Ezekieli 20
1 Katika mwaka wa saba, mwezi wa tano siku ya kumi, baadhi ya wazee wa Israeli wakaja ili kutaka ushauri kwa Mwenyezi Mungu, wakaketi mbele yangu.
2 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
3 “Mwanadamu, sema na wazee wa Israeli uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa nini mmekuja? Je, ni kutaka ushauri kwangu? Hakika kama niishivyo, sitawaruhusu mtake ushauri toka kwangu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’
4 “Je, utawahukumu? Je, mwanadamu, utawahukumu? Basi uwakabili kwa ajili ya machukizo ya baba zao
5 na uwaambie: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Siku ile nilipochagua Israeli, niliwaapia wazao wa nyumba ya Yakobo kwa mkono ulioinuliwa nami nikajidhihirisha kwao huko Misri. Kwa mkono ulioinuliwa niliwaambia, “Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.”
6 Siku ile niliwaapia kwamba nitawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta katika nchi niliyowachagulia, nchi inayotiririka maziwa na asali, nchi nzuri kupita zote.
7 Nami nikawaambia, “Kila mmoja wenu aondolee mbali sanamu za chukizo ambazo mmekazia macho, nanyi msijitie unajisi kwa sanamu za Misri. Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.”
8 “ ‘Lakini waliniasi na hawakunisikiliza, hawakuondolea mbali sanamu za machukizo ambazo walikuwa wamezikazia macho, wala kuondolea mbali sanamu za Misri. Ndipo nikasema, nitawamwagia ghadhabu yangu na kutimiza hasira yangu dhidi yao huko Misri.
9 Lakini kwa ajili ya Jina langu niliwatoa katika nchi ya Misri. Nilifanya hivyo ili kulinda Jina langu lisinajisiwe machoni mwa mataifa walioishi miongoni mwao, na ambao machoni pao nilikuwa nimejifunua kwa Waisraeli.
10 Kwa hiyo nikawaongoza watoke Misri na kuwaleta jangwani.
11 Nikawapa amri zangu na kuwajulisha sheria zangu, kwa kuwa mtu anayezitii ataishi kwa hizo.
12 Pia niliwapa Sabato zangu kama ishara kati yangu nao, ili wapate kujua kuwa Mimi Mwenyezi Mungu niliwafanya watakatifu.
13 “ ‘Lakini watu wa Israeli waliniasi Mimi jangwani. Hawakufuata amri zangu, bali walikataa sheria zangu, ingawa mtu yule anayezitii ataishi kwa hizo sheria, nao walizinajisi Sabato zangu kabisa. Hivyo nilisema ningemwaga ghadhabu yangu juu yao na kuwaangamiza huko jangwani.
14 Lakini kwa ajili ya Jina langu nikafanya kile ambacho kitalifanya Jina langu lisitiwe unajisi machoni mwa mataifa ambao mbele yao nilikuwa nimewatoa Waisraeli.
15 Tena kwa mkono ulioinuliwa nikawaapia huko jangwani kwamba nisingewaingiza katika nchi niliyowapa, nchi inayotiririka maziwa na asali, nchi nzuri kuliko zote,
16 kwa sababu walikataa sheria zangu na hawakufuata amri zangu, na wakazinajisi Sabato zangu. Kwa kuwa mioyo yao iliandama sanamu zao.
17 Lakini niliwahurumia, wala sikuwaangamiza wala kuwafuta kabisa jangwani.
18 Niliwaambia watoto wao kule jangwani, “Msifuate amri za baba zenu wala kushika sheria zao au kujinajisi kwa sanamu zao.
19 Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu; fuateni amri zangu, tena kuweni waangalifu kushika sheria zangu.
20 Zitakaseni Sabato zangu ili ziwe ishara kati yangu nanyi. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.”
21 “ ‘Lakini watoto hao wakaniasi: Hawakufuata amri zangu, wala hawakuwa waangalifu kushika sheria zangu, ingawa mtu anayezitii anaishi kwa hizo sheria, nao wakazinajisi Sabato zangu. Hivyo nikasema ningemwaga ghadhabu yangu juu yao na kutimiza hasira yangu dhidi yao huko jangwani.
22 Lakini nikauzuia mkono wangu, na kwa ajili ya Jina langu nikafanya kile kingezuia Jina langu kunajisiwa machoni mwa mataifa ambao mbele yao nilikuwa nimewatoa Waisraeli.
