Marko 10
1 Isa akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Yudea. Umati mkubwa wa watu wakaenda kwake tena, naye akawafundisha, kama ilivyokuwa desturi yake.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 Isa akawajibu, “Je, Musa aliwaamuru nini?”
4 Wakajibu, “Musa aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 Isa akawaambia, “Musa aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke’.
7 ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe,
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’ Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
13 Watu walikuwa wakimletea Isa watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
14 Isa alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
17 Isa alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”
18 Isa akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’ ”
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 Isa akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Isa akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika ufalme wa Mungu!”
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Isa akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika ufalme wa Mungu.
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
27 Isa akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
29 Isa akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao.
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Isa alikuwa amewatangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Isa akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa Torati. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
38 Lakini Isa akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Isa akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 Lakini Isa akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonesha mamlaka yao.
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
46 Kisha wakafika Yeriko. Isa alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo (maana yake “mwana wa Timayo”), alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
47 Aliposikia kuwa ni Isa Al-Nasiri aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Isa, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 Isa akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Isa.
51 Isa akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
52 Isa akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Isa njiani.
Cross-references
328
- 1Jhn 10:40, Mat 4:23, Mrk 4:2, Mrk 6:34, Mrk 6:6, Jhn 11:7, Mrk 2:13, Jer 32:33
- 21Co 7:10–11, Jhn 8:6, Luk 11:53–54, Mat 23:13, Mrk 8:15, Jhn 11:47, Jhn 7:32, Luk 11:39
- 3Gal 4:21, Isa 8:20, Jhn 5:39, Luk 10:25
- 4Deu 24:1–4, Mat 5:31–32, Mat 19:7, Isa 50:1, Mat 1:19, Jer 3:1
- 5Mat 19:8, Act 7:51, Neh 9:16–17, Heb 3:7–10, Neh 9:26, Deu 31:27, Deu 9:6
- 6Gen 1:27, Gen 5:2, Gen 1:1, Gen 2:20–23, 2Pe 3:4, Mal 2:14–16, Mrk 13:19
- 7Gen 2:24, Mat 19:5–6, Eph 5:31
- 8Eph 5:28, Gen 2:24, 1Co 6:16
- 9Rom 7:1–3
- 10Mrk 9:33, Mrk 4:10, Mrk 9:28
- 11Mat 19:9, Rom 7:3, 1Co 7:10–11, Mat 5:31–32, 1Co 7:4, Luk 16:18, Heb 13:4
- 121Co 7:11, 1Co 7:13
- 13Mat 19:13–15, Luk 18:15–17, Deu 31:12–13
- 14Mat 19:14, Mat 18:4, Mat 18:10, Psa 131:1–2, 1Pe 2:2, Luk 18:15–16, 2Ti 3:15, Rev 14:5
- 15Mat 18:3, Luk 18:17, Jhn 3:3–6
- 16Isa 40:11, Mrk 9:36, Luk 2:28–34, Deu 28:3, Gen 48:14–16, Jhn 21:15–17, Luk 24:50–51
- 17Mat 19:16–30, Luk 18:18–30, Rom 2:7, Jhn 6:27–28, Luk 10:25, Rom 10:2–4, Act 16:30, Act 2:37
- 18Luk 18:19, Mat 19:17, 1Jn 4:16, Rom 3:12, 1Sa 2:2, 1Jn 4:8, Jas 1:17, Psa 119:68
