Ezekieli 21
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, uelekeze uso wako juu ya Yerusalemu na uhubiri dhidi ya mahali patakatifu. Tabiri dhidi ya nchi ya Israeli
3 uiambie: ‘Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: Mimi niko kinyume nawe. Nitautoa upanga wangu kwenye ala yake na kumkatilia mbali mwenye haki na mwovu.
4 Kwa sababu nitamkatilia mbali mwenye haki na mwovu, upanga wangu utatolewa alani mwake uwe dhidi ya kila mtu kuanzia kusini hadi kaskazini.
5 Ndipo watu wote watajua ya kuwa Mimi Mwenyezi Mungu nimeutoa upanga wangu kwenye ala yake, nao hautarudi humo tena.’
6 “Kwa hiyo lia kwa uchungu, mwanadamu! Lia kwa uchungu mbele yao kwa moyo uliopondeka na kwa huzuni nyingi.
7 Nao watakapokuuliza, ‘Kwa nini unalia kwa uchungu?’ Utasema hivi, ‘Kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila moyo utayeyuka na kila mkono utalegea, kila roho itazimia na kila goti litalegea kama maji.’ Habari hizo zinakuja! Hakika zitatendeka, asema Bwana Mungu Mwenyezi.”
8 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia, kusema:
9 “Mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: “ ‘Upanga, upanga, ulionolewa na kusuguliwa:
10 umenolewa kwa ajili ya mauaji, umesuguliwa ili ung’ae kama miali ya radi! “ ‘Je, tuifurahie fimbo ya utawala ya mwanangu Yuda? Upanga unadharau kila fimbo kama hiyo.
11 “ ‘Upanga umewekwa tayari ili kusuguliwa, ili upate kushikwa mkononi, umenolewa na kusuguliwa, umewekwa tayari kwa mkono wa muuaji.
12 Piga kelele na uomboleze, ee mwanadamu, kwa kuwa upanga u dhidi ya watu wangu; u dhidi ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa wauawe kwa upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo pigapiga kifua chako.
13 “ ‘Lazima kuwe na kujaribiwa. Itakuwaje basi ikiwa fimbo ya ufalme ya Yuda inayodharauliwa na upanga haitakuwepo tena? asema Bwana Mungu Mwenyezi.’
14 “Hivyo basi, mwanadamu, tabiri na ukapige makofi. Upanga wako na upige mara mbili, naam, hata mara tatu. Ni upanga wa mauaji, upanga wa mauaji makuu, ukiwashambulia kutoka kila upande.
15 Ili mioyo ipate kuyeyuka na wanaouawa wawe wengi, nimeweka upanga wa mauaji kwenye malango yao yote. Lo! Umetengenezwa umetemete kama miali ya radi, umeshikwa kwa ajili ya kuua.
16 Ee upanga, kata upande wa kuume, kisha upande wa kushoto, mahali popote makali yako yatakapoelekezwa.
17 Mimi nami nitapiga makofi, nayo ghadhabu yangu itapungua. Mimi Mwenyezi Mungu nimesema.”
18 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
19 “Mwanadamu, weka alama njia mbili ambazo upanga wa mfalme wa Babeli utapitia, njia hizo zikianzia katika nchi hiyo hiyo. Weka kibao pale ambapo njia zinagawanyika kuelekea mjini.
20 Weka alama njia moja kwa ajili ya upanga upate kuja dhidi ya Raba ya Waamoni na nyingine upate kuja dhidi ya Yuda na Yerusalemu iliyozungushiwa ngome.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli sasa amesimama katika njia panda, katika makutano ya njia mbili, akipiga ramli: anapiga kura kwa kutumia mishale, anataka shauri kwa sanamu zake, anachunguza maini ya wanyama.
22 Upande wake wa kuume inakuja kura ya Yerusalemu, ambapo ataweka magogo ya kubomoa, ili kuamrisha mauaji, kupiga ukelele wa vita, kuweka magogo ya kubomoa dhidi ya malango, kupandisha kilima hadi kuta zako, na kujenga husuru dhidi yako.
23 Itakuwa kama kupiga ramli kwa uongo kwa wale watu ambao wameapa kumtii yeye. Lakini mfalme wa Babeli atawakumbusha kuhusu uovu wao na kuwachukua mateka.
24 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: ‘Kwa sababu ninyi mmefanya uovu wenu ukumbukwe kwa kuasi waziwazi, mkidhihirisha dhambi zenu katika yale yote mnayoyafanya: kwa kuwa mmefanya hivi, mtachukuliwa mateka.
25 “ ‘Ee mtawala kafiri na mwovu wa Israeli, ambaye siku yake imewadia, ambaye wakati wake wa adhabu umefikia kilele chake;
26 hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Vua kilemba, ondoa taji. Kwa kuwa mambo hayatakuwa vile yalivyokuwa. Aliye mnyonge atakwezwa, na aliyekwezwa atashushwa.
27 Mahame! Mahame! Nitaufanya mji kuwa mahame! Hautajengwa upya hadi aje yule aliye mwenye taji kwa haki; huyo ndiye nitakayempa.’
28 “Nawe, mwanadamu, tabiri na useme, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kuhusu Waamoni na matukano yao: “ ‘Upanga, upanga, umefutwa kwa ajili ya kuua, umesuguliwa ili kuangamiza na unametameta kama miali ya radi!
29 Wakati wanatoa maono ya uongo juu yako, na wanapobashiri uongo juu yako, upanga utawekwa kwenye shingo za wapotovu watakaouawa, wale siku yao imewadia, wakati wa adhabu yao ya mwisho.
