Ezekieli 13
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wa Israeli wanaotabiri sasa. Waambie hao ambao hutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe: ‘Sikia neno la Mwenyezi Mungu!
3 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ole wao manabii wapumbavu wafuatao roho yao wenyewe na wala hawajaona chochote!
4 Manabii wako, ee Israeli, ni kama mbweha katikati ya magofu.
5 Hamjakwea kwenda kuziba mahali palipobomoka katika ukuta ili kuukarabati kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili isimame imara kwenye vita katika siku ya Mwenyezi Mungu.
6 Maono yao ni ya uongo na ubashiri wao ni wa udanganyifu. Wao husema, “Mwenyezi Mungu amesema”, wakati Mwenyezi Mungu hakuwatuma; bado wakitarajia maneno yao kutimizwa.
7 Je, hamjaona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu, hapo msemapo, “Mwenyezi Mungu asema”, wakati Mimi sijasema?
8 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa sababu ya maneno yenu ya uongo na maono yenu ya udanganyifu, Mimi niko kinyume nanyi, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
9 Mkono wangu utakuwa dhidi ya manabii ambao huona maono ya uongo na kusema ubashiri wa udanganyifu. Hawatakuwa katika baraza la watu wangu au kuorodheshwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli, wala hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mungu Mwenyezi.
10 “ ‘Kwa sababu wanapotosha watu wangu, wakisema, “Amani”, wakati hakuna amani; pia kwa sababu, wakati ukuta dhaifu unapojengwa, wanaufunika kwa kupaka chokaa,
11 kwa hiyo waambie hao wanaoupaka chokaa isiyokorogwa vyema kwamba ukuta huo utaanguka. Mvua kubwa ya mafuriko itanyesha, nami nitaleta mvua ya mawe inyeshe kwa nguvu, nao upepo wa dhoruba utavuma juu yake.
12 Ukuta utakapoanguka, je, watu hawatawauliza, “Iko wapi chokaa mliyopaka ukuta?”
13 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Katika ghadhabu yangu nitauachia upepo wa dhoruba, na katika hasira yangu, mvua ya mawe na ya mafuriko itanyesha, ikiwa na ghadhabu ya kuangamiza.
14 Nitaubomoa ukuta mlioupaka chokaa na kuuangusha chini ili msingi wake uwe wazi. Utakapoanguka, mtaangamizwa ndani yake, nanyi mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
15 Hivyo ndivyo nitakavyoitimiza ghadhabu yangu dhidi ya huo ukuta na dhidi yao walioupaka chokaa. Nitawaambia ninyi, “Ukuta umebomoka na vivyo hivyo wale walioupaka chokaa,
16 wale manabii wa Israeli walioitabiria Yerusalemu na kuona maono ya amani kwa ajili yake wakati hakukuwa na amani, asema Bwana Mungu Mwenyezi.” ’
17 “Sasa, mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya binti za watu wako wanaotabiri mambo kutoka mawazo yao wenyewe. Tabiri dhidi yao
18 na useme, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ole wao wanawake washonao hirizi za uchawi juu ya viwiko vyao vyote na kutengeneza shela za urefu wa aina mbalimbali kwa ajili ya kufunika vichwa vyao kwa makusudi ya kuwanasa watu. Je, mtatega uhai wa watu wangu lakini ninyi mponye wa kwenu?
19 Ninyi mmeninajisi miongoni mwa watu wangu kwa ajili ya konzi chache za shayiri na chembe za mkate. Kwa kuwanenea uongo watu wangu, ambao husikiliza uongo, mmewaua watu ambao hawakustahili kufa, na kuwaacha hai wale ambao walistahili kufa.
20 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Niko kinyume na hizo hirizi zenu za uchawi mnazotumia kuwatega watu kama ndege, nami nitazirarua mikononi mwenu; nitawaweka huru watu mliowatega kama ndege.
