Nehemia 9
1 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa gunia, na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma katika kile Kitabu cha Torati ya Mwenyezi Mungu, Mungu wao, kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Mwenyezi Mungu, Mungu wao.
4 Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Mwenyezi Mungu, Mungu wao, kwa sauti kubwa.
5 Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele.” “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 Wewe peke yako ndiwe Mwenyezi Mungu. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 “Wewe ni Bwana Mwenyezi Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Ibrahimu.
8 Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 “Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 “Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti ya kweli na haki, na sheria za kweli na haki, na pia amri na maagizo mazuri.
14 Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Musa.
15 Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 “Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipokufuru sana.
19 “Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 “Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 “Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakakufuru sana.
27 Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Uliwasikia ukiwa mbinguni, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa wakombozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 “Lakini mara walipokuwa na amani, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia ukiwa mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 “Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao na kwa Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 “Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 “Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 “Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”
Перехресні посилання
282
- 1Jos 7:6, Neh 8:2, Act 13:2–3, Ezr 8:23, 1Sa 4:12, Isa 22:12, 2Ch 7:10, 2Sa 1:2
- 2Neh 13:3, Dan 9:3–10, Ezr 10:11, Neh 13:30, Dan 9:20, Hos 5:7, Ezr 9:2, Psa 144:11
- 3Neh 8:7–8, Neh 8:3–4
- 4Neh 8:7, Neh 12:8, 2Ch 20:19, Neh 10:9–13, Neh 9:5, Jhn 11:43, Psa 77:1, Act 7:60
- 5Psa 103:1–2, 1Pe 1:3, 2Co 4:6, Jer 33:10–11, Psa 106:2, Psa 117:1–2, Mat 11:25, Ezr 3:11
- 6Isa 37:16, Gen 1:1, Rev 4:11, Deu 10:14, Deu 6:4, Isa 44:6, Jer 10:11–12, Gen 2:1
- 7Gen 11:31, Gen 17:5, Isa 51:2, Act 7:2–4, Jos 24:2–3, Isa 41:8–9, Gen 15:7, Deu 10:15
- 8Heb 6:18, Gen 15:6, Gen 15:18–21, Jos 23:14, Jos 21:43–45, Gen 17:7–8, Tit 1:2, Gen 12:7
- 9Exo 3:7–9, Act 7:34, Exo 2:25, Exo 14:10–14, Exo 3:16
- 10Jer 32:20, Dan 9:15, Exo 18:11, Isa 63:12, Exo 5:2, Isa 63:14, Deu 4:34, Exo 14:1–31
- 11Psa 78:13, Exo 14:21–22, Exo 14:27–28, Psa 114:3–5, Psa 136:13–15, Isa 63:11–13, Heb 11:29, Psa 66:6
- 12Exo 13:21–22, Neh 9:19, Psa 105:39, Psa 107:7, Psa 143:8, Exo 14:19–20, Psa 78:14
