Ayubu 39
1 “Je, unajua wakati mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, unatambua wakati kulungu jike anapozaa mtoto wake?
2 Je, unaweza kuhesabu miezi hadi wanapozaa? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; uchungu wa kuzaa unakoma.
4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7 Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
9 “Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
10 Je, unaweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15 bila kujali kuwa mguu unaweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
19 “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22 Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23 Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaong’aa na fumo.
24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, husikia sauti ya mtoa amri na kelele za vita.
26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
29 Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
30 Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”
Перехресні посилання
132
- 1Psa 29:9, 1Sa 24:2, Psa 104:18, Jer 14:5, Deu 14:5
- 2Jer 2:24
- 5Job 6:5, Job 11:12, Job 24:5, Psa 104:11, Gen 49:14, Jer 14:6, Hos 8:9, Isa 32:14
- 6Psa 107:34, Job 24:5, Jer 2:24, Jer 17:6, Deu 29:23, Ezk 47:11, Hos 8:9
- 7Job 3:18, Exo 5:18, Isa 58:3, Isa 31:4, Job 39:18, Exo 5:13–16
- 8Psa 145:15–16, Psa 104:27–28, Job 40:20–22, Gen 1:29–30, Job 40:15
- 9Num 23:22, Psa 92:10, Deu 33:17, Psa 22:21, Isa 1:3
- 10Job 39:7, Job 39:5, Psa 129:3, Hos 10:10–11, Job 1:14, Mic 1:13, Job 41:5
- 11Gen 1:28, Psa 144:14, Psa 33:16–17, Psa 20:7, Gen 42:26, Psa 147:10, Isa 31:1–3, Isa 30:16
- 12Amo 2:13, Neh 13:15, Pro 3:16, Mat 3:2, Hag 2:19, Mat 13:30
- 13Jer 8:7, Zec 5:9, Job 30:29, Psa 104:17, 1Ki 10:22, 2Ch 9:21, Lev 11:19
- 16Lam 4:3, Rom 1:31, 1Ki 3:26–27, Ecc 10:15, Lam 2:20, Hab 2:13, 2Ki 6:28–29, Deu 28:56–57
- 17Job 35:11, 2Ch 32:31, Deu 2:30, Jas 1:17, Isa 19:11–14, Job 17:4, Isa 57:17
- 18Job 39:22, Job 39:7, Job 5:22, Job 41:29, 2Ki 19:21
- 19Psa 104:1, Psa 147:10, Psa 93:1, Mrk 3:17, Exo 15:1, Job 39:25
- 20Jer 8:16, Jol 2:5, Job 41:20–21
- 21Jer 8:6, 1Sa 17:42, 1Sa 17:4–10, Jer 9:23, Jdg 5:22, Pro 21:31, Psa 19:5
- 22Job 39:18, Job 41:33, Job 39:16
- 23Job 41:26–29
- 24Amo 3:6, Job 9:16, Job 29:24, Jer 4:19, Luk 24:41, Job 37:20, Hab 1:8–9
- 25Ezk 36:2, Ezk 26:2, Psa 70:3
- 26Jer 8:7, Lev 16:11, Deu 14:15, Sng 2:12
- 27Oba 1:4, Jer 49:16, Exo 19:4, Lev 11:13, Isa 40:31, Pro 23:5, Psa 103:5, Hos 8:1
- 281Sa 14:4
- 29Job 9:26
- 30Mat 24:28, Luk 17:37, Ezk 39:17–19