23 Tena kwa mkono ulioinuliwa nikawaapia huko jangwani kwamba ningewatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali,
24 kwa sababu hawakutii sheria zangu lakini walikuwa wamekataa amri zangu na kuzinajisi Sabato zangu, nayo macho yao yakatamani sanamu za baba zao.
25 Pia niliwaacha wafuate amri ambazo hazikuwa nzuri na sheria ambazo mtu hawezi kuishi kwa hizo sheria.
26 Nikawaacha wanajisiwe kwa matoleo yao ya kuwatoa kafara wazaliwa wao wa kwanza kwa sanamu, ili nipate kuwajaza na hofu hadi wajue kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’
27 “Kwa hiyo, mwanadamu, sema na watu wa Israeli na uwaambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Katika jambo hili pia, baba zenu walinikufuru kwa kuniacha mimi:
28 Nilipowaleta katika nchi niliyokuwa nimeapa kuwapa na kuona kilima chochote kirefu au mti wowote wenye majani mengi, huko walitoa dhabihu zao, wakatoa sadaka ambazo zilichochea hasira yangu, wakafukiza uvumba wenye harufu nzuri na kumimina sadaka zao za kinywaji.
29 Ndipo nikawaambia: Ni nini maana yake hapa mahali pa juu pa kuabudia mnapopaendea?’ ” (Basi mahali pale panaitwa Bama hata leo.)
30 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Je, mtajinajisi kama vile baba zenu walivyofanya na kutamani vinyago vyao vya machukizo?
31 Mnapotoa matoleo yenu, yaani kutoa kafara watoto wenu motoni, mnaendelea kujinajisi na sanamu zenu zote hadi leo. Je, niulizwe ushauri na ninyi, ee nyumba ya Israeli? Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, mimi sitaulizwa ushauri na ninyi.
32 “ ‘Lile lililoko mioyoni mwenu kamwe halitatokea, mnaposema, “Tunataka tuwe kama mataifa mengine, kama watu wengine wa dunia, wanaotumikia miti na mawe.”
33 Hakika kama niishivyo asema Bwana Mungu Mwenyezi, nitawatawala kwa mkono wa nguvu, na kwa mkono ulionyooshwa, na kwa ghadhabu iliyomwagika.
34 Nitawatoa toka katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mlikotawanywa, kwa mkono wa nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa ghadhabu iliyomwagwa.
35 Nitawaleta katika jangwa la mataifa na huko nitatekeleza hukumu juu yenu uso kwa uso.
36 Kama nilivyowahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
37 Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, nami nitawaleta katika mkataba wa agano.
38 Nitawaondoa miongoni mwenu wale wanaohalifu na wale wanaoasi dhidi yangu. Ingawa nitawatoa katika nchi wanazoishi, hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
39 “ ‘Kwenu ninyi, ee nyumba ya Israeli, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nendeni mkatumikie sanamu zenu, kila mmoja wenu! Lakini baadaye hakika mtanisikiliza mimi nanyi hamtalinajisi tena Jina langu takatifu, kwa matoleo yenu na sanamu zenu.
40 Kwa kuwa katika mlima wangu mtakatifu, mlima mrefu wa Israeli, asema Bwana Mungu Mwenyezi, hapo katika nchi nyumba yote ya Israeli itanitumikia mimi, nami huko nitawakubali. Huko nitataka sadaka zenu na matoleo ya malimbuko yenu, pamoja na dhabihu zenu takatifu zote.
41 Nitawakubali ninyi kama uvumba wenye harufu nzuri wakati nitakapowatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mlipokuwa mmetawanyika, nami nitajionesha kuwa mtakatifu miongoni mwenu na machoni mwa mataifa.
42 Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, nchi niliyokuwa nimeapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu.
43 Hapo ndipo nitakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu yote ambayo kwayo mlijitia unajisi, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya maovu yote mliyokuwa mmetenda.
44 Nanyi mtajua kuwa mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapowatendea kwa ajili ya Jina langu, wala si sawasawa na njia zenu mbaya na matendo yenu maovu, ee nyumba ya Israeli, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
45 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
46 “Mwanadamu, uelekeze uso wako upande wa kusini, hubiri dhidi ya upande wa kusini, na utoe unabii dhidi ya msitu wa Negebu.
