Ezra 3
1 Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
2 Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto, kulingana na ilivyoandikwa katika Torati ya Musa mtu wa Mungu.
3 Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Mwenyezi Mungu dhabihu za sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni.
4 Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
5 Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Mwenyezi Mungu zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mwenyezi Mungu.
6 Ingawa bado msingi wa Hekalu la Mwenyezi Mungu ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mwenyezi Mungu tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
7 Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mwerezi kupitia bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
8 Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri wa miaka ishirini na zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Mwenyezi Mungu.
9 Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
10 Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Mwenyezi Mungu, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumhimidi Mwenyezi Mungu, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
11 Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Mwenyezi Mungu hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu msingi wa nyumba ya Mwenyezi Mungu ulikuwa umewekwa.
12 Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
13 Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.
Перехресні посилання
87
- 1Act 4:32, Lev 23:24, 1Co 1:10, Neh 7:73–8:2, Zep 3:9, Exo 23:14–17, Lev 16:29, Jdg 20:1
- 2Hag 1:1, Luk 3:27, 1Ch 3:17, Ezr 2:2, Exo 20:24–25, Mat 1:12–13, Psa 78:68, Hag 1:12
- 3Ezr 4:4, Num 28:2–8, 2Ch 4:1, Ezr 8:21–22, Ezr 4:11–16, Exo 29:38–42, Psa 27:1–2, Psa 56:2–4
- 4Num 29:12–38, Neh 8:14–17, Exo 23:16, Zec 14:16–19, Jhn 7:37, Exo 29:38, Jer 52:34, Jhn 7:2
- 5Num 29:39, Exo 29:38–42, Deu 12:6, Num 28:27, Lev 1:3, Num 28:19, Deu 12:17, Num 29:8
- 71Ki 5:6, Act 9:36, Act 12:20, Jon 1:3, Act 10:5–6, 2Ki 12:11–12, Ezr 6:3–5, 2Ch 24:12–13
- 8Ezr 4:3, 1Ch 23:4, Num 4:3, 1Ch 23:24–32
- 9Ezr 2:40, Ezr 3:8, Neh 7:43
- 101Ch 25:1–7, 1Ch 15:24, 1Ch 16:37, 1Ch 15:27, Exo 28:40–42, 1Ch 16:4–7, 2Ch 35:15, 1Ch 23:5
- 11Psa 106:1, 1Ch 16:34, Psa 107:1, Psa 103:17, Psa 118:1, Jer 33:11, Psa 135:3, 2Ch 7:3
- 12Hag 2:3, Psa 126:6, Dan 2:34–35, Job 8:7, Zec 4:10, Jer 31:8–9, Mat 13:31–32, Isa 60:22
- 131Sa 4:5, Luk 19:37–40, Jer 33:11, Zec 4:7, Psa 100:1–2, Neh 12:43, 1Ki 1:40, 1Ki 1:45
Теми в цьому розділі
37
Altar, Asaph, Captivity, Cedar, Cymbal, Cyrus, Daily Offering, Ethanim, Feasts, Free-Will Offerings, Henadad, Israel, Prophecies Concerning, Jehozadak, Jeshua, Joppa, Joshua, Joy, Kadmiel, Levites, Liberality, Mason, Mediterranean Sea, Money, Month, Moon, Music, Offerings, Persia, Priest, Shealtiel, Shouting, Sidon, Tabernacles, Feast of, Temple, Trumpet, Worship, Zerubbabel