Nehemia 13
1 Siku hiyo, Kitabu cha Musa kilisomwa kwa sauti kuu, na watu wote wakasikia. Humo ilionekana imeandikwa kwamba hakuna Mwamoni wala Mmoabu atakayeruhusiwa katika kusanyiko la watu wa Mungu,
2 kwa sababu hawakuwalaki Waisraeli kwa chakula na maji. Badala yake walimwajiri Balaamu kuwalaani. (Lakini hata hivyo Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka.)
3 Watu waliposikia sheria hii, waliwatenga watu wote wasio Waisraeli waliokuwa wa uzao wa kigeni.
4 Kabla ya hili, kuhani Eliashibu alikuwa amewekwa kuwa msimamizi wa vyumba vya ghala ya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano wa karibu na Tobia,
5 naye alikuwa amempa Tobia chumba kikubwa ambacho mwanzo kilikuwa kikitumika kuweka sadaka za nafaka, uvumba na vyombo vya Hekalu, pamoja na zaka za nafaka, divai mpya na mafuta waliyoagizwa Waisraeli kwa ajili ya Walawi, waimbaji na mabawabu wa lango, pamoja na matoleo kwa makuhani.
6 Lakini wakati haya yote yalipokuwa yakitendeka, sikuwa Yerusalemu, kwa kuwa katika mwaka wa thelathini na mbili wa utawala wa Artashasta mfalme wa Babeli nilikuwa nimerudi kwa mfalme. Baadaye nilimwomba ruhusa,
7 nikarudi Yerusalemu. Hapo niligundua jambo la uovu alilofanya Eliashibu kwa kumpa Tobia chumba katika nyua za nyumba ya Mungu.
8 Nilikasirika sana na nikavitupa nje vyombo vyote vya Tobia.
9 Nilitoa amri kutakasa vyumba, kisha nikavirudisha vifaa vya nyumba ya Mungu, pamoja na sadaka za nafaka na uvumba.
10 Pia niligundua kuwa mafungu yaliyopangwa kupewa Walawi hawakuwa wamepewa, nao Walawi wote na waimbaji waliowajibika kwa huduma walikuwa wamerudi katika mashamba yao.
11 Basi niliwakemea maafisa na kuwauliza, “Kwa nini nyumba ya Mungu imepuuzwa?” Kisha niliwaita pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
12 Yuda wote walileta zaka za nafaka, divai mpya na mafuta kwenye ghala.
13 Nikamweka kuhani Shelemia, mwandishi Sadoki, na Mlawi aliyeitwa Pedaya kuwa wasimamizi wa ghala, na kumfanya Hanani mwana wa Zakuri, mwana wa Matania kuwa msaidizi wao, kwa sababu watu hawa walionekana kuwa waaminifu. Walipewa wajibu wa kugawa mahitaji kwa ndugu zao.
14 Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa hili, wala usifute kile nilichokifanya kwa uaminifu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na kwa ajili ya huduma yake.
15 Siku hizo nikaona watu katika Yuda wakikanyaga mashinikizo ya divai siku ya Sabato na kuleta nafaka wakiwapakiza punda, pamoja na divai, zabibu, tini na aina nyingine za mizigo. Nao walikuwa wakileta haya yote Yerusalemu siku ya Sabato. Kwa hiyo niliwaonya dhidi ya kuuza vyakula siku hiyo.
16 Watu kutoka Tiro walioishi Yerusalemu walileta samaki na aina nyingi za bidhaa na kuziuza Yerusalemu siku ya Sabato kwa watu wa Yuda.
17 Niliwakemea wakuu wa Yuda na kuwaambia, “Ni uovu gani huu mnaofanya wa kuinajisi siku ya Sabato?
18 Je, baba zenu hawakufanya mambo kama haya, hata wakamsababisha Mungu wetu kuleta maafa haya yote juu yetu na juu ya mji huu? Sasa bado mnazidi kuchochea ghadhabu yake dhidi ya Israeli kwa kuinajisi Sabato.”
19 Vivuli vya jioni vilipoangukia juu ya malango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe, wala isifunguliwe hadi Sabato iishe. Nikawaweka baadhi ya watu wangu mwenyewe kwenye malango ili pasiwepo mzigo utakaoingizwa ndani siku ya Sabato.
20 Mara moja au mbili wachuuzi na wauzaji wa bidhaa za aina zote walilala usiku nje ya mji wa Yerusalemu.
21 Lakini niliwaonya na kuwaambia, “Kwa nini mnalala karibu na ukuta? Mkifanya hivi tena, nitawaadhibu.” Kuanzia wakati ule hawakuja tena siku ya Sabato.
22 Kisha nikawaamuru Walawi kujitakasa na kwenda kulinda malango ili kutunza Sabato iwe takatifu. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya hili pia, nawe unioneshe wema wako sawasawa na upendo wako mkuu.
23 Zaidi ya hayo, niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake kutoka Ashdodi, Amoni na Moabu.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Kiashidodi au lugha ya watu wengine, bali hawakuweza kuzungumza Kiyahudi.
25 Niliwakemea na kuwalaani. Niliwapiga baadhi ya watu na kung’oa nywele zao. Niliwaapisha kwa jina la Mungu na kusema: “Msiwaoze binti zenu kwa wana wao, wala binti zao wasiolewe na wana wenu wala ninyi wenyewe.
26 Je, Sulemani hakutenda dhambi kwa sababu ya wanawake wa aina hiyo? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwa na mfalme kama yeye. Alipendwa na Mungu wake. Naye Mungu alimweka kuwa mfalme juu ya Israeli yote, lakini hata yeye, wanawake wa mataifa mengine walimfanya atende dhambi.
27 Je, tulazimike sasa kusikia kwamba ninyi pia mmefanya uovu huu mkubwa na kutokuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni?”
