Ayubu 33
1 “Lakini Ayubu, sasa sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Перехресні посилання
230
- 1Job 13:6, Job 34:2, Mrk 4:9, Psa 49:1–3
- 2Job 3:1, Psa 78:2, Mat 5:2, Job 31:30
- 3Job 27:4, Pro 20:15, 1Th 2:3–4, Job 36:3–4, Pro 15:7, Pro 8:7–8, Psa 37:30–31, Pro 15:2
- 4Job 32:8, Gen 2:7, Job 27:3, 1Co 15:45, Job 10:12, Psa 33:6, Rom 8:2, Job 10:3
- 5Job 33:32–33, Job 13:18, Job 32:12, Job 32:1, Act 10:26, Job 32:14, Psa 50:21, Job 23:4–5
- 6Job 4:19, 2Co 5:1, Job 10:9, Gen 2:7, Exo 4:16, Job 13:12, Job 20:22, Job 9:32–35
- 7Job 13:21, Job 9:34, Psa 32:4, Psa 88:16
- 8Deu 13:14, Jer 29:23
- 9Job 16:17, Job 10:7, Job 11:4, Job 9:21, Job 29:14, Job 9:28, Job 9:17, Jer 2:35
- 10Job 19:11, Job 13:24–25, Job 14:16, Job 31:35, Job 16:9, Job 34:5, Job 30:21, Job 10:15–17
- 11Job 13:27, Job 31:4, Psa 105:18, Job 14:16, Act 16:24, Dan 4:35, Jer 20:2
- 12Ezk 18:25, Job 36:5, Job 40:8–9, Job 35:4, Job 34:17–19, Job 34:10–12, Job 34:23, Jer 18:6
- 13Job 40:2, Isa 45:9, Rom 11:34, Dan 4:35, Ezk 22:14, Psa 62:11, Job 15:25–26, Act 1:7
- 14Pro 1:24, 2Ch 33:10, Psa 62:11, Job 33:29, Luk 24:25, Jhn 3:19, Isa 6:9, Mat 13:14
- 15Num 12:6, Job 4:13, Gen 31:24, Gen 20:3, Dan 4:5, Jer 23:28, Dan 8:18, Heb 1:1
- 16Job 36:10, Job 36:15, Psa 40:6, Isa 50:5, Luk 24:45, Isa 6:10, Act 16:14, Isa 48:8
- 17Jas 4:10, Isa 2:11, 2Co 12:7, 2Ch 32:25, Gen 20:6, Mat 27:19, Job 17:11, Act 9:2–6
- 18Job 33:30, Job 33:28, 2Pe 3:9, Rom 2:4, Act 16:27–33, Job 33:24, Job 33:22, Job 15:22
- 19Job 30:17, Job 5:17–18, Psa 94:12, 1Co 11:32, Psa 119:71, Isa 37:12–13, Psa 119:67, 2Ch 16:12
- 20Job 3:24, Psa 107:17–18, Amo 5:11, Gen 3:6, Jer 3:19
- 21Job 19:20, Job 7:5, Job 13:28, Pro 5:11, Psa 102:3–5, Psa 39:11, Job 16:8, Job 14:20
- 222Sa 24:16, Job 33:28, Rev 9:11, Job 17:1, Psa 88:3–5, Job 15:21, Psa 17:4, Act 12:23
- 23Mal 3:1, Ecc 7:28, 2Co 5:20, Mal 2:7, Hag 1:13, Psa 119:75, Isa 61:1–3, Job 37:23
- 24Psa 49:7–8, Job 33:18, Mat 20:28, 1Pe 1:18–19, Zec 9:11, Exo 33:19, Mic 7:18–20, 1Ti 2:6
- 25Psa 103:5, 2Ki 5:14, Jos 14:10–11, Deu 34:7, Job 42:16, Hos 2:15
- 26Psa 50:15, Psa 30:5, Act 2:28, Act 9:11, Isa 30:19, Jud 1:24, Heb 11:26, Psa 91:15
- 27Rom 6:21, 2Sa 12:13, Psa 14:2, Rom 7:22, Mat 16:26, 1Jn 1:8–10, Jer 31:18–19, Rom 7:16
- 28Job 33:24, Job 3:9, Job 3:16, Job 33:22, Jhn 11:9, Job 3:20, Psa 69:15, Psa 49:19
- 29Eph 1:11, Php 2:13, 1Co 12:6, Heb 13:21, 2Co 5:5, 2Ki 6:10, Job 33:14–17, Col 1:29
- 30Psa 56:13, Isa 38:17, Psa 40:1–2, Job 33:28, Jhn 8:12, Isa 2:5, Psa 118:17–18, Act 26:18
- 31Job 18:2, Job 32:11, Job 21:2, Job 13:6
- 32Job 27:5, Job 21:27, Job 15:4–5, Job 22:5–9
- 33Psa 34:11, Pro 4:1–2, Job 33:3, Pro 8:5, Pro 5:1–2, Psa 49:3
Теми в цьому розділі
31
Afflictions and Adversities, Agency, Ambassadors, Blasphemy, Breath, Chastisement, Clay, Conviction, Elihu, God, Ground, Holy Spirit, Humility, Impenitence, Interpreter, Job, Joy, Man, Murmuring, Pain, Penitent, Philosophy, Prayer, Prophets, Ransom, Repentance, Righteousness, Self-Righteousness, Stocks, Wicked (People), Wisdom