ki 20:38–41
- 13Luk 11:54, Luk 20:20–26, Mrk 3:6, Mrk 8:15, Jer 18:18, Mat 16:6, Mat 22:15–22, Psa 140:5
- 14Jhn 7:18, 2Co 2:2, 2Co 2:17, 1Th 2:4, Gal 2:11–14, Gal 1:10, Luk 20:22, 2Co 5:16
- 15Rev 2:23, Ezk 17:2, Luk 20:23, Mat 22:18, Act 5:9, 1Co 10:9, Mrk 10:2, Jhn 2:24–25
- 16Luk 20:24–26, Mat 22:19–22, 2Ti 2:19, Rev 3:12
- 17Rom 13:7, 1Co 14:24–25, 1Pe 2:17, 2Co 5:14–15, Pro 24:21, Act 4:19–20, Mat 22:46, Job 5:12–13
- 18Act 4:1–2, Mat 22:23–33, Act 23:6–9, 2Ti 2:18, Luk 20:27–40, 1Co 15:13–18
- 19Deu 25:5–10, Rut 4:5, Gen 38:8, Rut 1:11–13
- 20Luk 20:29–33, Mat 22:25–28
- 242Ti 3:15–17, Jhn 20:9, Mat 22:29, Eph 1:19, Isa 25:8, Jer 32:17, Php 3:21, Mrk 10:27
- 25Luk 20:35–36, Mat 22:30, 1Jn 3:2, Heb 12:22–23, 1Co 15:42–54
- 26Exo 3:2–6, Luk 20:37, Gen 17:7–8, Gen 33:20, Isa 41:8–10, Gen 26:24, Exo 3:16, Gen 31:42
- 27Rom 14:9, Mrk 12:24, Rom 4:17, Heb 3:10, Heb 11:13–16
- 28Mat 22:34–40, Luk 10:25–28, Luk 20:39, Mat 5:19, Mat 19:18
- 29Deu 6:4, Luk 10:27, Gal 3:20, Rom 3:30, Jud 1:25, Jas 2:19, 1Co 8:4, Mrk 12:32–33
- 30Deu 6:5
- 31Rom 13:8–9, Mat 22:39, Lev 19:18, Luk 10:27, 1Co 13:4–8, Mat 7:12, Gal 5:14, 1Jn 4:21
- 32Deu 4:39, Deu 4:35, Isa 46:9, Isa 45:14, Deu 6:4, Isa 45:18, Isa 45:5–6, Deu 5:7
- 33Hos 6:6, Mic 6:6–8, 1Sa 15:22, Mat 12:7, Mat 9:13, 1Co 13:1–3, Amo 5:21–24, Jer 7:21–23
- 34Col 4:6, Luk 20:40, Mat 22:46, Mat 12:20, Rom 7:9, Rom 3:19–20, Gal 2:19, Tit 1:9–11
- 35Luk 20:41–44, Mat 22:41–45, Mat 26:55, Jhn 7:42, Luk 19:47, Mrk 11:27, Mat 9:27, Luk 21:37
- 36Psa 110:1, Mat 22:43–45, Heb 1:13, 1Co 15:25, Heb 10:12–13, Act 2:34–36, Act 1:16, Neh 9:30
- 37Rom 1:3–4, Jas 2:5, Mat 11:25, Mat 11:5, Jhn 12:9, Jhn 7:46–49, Luk 21:38, Rev 22:16
- 38Mat 23:1–7, Luk 20:45–47, Luk 11:43, Mat 6:5, Mrk 4:2, Luk 14:7–11, Mat 10:17
- 39Jas 2:2–3
- 40Luk 20:47, Mat 23:13, Mat 23:33, Ezk 22:25, Mat 6:7, Mic 3:1–4, Luk 12:47–48, 2Ti 3:6
- 41Luk 21:1–4, 2Ki 12:9, Jhn 8:20, Mat 27:6
- 432Co 9:6–8, 2Co 8:2, Act 11:29, 2Co 8:12, Exo 35:21–29, Mat 10:42
- 441Jn 3:17, 2Co 8:2–3, Ezr 2:68–69, Luk 21:2–4, Mrk 14:8, Luk 8:43, Luk 15:30, 2Ch 24:10–14
Parallel passages
4
- Paying Taxes to CaesarMat 22:15–22, Mrk 12:13–17, Luk 20:20–26
- The Question about the ResurrectionMat 22:23–33, Mrk 12:18–27, Luk 20:27–40
- The Greatest CommandmentMat 22:34–40, Mrk 12:28–34
- The Widow's OfferingMrk 12:41–44, Luk 21:1–4
Topics in this chapter
64
Affections, Ambition, Angel (A Spirit), Blindness, Brass, Brother, Capital and Labor, Church, Citizens, Commandments, Cornerstone, Craftiness, Eviction, Farthing, Fort, God, Hedge, Herodians, Holy Spirit, Husbandman, Hypocrisy, Immortality, Instruction, Jesus, the Christ, King, Law, Lease, Love, Malfeasance in Office, Malice, Marriage, Mite (A Lepta), Money, Neighbor, Offerings, Opinion, Public, Persecution, Poor, Prayer, Pride, Prophecy, Prophets, Quotations and Allusions, Reproof, Resurrection, Sadducees, Satire, Seasons, Self-Condemnation, Self-Denial, Servant, Stones, Stool, Temple, Tenants, Treasure-Houses, Unfaithfulness, Vineyard, Wicked (People), Widow, Wine Press, Wisdom, Women, Word of God