- 13Psa 119:160, Exo 20:1, Exo 19:11, Psa 119:127–128, Psa 19:7–11, Ezk 20:11–13, Rom 7:12–14, Deu 5:22–26
- 14Exo 20:8–11, Gen 2:3, Ezk 20:12, Ezk 20:20, Exo 16:29, Exo 16:23, Lev 27:34, Deu 4:45
- 151Co 10:3–4, Exo 17:6, Deu 1:8, Exo 16:4, Exo 16:14–15, Jhn 6:31–35, Psa 105:40–41, Ezk 20:15
- 16Neh 9:29, Psa 81:11–14, Heb 3:15, Deu 31:27, Neh 9:10, Rom 2:5, Deu 9:23–24, Deu 9:27
- 17Psa 86:5, Jol 2:13, Psa 86:15, Psa 145:8–9, Mic 7:18–19, Num 14:18–19, Psa 78:42–43, Exo 34:6–7
- 18Psa 106:19–23, Exo 32:4–8, Ezk 20:7–44, Exo 32:31–32, Deu 9:12–16
- 19Neh 9:27, Psa 106:45, Neh 9:12, Mal 3:6, Dan 9:9, Num 14:14, Dan 9:18, Isa 44:21
- 20Psa 143:10, Num 11:17, Isa 63:11–14, Jhn 4:10, 2Pe 1:21, Isa 41:17–18, Isa 48:21, Jhn 4:14
- 21Deu 2:7, Deu 8:4, Deu 29:5, Psa 34:10, Amo 5:25, Num 14:33–34, Exo 16:35, Deu 8:2
- 22Num 21:21–35, Jos 11:23, Psa 135:10–12, Psa 136:17–22, Deu 2:26–36, Deu 3:1–17, Deu 32:26, Jos 10:11
- 23Gen 22:17, Gen 15:5, Gen 15:18, Gen 13:15–17, Gen 12:7, Gen 26:3, 1Ch 27:23, Gen 17:8
- 24Jos 21:43, Jos 18:1, Jos 11:23, Psa 44:2–3, Jos 21:45, Num 14:31, 1Ch 22:18, 2Ti 2:26
- 25Deu 32:15, Neh 9:35, Deu 3:5, 1Ki 8:66, Deu 6:10–12, Hos 3:5, Rom 2:4, Deu 32:13
- 261Ki 14:9, Jdg 2:11–12, Neh 9:18, 1Ki 18:4, 1Ki 19:10, Act 7:52, 2Ch 24:20–21, Psa 50:17
- 27Psa 106:41–45, Dan 9:10–14, 2Ki 13:5, 2Ki 14:27, Jdg 2:14–16, 1Sa 12:10–11, Deu 31:16–18, Oba 1:21
- 28Jdg 5:31–6:1, Jdg 4:1, Jdg 3:11–12, 1Ki 8:39, Jdg 3:30, 1Ki 8:33–34, Psa 106:43–45, Isa 63:15
- 29Lev 18:5, Neh 9:16, Neh 9:26, Neh 9:10, Jer 43:2, Hos 6:5, Zec 7:11–12, Jas 4:6–10
- 30Rom 2:4, 2Ch 36:15–16, Act 7:51, 2Ki 17:13–18, Isa 42:24, Isa 63:10, Isa 5:5–6, Lam 2:17
- 31Lam 3:22, Neh 9:17, Exo 34:6–7, Psa 103:8–9, Jer 4:27, Jer 5:18, Jer 5:10, Psa 145:8–9
- 32Neh 1:5, Deu 7:9, Dan 9:4, Mic 7:18–20, Dan 9:8, Psa 66:3, Dan 9:6, Psa 66:5
- 33Gen 18:25, Psa 106:6, Dan 9:5–14, Job 34:23, Jer 12:1, Job 33:27, Lam 1:18, Lev 26:40–41
- 342Ki 17:13, Jer 29:19, Deu 31:21, Neh 9:30, 2Ki 17:15
- 35Deu 28:47, Jer 5:19, Deu 32:12–15, Neh 9:25, Deu 8:7–10, Rom 3:4–5, Deu 31:21
- 36Ezr 9:9, Deu 28:48, 2Ch 12:8
- 37Deu 28:33, Deu 28:48, Ezr 7:24, Ezr 4:13, Deu 28:39, Lev 26:17, Deu 28:51, Neh 5:8
- 38Neh 10:1, 2Ch 34:31, Neh 10:29, Ezr 10:3, 2Ch 23:16, 2Ch 29:10, 2Ki 23:3, 2Ch 15:12–13
Теми в цьому розділі
57
Abraham, Afflictions and Adversities, Angel (A Spirit), Backsliders, Bani, Blessing, Bunni, Calf, Character, Chenani, Clothing, Cloud, Covenant, Decision, Earth, Fasting, Girgashites, Glory, God, Hashabniah, Heart, Heaven, Hodiah, Holy Spirit, Idolatry, Immortality, Impenitence, Ingratitude, Israel, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Kadmiel, Law, Manna, Nehemiah, Obedience, Og, Pethahiah, Praise, Prayer, Predestination, Prophets, Red Sea, Repentance, Resignation, Rulers, Sabbath, Seal, Self-Will, Shebaniah, Sherebiah, Sin, Sinai, Synagogue, Thankfulness, Ur, Wisdom