Habakuki 3
1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
2 Mwenyezi Mungu, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Mwenyezi Mungu. Fufua kazi yako katika siku hizi zetu, tangaza habari yako wakati huu wetu; katika ghadhabu kumbuka rehema.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
4 Mng’ao wake ulikuwa kama jua linapochomoza; miali ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
8 Ee Mwenyezi Mungu, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya vita ili ushinde?
9 Uliufunua upinde wako na kuitisha mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mng’ao wa mishale yako inayoruka, na katika mng’ao wa mkuki wako umeremetao.
12 Kwa ghadhabu ulipitia kwenye dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyempaka mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ng’ombe katika zizi,
18 hata hivyo nitashangilia katika Mwenyezi Mungu, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
19 Bwana Mungu Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Перехресні посилання
140
- 1Psa 86:1–17, Psa 7:1–17, Psa 90:1–17
- 2Psa 85:6, Psa 90:13–17, Hos 6:2–3, Lam 3:32, Isa 51:9–11, Isa 63:15–64:4, Php 1:6, Hab 3:16
- 3Deu 33:2, Psa 4:4, Oba 1:9, Amo 1:12, Psa 68:17, Rev 5:13–14, Isa 6:3, Jer 49:7
- 4Mat 17:2, Isa 60:19–20, Rev 22:5, Job 26:14, Exo 14:20, Psa 104:2, 1Ti 6:16, Exo 13:21
- 5Exo 12:29–30, Num 16:46–49, Num 14:12, Psa 18:7–13, Deu 32:24, Nam 1:2–3, Psa 78:50–51
- 6Gen 49:26, Nam 1:5, Deu 33:15, Mic 5:8, Isa 64:1–3, Zec 14:4–5, Isa 51:6, Jos 11:18–23
- 7Exo 15:14–16, Jos 9:24, Jdg 7:24–25, Gen 25:1–4, Jos 2:10, Num 31:2–12, Psa 83:5–10, Num 22:3–4
- 8Psa 68:17, Deu 33:26–27, Psa 114:5, Exo 14:21–22, Isa 50:2, Psa 18:10, Psa 114:3, Nam 1:4
- 9Psa 7:12–13, Psa 78:15–16, Psa 105:41, Luk 1:72–75, 1Co 10:4, Heb 6:13–18, Deu 32:23, Psa 143:6
- 10Jer 4:24, Jos 4:23–24, Psa 93:3, Psa 98:7–8, Isa 43:20, Heb 11:29, Jos 4:18, Mat 27:51
- 11Psa 144:5–6, Jos 10:11–13, Psa 18:12–14, Isa 28:21, Isa 38:8, Psa 77:17–18, Psa 19:4
- 12Jer 51:33, Mic 4:12–13, Num 21:23–35, Isa 41:15, Jos 6:1–12, Act 13:19, Psa 44:1–3, Amo 1:3
- 13Psa 110:6, Psa 105:15, Jos 10:42, Exo 15:1–2, Psa 20:6, Jos 11:12, Jos 10:11, Psa 68:19–23
- 14Zec 9:14, Dan 11:40, Psa 118:10–12, Exo 14:5–9, Psa 10:8, Exo 15:9–10, Exo 11:4–7, Exo 1:10–16
- 15Psa 77:19, Hab 3:8, Exo 15:8
- 16Jer 23:9, Hab 1:5–11, Hab 3:2, Dan 10:8, Psa 119:120, Jer 45:3–5, Jer 25:9–11, 2Th 1:6–9
- 17Jol 1:16–18, Jer 5:17, Deu 28:30–41, Deu 28:15–18, Amo 4:6–10, Hag 2:16–17, Jol 1:10–13, Jer 14:2–8
- 18Job 13:15, Php 4:4, Mic 7:7, Isa 61:10, Isa 12:2, Rom 5:2–3, Psa 25:5, Psa 46:1–5
- 192Sa 22:34, Psa 18:33, Php 4:13, Psa 46:1, Deu 32:13, Psa 27:1, Isa 58:14, 2Co 12:9–10