47 Waambie watu wa Negebu: ‘Sikieni neno la Mwenyezi Mungu. Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ninakaribia kukuwasha moto, nao utateketeza miti yako yote, mibichi na iliyokauka. Miali ya moto haitaweza kuzimwa na kila uso kutoka kusini mpaka kaskazini utakaushwa kwa moto huo.
48 Kila mmoja ataona kuwa Mimi Mwenyezi Mungu ndiye niliyeuwasha huo moto; nao hautazimwa.’ ”
49 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mungu Mwenyezi! Wao hunisema, ‘Huyu si huzungumza mafumbo tu?’ ”
Перехресні посилання
351
- 1Ezk 8:1, Ezk 29:1, Ezk 40:1, Ezk 26:1, Ezk 30:20, Ezk 24:1, Ezk 31:1, Ezk 32:1
- 3Pro 28:9, Mic 3:7, Mat 15:8–9, Psa 50:15–21, Isa 1:12, Pro 21:27, Jhn 4:24, Pro 15:8
- 4Ezk 22:2, Ezk 23:36, Jer 7:16, Ezk 14:20, Ezk 16:2–3, Isa 5:3, Jer 15:1, Act 7:51–52
- 5Ezk 20:23, Exo 3:8, Ezk 47:14, Exo 4:31, Gen 14:22, Deu 7:6, Ezk 20:15, Exo 6:6–7
- 6Jer 32:22, Ezk 20:15, Exo 3:8, Zec 7:14, Dan 8:9, Psa 48:2, Exo 3:17, Gen 15:13–14
- 7Lev 18:3, Ezk 20:8, Lev 11:44, Ezk 18:31, Deu 29:16–18, Exo 20:4, Ezk 23:3, Exo 20:2
- 8Ezk 7:8, Ezk 20:7, Isa 63:10, Ezk 20:21, Ezk 5:13, Exo 32:4–6, Deu 9:7, Ezk 20:13
- 9Ezk 39:7, Ezk 20:22, Ezk 20:14, Ezk 36:21–22, Exo 32:12, Deu 32:26–27, 1Sa 12:22, Deu 9:28
- 10Exo 15:22, Exo 20:2, Exo 14:17–22, Exo 13:17–18
- 11Rom 10:5, Lev 18:5, Luk 10:28, Deu 4:8, Gal 3:12, Ezk 20:13, Psa 147:19–20, Neh 9:13–14
- 12Ezk 20:20, Ezk 37:28, Lev 21:23, 1Th 5:23, Exo 20:8–11, Exo 19:5–6, Mrk 2:27–28, Exo 31:13–17
- 13Ezk 20:21, Ezk 20:8, Ezk 20:24, Isa 56:6, Deu 9:8, Num 14:29, Num 14:22, Exo 32:10
- 14Ezk 20:9, Ezk 20:22, Ezk 36:22–23, Eph 1:6, Eph 1:12
- 15Psa 95:11, Psa 106:26, Ezk 20:23, Heb 3:11, Heb 3:18, Heb 4:3, Deu 1:34–35, Num 14:23–30
- 16Num 15:39, Ezk 14:3–4, Ezk 20:8, Ezk 20:13–14, Amo 5:25–26, Exo 32:1–8, Num 25:2, Act 7:39–43
- 17Ezk 11:13, Jer 5:18, Jer 4:27, Ezk 8:18, 1Sa 24:10, Ezk 7:2, Neh 9:19, Psa 78:37–38
- 18Zec 1:2–4, Psa 78:6–8, Deu 4:3–6, 1Pe 1:18, Act 7:51, Ezk 20:7, Jer 2:7, Num 32:13–15
- 19Psa 105:45, Deu 5:32–6:8, Ezk 36:27, Jer 3:22–23, Psa 81:9–10, Ezk 37:24, Ezk 11:20, Deu 12:1
- 20Jer 17:22, Isa 58:13, Ezk 20:12, Exo 31:13–17, Ezk 44:24, Neh 13:15–22, Jer 17:27, Exo 20:11
- 21Ezk 20:13, Ezk 20:8, Deu 31:27, Num 21:5, Act 13:18, Ezk 21:31, Ezk 13:15, 2Ch 34:25