21 Nitazirarua shela zenu na kuwaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu, nao hawatakuwa tena mawindo ya nguvu zenu. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
22 Kwa sababu mliwavunja moyo wenye haki kwa uongo wenu, wakati mimi sikuwaletea huzuni na kwa kuwa mliwatia moyo waovu ili wasiziache njia zao mbaya na hivyo kuokoa maisha yao,
23 kwa hiyo hamtaona tena maono ya uongo wala kufanya ubashiri. Nitawaokoa watu wangu kutoka mikononi mwenu. Nanyi ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
Перехресні посилання
155
- 2Ezk 13:17, Jer 37:19, Isa 1:10, Ezk 22:28, Isa 9:15, Ezk 22:25, Zep 3:4, Jer 6:13–14
- 3Lam 2:14, Jer 23:28–32, Hos 9:7, Pro 15:14, Mat 23:13–29, Jer 23:1, Ezk 34:2, Zec 11:15
- 4Rev 19:20, 2Co 11:13–15, Tit 1:10–12, Mat 7:15, Rev 13:11–14, Mic 3:5, 2Th 2:9–10, Sng 2:15
- 5Ezk 22:30, Psa 106:23, Isa 58:12, Isa 13:6, Isa 13:9, Jer 23:22, Zep 2:2–3, 2Pe 3:10
- 6Jer 29:8, Ezk 22:28, Jer 28:15, Ezk 21:29, Jer 37:19, Zec 10:2, Jer 14:14, Jer 23:31–32
- 7Ezk 13:2–3, Ezk 13:6, Mat 24:23–24
- 8Ezk 5:8, Ezk 21:3, Nam 2:13, Ezk 35:3, Ezk 26:3, Ezk 28:22, 1Ti 4:8, Ezk 29:3–4
- 9Psa 87:6, Psa 69:28, Ezr 2:59, Jer 28:15–17, Ezk 20:38, Dan 12:1, Jer 20:3–6, Psa 101:7
- 10Ezk 13:16, Ezk 22:28, Jer 8:11, Jer 14:13, Jer 6:14, 2Ki 21:9, 2Ti 3:13, Jer 5:31
- 11Ezk 38:22, Isa 28:2, Isa 32:19, Isa 25:4, Nam 1:3, Job 27:21, Mat 7:25, Luk 6:48–49
- 12Jer 37:19, Jer 2:28, Jer 29:31–32, 2Ki 3:13, Deu 32:37, Jdg 9:38, Lam 2:14–15, Jdg 10:14
- 13Isa 30:30, Rev 16:21, Rev 11:19, Psa 148:8, Psa 18:12–13, Jer 23:19, Rev 8:7, Exo 9:18–29
- 14Jer 6:15, Mic 1:6, Jer 14:15, Ezk 13:9, Ezk 13:23, Hab 3:13, Ezk 13:21, Jer 23:15
- 15Isa 30:13, Psa 62:3, Neh 4:3
- 16Jer 6:14, Ezk 13:10, Jer 8:11, Jer 5:31, Isa 48:22, Jer 29:31, Isa 57:20–21, Jer 28:1
- 17Ezk 13:2, Rev 2:20, Jdg 4:4, 2Ki 22:14, Luk 2:36, Ezk 4:3, Isa 4:4, Ezk 20:46
- 182Pe 2:14, Ezk 13:20, Jer 6:14, 2Ti 4:3, Ezk 22:25, Ezk 13:10, Jer 4:10, Ezk 13:16
- 19Mic 3:5, Pro 28:21, Jer 23:17, Jer 23:14, Ezk 20:39, Ezk 22:26, Rom 16:18, Mic 3:11
- 20Ezk 13:18, 2Ti 3:8–9, Ezk 13:8–9, Ezk 13:15–16
- 21Psa 91:3
- 22Jer 23:14, Jer 14:13–17, Ezk 9:4, 2Pe 2:18–19, Ezk 13:16, Jer 23:17, Gen 3:4–5, Ezk 18:21
- 23Ezk 13:21, Mic 3:6, Ezk 12:24, Rev 12:11, Rev 12:9, Ezk 34:10, Zec 13:3, Deu 18:20