28 Mmoja wa wana wa Yoyada mwana wa Eliashibu kuhani mkuu alikuwa mkwewe Sanbalati Mhoroni. Nami nilimfukuza mbele yangu.
29 Ee Mungu wangu, uwakumbuke, kwa sababu wamenajisi ukuhani, na agano la kikuhani na la Walawi.
30 Kwa hiyo niliwatakasa makuhani na Walawi kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni, na kuwapa wajibu, kila mmoja katika kazi yake.
31 Pia nilihakikisha kwamba matoleo ya kuni yaliletwa kwa wakati unaopaswa, na malimbuko kwa wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke, unitendee mema.
Перехресні посилання
185
- 1Deu 23:3–5, Neh 9:3, Neh 13:23, Deu 31:11–12, 2Ki 23:2, Ezk 25:1–11, Neh 2:19, Psa 83:7–9
- 2Deu 23:5, Jos 24:9–10, Psa 109:28, Num 23:8–11, Mic 6:5, Mat 25:40, Num 24:5–10, Num 23:18
- 3Neh 9:2, Exo 12:38, Neh 10:28, Num 11:4, Jas 1:27, Pro 6:23, Psa 119:9, Psa 19:7–11
- 4Neh 12:44, Neh 13:28, Neh 2:10, Neh 6:17–18, Neh 12:10
- 5Neh 10:38, Neh 12:44, 2Ch 34:11, Num 18:21–24
- 6Neh 5:14, Ezr 6:22, Mat 13:25, Neh 2:1, Exo 32:1, Neh 2:5–6, 2Ch 24:17–18
- 7Neh 13:5, Mat 21:12–13, Act 21:28–29, 1Co 1:11, Lam 1:10, Neh 13:1, Ezr 9:1
- 8Jhn 2:13–17, Mrk 11:15–17, Ezr 9:3–4, Ezr 10:1, Psa 69:9
- 92Ch 29:5, Neh 12:45, 2Ch 29:15–19
- 10Neh 10:37, Mal 3:8, Mal 1:6–14, Neh 12:47, Deu 12:19, 1Ti 5:17–18, Num 35:2, Neh 12:28–29
- 11Neh 10:39, Neh 13:25, Neh 13:17, Job 31:34, Pro 28:4, Mal 3:8–11, Neh 5:6–13, 1Sa 2:17
- 12Neh 10:37–39, Mal 3:10, Neh 12:44, Num 18:20–26, Lev 27:30, Deu 14:22
- 13Neh 7:2, 2Ki 22:7, 2Ki 12:15, Act 6:3, 1Co 4:2, Neh 12:44, Act 6:1, Luk 16:10–12
- 14Psa 122:6–9, Heb 6:10, Neh 13:31, Neh 13:22, Ezr 7:20, 2Ch 31:20–21, Neh 5:19, 2Ch 24:16
- 15Neh 10:31, Neh 13:21, Exo 34:21, Isa 58:13, Jer 17:21–22, Exo 20:8–11, Num 15:32–36, Deu 5:12–14
- 16Exo 23:12, Deu 5:14
- 17Neh 13:11, Neh 13:25, Mic 3:1, Jer 5:5, Psa 82:1–2, Mic 3:9, Jer 22:2–23, Pro 28:4
- 18Jer 17:21–23, Lev 26:28, Jer 44:9, Jer 17:27, Lev 26:18, Jos 22:17–18, Num 32:14, Ezk 23:26
- 19Lev 23:32, Exo 31:14–17, Jer 17:19–22
- 21Rom 13:3–4, Ezr 7:26, 1Pe 2:14, Neh 13:15
- 22Neh 12:30, Neh 13:14, Neh 13:31, 2Ki 23:4, Psa 5:7, Deu 5:12, 2Ch 29:24, Psa 130:7
- 23Ezr 9:1–2, Ezr 10:10, Neh 10:30, Neh 13:1, 2Co 6:14, Ezr 10:44, Ezr 9:11–12, Neh 4:7
- 24Zep 3:9
- 25Neh 13:17, Deu 7:3, Neh 10:29–30, Ezr 10:5, Neh 5:13, Neh 13:11, Deu 25:2–3, 2Ch 15:12–15
- 261Ki 11:1–8, Ecc 7:26, 1Ki 3:13, 2Sa 12:24–25, 2Ch 1:12, 2Ch 9:22
- 27Ezr 10:2, 1Sa 30:24
- 28Neh 2:19, Neh 12:22, Neh 12:10, Neh 3:1, Neh 6:17–19, Neh 2:10, Pro 20:8, Psa 101:8
- 29Neh 6:14, Lev 21:1–7, Num 25:12–13, Num 16:9–10, Mal 2:4–8, Psa 59:5–13, 2Ti 4:14, 1Sa 2:30
- 30Neh 10:30, Neh 12:1–26, 1Ch 23:1–26
- 31Neh 13:14, Neh 13:22, Psa 106:4, Psa 26:8–9, Neh 10:34, Psa 25:7, Luk 23:42
Теми в цьому розділі
50
Ammonites, Art, Ashdod, Backsliders, Balaam, Church, Covenant, Covetousness, Divorce, Eliashib, Ezra, Fig, Fish, Fuel, Gates, God, Hanan, Harvest, Honesty, Israel, Prophecies Concerning, Joiada, Language, Levites, Liberality, Lukewarmness, Marriage, Mattaniah, Merchant, Minister, Christian, Moabites, Nehemiah, Offerings, Pedaiah, Priest, Reproof, Sabbath, Sanballat, Scribe (S), Shelemiah, Solomon, Temptation, Tithes, Tobiah, Traffic, Treasure-Houses, Wife, Women, Works, Zadok, Zeal, Religious