- 22Ezk 20:9, Ezk 20:14, Psa 78:38, Isa 48:9–11, Jer 14:21, Jer 14:7, Job 13:21, Ezk 20:17
- 23Lev 26:33, Deu 28:64–68, Psa 106:27, Ezk 20:15, Deu 32:40, Rev 10:5–6, Jer 15:4, Deu 32:26–27
- 24Ezk 20:16, Ezk 6:9, Amo 2:4, Ezk 20:13, Job 31:26–27, Deu 4:19, Ezk 18:6, Ezk 18:12
- 25Psa 81:12, Ezk 20:39, Isa 66:4, 2Th 2:9–11, Ezk 14:9–11, Ezk 20:26, Deu 4:27–28, Deu 28:36
- 26Lev 18:21, Ezk 6:7, Isa 63:17, Ezk 16:20–21, Ezk 20:31, 2Ki 17:17, Rom 11:7–10, Exo 13:12
- 27Rom 2:24, Ezk 3:27, Ezk 3:4, Ezk 2:7, Ezk 3:11, Rev 13:5, Ezk 18:24
- 28Ezk 6:13, Jos 23:14, Jer 3:6, Neh 9:22–26, Isa 57:5–7, Jer 2:7, Gen 15:18–21, Ezk 16:19
- 29Ezk 16:31, Ezk 16:24–25
- 30Jer 16:12, Jdg 2:19, Jer 7:26, Jer 9:14, Mat 23:32, Act 7:51, Num 32:14
- 31Jer 7:31, Ezk 20:26, Psa 106:37–39, Job 27:8, Pro 28:9, Jer 14:12, Mat 25:11–12, 2Ki 3:13–14
- 32Ezk 11:5, Jer 44:17, Dan 5:4, Deu 4:28, Psa 139:2, Rev 9:20, Isa 37:19, 1Sa 8:5
- 33Jer 21:5, Jer 42:18, Jer 44:6, Ezk 8:18, Lam 2:4, Dan 9:11–12
- 34Ezk 20:38, Amo 9:9–10, Ezk 34:16, Isa 27:9–13, Jer 44:6, Lam 2:4
- 35Hos 2:14, Ezk 20:36, Ezk 19:13, Rev 12:14, Ezk 17:20, Jer 2:35, Mic 7:13–15, Jer 25:31
- 36Num 11:1–35, 1Co 10:5–10, Ezk 20:13, Ezk 20:21, Psa 106:15–48, Num 14:1–45, Num 16:1–50, Num 25:1–18
- 37Jer 33:13, Lev 27:32, Mat 25:32–33, Ezk 16:59–60, Psa 89:30–32, Amo 3:2, Lev 26:25, Ezk 34:17
- 38Ezk 13:9, Psa 95:11, Amo 9:9–10, Jer 44:14, Zec 13:8–9, Ezk 6:7, Mal 3:3, Mal 4:1–3
- 39Ezk 43:7, Hos 4:17, Jdg 10:14, Ezk 20:25–26, Isa 1:13–15, 2Ki 3:13, Rev 3:15–16, Psa 81:12
- 40Isa 56:7, Mal 3:4, Isa 60:7, Ezk 17:23, 1Pe 2:5, Ezk 43:27, Isa 66:23, Ezk 37:22–28
- 41Ezk 28:25, Ezk 11:17, Ezk 38:23, Ezk 28:22, Mic 7:12–16, Jer 23:3, Ezk 39:27–29, Php 4:18
- 42Ezk 38:23, Ezk 34:13, Ezk 36:23–24, Ezk 11:17–20, Jer 24:7, Ezk 26:13, Jhn 17:3, 1Jn 5:20
- 43Ezk 6:9, Hos 5:15, Jer 31:18, Ezk 36:31, Zec 12:10–14, Neh 1:8–10, Ezk 16:61–63, Lev 26:39–41
- 44Ezk 24:24, Ezk 20:9, Ezk 20:22, Ezk 20:14, Psa 115:1, Eph 1:6, Ezk 36:21–22, 1Ti 1:16
- 46Amo 7:16, Ezk 21:2, Jer 13:19, Zec 11:1–2, Job 29:22, Jer 22:7, Mic 2:6, Ezk 4:7
- 47Jer 21:14, Isa 9:18–19, Ezk 17:24, Isa 24:1–6, Luk 23:31, Ezk 21:3–4, Isa 66:24, Ezk 15:6–7
- 48Deu 29:24–28, Lam 2:16–17, 2Ch 7:20–22, Jer 40:2–3, Jer 7:20, Isa 26:11
- 49Jhn 16:25, Mat 13:13–14, Act 17:18, Ezk 17:2