- 19Exo 20:12–17, Rom 13:9, Jas 2:11, Luk 18:20, Mat 19:17–19, 1Co 6:7–9, Deu 5:16–24, Isa 8:20
- 202Ti 3:5, Ezk 33:31–32, Php 3:6, Mat 19:20, Rom 7:9, Luk 18:11–12, Luk 10:29, Mal 3:8
- 21Mat 6:19–21, Rev 2:4, Luk 18:22, 1Ti 6:17–19, Luk 10:42, Act 2:45, Jas 2:10, 1Pe 1:4–5
- 221Jn 2:15–16, 1Ti 6:9–10, Luk 12:15, Eph 5:5, 2Ti 4:10, Mat 19:22, Mat 13:22, Ezk 33:31
- 231Co 1:26, Jas 2:5, Luk 18:24, Jhn 3:5, Mat 19:23–26, 2Pe 1:11, Mrk 3:5, Mrk 10:15
- 24Pro 11:28, Jas 5:1–3, 1Ti 6:17, Psa 52:7, Rev 3:17, Pro 18:11, Luk 12:16–21, Psa 62:10
- 25Mat 19:24–25, Luk 18:25, Mat 23:24, Jer 13:23, Mat 7:3–5
- 26Act 16:31, Rom 10:9–13, 2Co 11:23, Mrk 6:51, Mrk 7:37, Luk 18:26, Luk 13:23
- 27Jer 32:27, Mat 19:26, Job 42:2, Jer 32:17, Gen 18:13–14, Luk 1:37, Luk 18:27, Num 11:21–23
- 28Mat 19:27–30, Luk 18:28–30, Mrk 1:16–20, Luk 14:33, Php 3:7–9, Mat 4:22, Mat 4:20
- 291Co 9:23, Mat 5:10–11, Heb 11:24–26, Rev 2:3, Mrk 8:35, Mat 10:18, Gen 12:1–3, Luk 22:28–30
- 30Php 3:8, Luk 18:30, 2Co 6:10, Jas 1:12, Pro 3:9–10, Mat 5:11–12, 1Ti 6:6, Pro 16:16
- 31Mat 19:30, Mat 20:16, Luk 13:30, Rom 9:30–33, Luk 18:11–14, Mat 21:31, Mat 8:11–12, Act 13:46–48
- 32Mat 20:17–19, Luk 18:31–34, Luk 9:51, Luk 10:23, Jhn 11:16, Mat 13:11, Mrk 4:34, Jhn 11:8
- 33Mat 20:17–19, Mat 27:2, Mat 16:21, Mrk 8:31, Jhn 18:28, Act 3:13–14, Jas 5:6, Jhn 19:11
- 34Mrk 14:65, Mat 26:67, Mat 16:21, Luk 22:63–65, Luk 23:11, Mrk 15:29–31, Luk 23:35–39, Mrk 15:17–20
- 35Mat 20:20–28, 2Sa 14:4–11, Mrk 14:33, Mrk 5:37, Mrk 1:19–20, 1Ki 2:20, 1Ki 2:16
- 361Ki 3:5–15, Jhn 15:7, Mrk 10:51
- 37Mat 19:28, 1Ki 22:19, Luk 24:26, Psa 110:1, Mrk 16:19, 1Pe 1:11, Mat 25:31, Mrk 8:38
- 38Luk 12:50, Mat 20:21–22, Psa 75:8, Jhn 18:11, Jas 4:3, Isa 51:22, Luk 22:42, Rom 8:26
- 39Rev 1:9, Act 12:2, Jhn 17:14, Jhn 15:20, Jhn 13:37, Mat 10:25, Mrk 14:31, Mrk 14:36
- 40Mat 20:23, Mat 25:34, Jhn 17:24, Jhn 17:2, Heb 11:16
- 41Mat 20:24, Pro 13:10, Php 2:3, Rom 12:10, Jas 4:5, Mrk 9:33–36, Luk 22:24
- 42Luk 22:25, 1Pe 5:3, Mat 20:25
- 43Mat 23:8–12, Luk 14:11, Mat 20:26–27, Mrk 9:35, Luk 9:48, Gal 5:13, 1Pe 5:5–6, Rom 12:2
- 45Mat 20:28, Php 2:5–8, 2Co 8:9, Tit 2:14, Jhn 13:14, Jhn 10:15, Luk 22:26–27, Heb 5:8
- 46Luk 18:35–19:1, Mat 20:29–34, Jhn 9:8, Luk 16:22
- 47Mrk 1:24, Mat 9:27, Mat 15:22, Rev 22:16, Act 13:22–23, Luk 18:36–37, Mat 26:71, Jhn 7:52
- 48Jer 29:13, Mrk 7:26–29, Luk 18:39, Psa 62:12, Luk 18:1–8, Luk 11:5–10, Gen 32:24–28, Mat 20:31
- 49Luk 18:40, Mat 20:32–34, Jhn 11:28, Psa 145:8, Psa 86:15, Heb 4:15, Heb 2:17
- 50Php 3:7–9, Heb 12:1
- 51Luk 18:41–43, Mat 7:7, Mrk 10:36, 2Ch 1:7, Php 4:6, Mat 6:8, Mat 23:7
- 52Mat 9:22, Act 26:18, Luk 7:50, Mrk 8:25, Mrk 5:34, Isa 42:16–18, Luk 8:2–3, Jhn 9:32
Parallel passages
2
- Jesus Blesses the ChildrenMat 19:13–15, Mrk 10:13–16, Luk 18:15–17
- The Rich Young RulerMat 19:16–30, Mrk 10:17–31, Luk 18:18–30
Topics in this chapter
69
Adultery, Ambition, Apostles, Babes, Bartimeus (Bartimaeus), Beggars, Beneficence, Bigotry, Blindness, Call, Chiding, Children, Church, Civil Service, Commandments, Confidence, Cross, David, Deacon, Divorce, Example, Faith, False Confidence, Fellowship, Gentiles, God, Hand, Heart, Homicide, Honesty, Humility, Husband, Immortality, James, Jericho, Jesus, the Christ, John, Judea, Kingdom of Heaven, Life, Man, Marriage, Minister, Christian, Miracles, Mocking, Mother, Nazareth, Needle, Obedience, Polygamy, Prayer, Presumption, Pride, Quotations and Allusions, Rabbi, Redemption, Regeneration, Reward, Rich, the, Riches, Righteous, Self-Denial, Self-Righteousness, Symbols and Similitudes, Temptation, Thankfulness, Timaeus, Works, Young Men