Ezra 7
1 Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
4 mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Haruni.
6 Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi katika Torati ya Musa, ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Mwenyezi Mungu, Mungu wake, alikuwa pamoja naye.
7 Baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
8 Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
9 Ezra alianza safari yake kutoka Babeli siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa kuwa mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
10 Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika Torati ya Mwenyezi Mungu na kuwafundisha Waisraeli amri na sheria zake.
11 Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alimpa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo kuhusu maagizo na amri za Mwenyezi Mungu kwa Israeli.
12 Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Torati ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
13 Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
14 Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza habari za Yuda na Yerusalemu kulingana na Torati ya Mungu wako, iliyo mkononi mwako.
15 Zaidi ya hayo, uchukue fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
16 pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao ambalo liko Yerusalemu.
17 Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
18 Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
19 Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
20 Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, unaweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
21 Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ng’ambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Torati ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
22 talanta mia moja za fedha, ngano kori mia moja, divai bathi mia moja, mafuta ya zeituni bathi mia moja, na chumvi kiasi chochote.
23 Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
24 Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
25 Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu, ili watoe haki kwa watu wote wa Ng’ambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
26 Yeyote ambaye hataitii Torati ya Mungu wenu na pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyang’anywa mali au kufungwa gerezani.
27 Ahimidiwe Mwenyezi Mungu, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Mwenyezi Mungu iliyo Yerusalemu, kwa namna hii
28 ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Mwenyezi Mungu, Mungu wangu, ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.
Перехресні посилання
156
- 1Neh 2:1, 1Ch 6:4–14, Ezr 7:21, Ezr 6:14, 2Ki 22:4, Ezr 7:12, 2Ki 22:8, 2Ch 34:9
- 21Ki 2:35, 2Sa 8:17
- 5Exo 6:25, Num 20:25–28, Jos 22:31, Jos 14:1, Num 31:31, Num 27:2, Jdg 20:28, 1Ch 6:4
- 6Ezr 8:22, Ezr 7:28, Ezr 8:31, Neh 2:18, Ezr 7:21, Mat 28:20, Neh 2:8, Ezr 8:18
- 7Ezr 8:1–20, 1Ch 25:1–8, Neh 7:45–73, 1Ch 9:17–27, Ezr 7:11–12, Neh 10:28, Neh 2:1, Ezr 6:14
- 9Ezr 7:6, Neh 2:8, Neh 2:18
- 102Ti 4:2, Mal 2:7, Mat 7:24, Jhn 13:17, Psa 1:2, Ezr 7:25, Psa 19:7, Deu 33:10
- 11Mrk 7:1–13, Ezr 7:6, Ezr 5:6, Mat 23:2, Ezr 4:11, Mat 23:13
- 12Dan 2:37, Ezk 26:7, Ezr 4:17, Dan 2:47, Rev 19:16, 1Ti 6:15, Ezr 4:10–11, 1Ki 20:1
- 13Ezr 6:1, Php 2:13, Psa 148:6, Est 3:15, Ezr 5:13, Psa 110:3, Ezr 1:3, Rev 22:17
- 14Est 1:14, Dan 6:26, Ezr 5:8, Dan 6:20, Ezr 7:25–26, Isa 8:20, Ezr 6:12, Deu 17:18–19
- 15Psa 135:21, 2Ch 6:2, Ezr 6:12, Psa 72:10, Psa 76:11, 2Ch 6:6, Psa 68:29–30, Psa 26:8
- 161Ch 29:6, 1Ch 29:9, Ezr 1:6, Ezr 1:4, 2Co 8:12, 2Co 9:7, 1Ch 29:17, Ezr 8:25–28
- 17Deu 12:5–11, Ezr 6:9–10, Num 15:4–13, Deu 14:24–26, Mat 21:12–13, Jhn 2:14
- 18Ezr 7:26, 2Ki 22:7, 2Ki 12:15, Eph 5:17
- 19Jer 3:17, 2Ch 32:19, Ezr 8:27–30, Ezr 8:33–34
- 20Ezr 6:4, Ezr 6:8–18
- 21Ezr 4:16, Ezr 7:6, Ezr 4:20, Ezr 6:6, Ezr 7:10–13
- 22Lev 2:13, Ezk 45:14, Luk 16:6–7
- 23Psa 119:4, Ezr 7:13, Zec 12:3, Ezr 7:18, Ezr 6:10–12
- 24Ezr 7:7, Ezr 4:13, Ezr 2:36–55, Ezr 4:20
- 25Deu 16:18, Ezr 7:10, Jas 1:5, Mal 2:7, Jas 3:17–18, Psa 19:7, Neh 8:7–8, Neh 13:1–3
- 26Ezr 6:11, Deu 13:1–18, Lev 20:1–27, Exo 21:1–22, Dan 6:26, 2Ch 30:12, Psa 52:5, Dan 3:28–29
- 27Ezr 6:22, Rev 17:17, Isa 60:13, 2Co 8:16, Neh 2:12, Jas 1:17, Heb 10:16, Neh 2:8
- 282Ti 4:17–18, Ezr 9:9, Ezr 5:5, Gen 32:28, Ezr 8:18, Neh 2:8, Ezr 7:9, Gen 43:14
Теми в цьому розділі
53
Amariah, Artaxerxes, Azariah, Banishment, Bath, Bukki, Cabinet, Church, Church and State, Citizens, Cor, Criminals, Ezra, Free-Will Offerings, Genealogy, God, Heart, Hilkiah, Instruction, Israel, Prophecies Concerning, Judge, Justice, King, Law, Levites, Liberality, Loyalty, Magistrate, Measure, Meraioth, Minister, Christian, Money, Month, Nethinims, Obedience, Offerings, Officer, Persia, Priest, Prison, Rulers, Seekers, Seraiah, Seven, Shallum, Tax, Temple, Thankfulness, Treasure-Houses, Uzzi, Wisdom, Zeal, Religious, Zerahiah