30 “ ‘Urudishe upanga kwenye ala yake! Katika mahali ulipoumbiwa, katika nchi ya baba zako, huko nitakuhukumu.
31 Nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kupuliza moto wa hasira yangu dhidi yako; nitakutia mikononi mwa watu wakatili, watu stadi katika kuangamiza.
32 Mtakuwa kuni za kuwashia moto, damu yenu itamwagwa katika nchi yenu, wala hamtakumbukwa tena; kwa maana Mimi Mwenyezi Mungu nimesema.’ ”
Перехресні посилання
209
- 2Ezk 20:46, Ezk 4:7, Ezk 28:21, Ezk 25:2, Mic 2:11, Ezk 29:2, Jer 26:11–12, Eph 6:19
- 3Job 9:22, Jer 21:13, Ezk 5:8, Ezk 14:21, Nam 2:13, Ezk 21:19, Ezk 5:12, Nam 3:5
- 4Ezk 20:47, Ezk 7:2, Ezk 6:11–14
- 5Ezk 21:30, Nam 1:9, Ezk 20:48, Jer 23:20, 1Sa 3:12, Deu 29:24–28, Isa 55:11, Num 14:21–23
- 6Isa 22:4, Ezk 6:11, Hab 3:16, Ezk 4:12, Ezk 21:12, Ezk 9:4, Ezk 37:20, Nam 2:10
- 7Ezk 7:17, Ezk 7:26, Jer 50:43, Heb 12:12, Nam 2:10, Isa 13:7, Ezk 12:22–28, Deu 20:8
- 9Ezk 21:28, Isa 34:5–6, Ezk 21:3, Amo 9:4, Job 20:25, Ezk 21:15, Isa 27:1, Psa 7:11–13
- 10Psa 110:5–6, Ezk 20:47, Psa 89:26–32, Est 3:15, Isa 34:5–6, Ecc 3:4, Nam 1:10, Hab 3:11
- 11Ezk 21:19, Jer 25:9, Jer 51:20–23, Jer 25:33
- 12Ezk 21:6, Jol 1:13, Jer 31:12, Ezk 21:14, Ezk 6:11, Ezk 9:8, Ezk 30:2, Jer 25:34
- 13Ezk 21:25, Ezk 21:10, 2Co 8:2, Job 9:23
- 14Num 24:10, 2Ki 24:1, 2Ki 24:10–16, Lev 26:21, Ezk 6:11, Lev 26:24, Amo 9:2, 1Ki 22:25
- 15Jer 17:27, Ezk 21:10, Ezk 21:22, Ezk 21:7, Ezk 15:7, Psa 22:14, Ezk 20:47, Ezk 21:28
- 16Ezk 16:46, Ezk 21:20, Ezk 14:17, Gen 13:9, Ezk 21:4
- 17Ezk 5:13, Ezk 21:14, Zec 6:8, Ezk 22:13, Deu 28:63, Ezk 16:42, Num 24:10, Isa 1:24
- 19Ezk 4:1–3, Jer 1:10, Ezk 5:1–17
- 20Amo 1:14, Jer 49:2, Deu 3:11, Ezk 25:5, Psa 48:12–13, Psa 125:1–2, Lam 4:12, 2Sa 12:26
- 21Pro 16:33, Jdg 17:5, Jdg 18:20, Gen 31:30, Act 16:16, Gen 31:19, Num 23:23, Jdg 18:24
- 22Ezk 4:2, Ezk 26:9, Jer 51:14, Job 39:25, Jer 52:4, Exo 32:17–18, Jer 32:24, Jos 6:20
- 23Num 5:15, Ezk 21:24, Ezk 29:16, Ezk 12:22, 2Ch 36:13, Ezk 17:13–19, Rev 16:19, Isa 28:14–15
- 24Hos 4:2, Amo 9:1–3, Jer 9:2–7, Ezk 24:7, Ezk 22:3–12, Isa 3:9, Isa 22:17–18, Jer 8:12
- 25Ezk 35:5, Jer 52:2, Ezk 21:29, Ezk 17:19, 2Ch 36:13, Ezk 30:3, Psa 7:9, Ezk 7:6
- 26Ezk 17:24, Psa 75:7, Jer 52:31–34, Jer 13:18, Ezk 16:12, Luk 1:52, Jer 52:9–11, 1Sa 2:7–8
- 27Mic 5:2, Jer 23:5–6, Luk 1:32, Zec 9:9, Psa 2:6, Mat 28:18, Jhn 1:9, Hag 2:21–22
- 28Ezk 21:20, Ezk 21:9–10, Zep 2:8–10, Jer 49:1–5, Ezk 25:2–7, Amo 1:13–15, Jer 12:12
- 29Ezk 21:25, Ezk 22:28, Psa 37:13, Jer 27:9, Isa 47:13, Lam 2:14, Ezk 13:10, Isa 44:25
- 30Gen 15:14, Jer 47:6–7, Ezk 16:38, Ezk 21:4–5, Ezk 28:13, Ezk 16:3–4, Ezk 28:15
- 31Ezk 14:19, Jer 4:7, Psa 18:15, Nam 1:6, Hag 1:9, Ezk 7:8, Isa 30:33, Jer 6:22–23
- 32Ezk 25:10, Mal 4:1, Ezk 20:47–48, Num 23:19, Isa 34:3–7, Mat 3:12, Mat 24:35, Zep 2:9