Ezekieli 43
1 Kisha yule mtu akanileta kwenye lango linaloelekea upande wa mashariki,
2 nami nikaona utukufu wa Mungu wa Israeli ukija kutoka upande wa mashariki. Sauti yake ilikuwa kama ya ngurumo ya maji yaendayo kasi, nayo nchi ikang’aa kwa utukufu wake.
3 Maono niliyoyaona yalikuwa kama maono yale niliyokuwa nimeyaona wakati Mungu alipokuja kuangamiza mji na kama maono niliyokuwa nimeyaona kando ya Mto wa Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.
4 Utukufu wa Mwenyezi Mungu ukaingia hekaluni kupitia lango linaloelekea upande wa mashariki.
5 Kisha Roho wa Mungu akanichukua na kunileta katika ule ua wa ndani, nao utukufu wa Mwenyezi Mungu ulilijaza Hekalu.
6 Yule mtu akiwa amesimama kando yangu, nilisikia mtu mmoja akisema nami kutoka ndani ya Hekalu.
7 Akasema, “Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi, na mahali pa kuweka nyayo za miguu yangu. Hapa ndipo nitakapoishi miongoni mwa Waisraeli milele. Kamwe nyumba ya Israeli hawatalinajisi tena Jina langu takatifu, yaani wao wala wafalme wao, kwa ukahaba wao na kwa sanamu zao zisizokuwa na uhai za wafalme wao katika mahali pao pa juu pa kuabudia.
8 Walipoweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu na miimo yao ya milango karibu na miimo yangu, pakiwa na ukuta tu kati yangu na wao, walilinajisi Jina langu takatifu kwa matendo yao ya machukizo. Kwa sababu hiyo niliwaangamiza kwa hasira yangu.
9 Basi sasa na waweke mbali nami ukahaba wao na sanamu za wafalme wao zisizo na uhai, nami nitakaa miongoni mwao milele.
10 “Mwanadamu, elezea hilo Hekalu kwa watu wa Israeli, ili wapate kuona aibu kwa ajili ya dhambi zao. Wao na wapime hicho kielelezo.
11 Wakishaona aibu kwa ajili ya yale yote waliyotenda, wafahamishe kielelezo cha hilo Hekalu, yaani mpangilio wake, maingilio yake ya kutoka na kuingia, kielelezo chake chote, na masharti yake yote na sheria zake zote. Yaandike haya mbele yao ili wapate kuwa waaminifu kwa hicho kielelezo chake na kufuata masharti yake yote.
12 “Hii ndiyo sheria ya Hekalu: Eneo lote linalozunguka Hekalu juu ya mlima litakuwa takatifu kuliko yote. Hii ndiyo sheria ya Hekalu.
13 “Hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ndefu, yaani dhiraa moja na nyanda nne: Tako lake liwe na kina cha hiyo dhiraa moja, na upana wa hiyo dhiraa moja, ikiwa na ukingo wa shibiri moja kuizunguka pembeni. Hiki kitakuwa ndicho kimo cha madhabahu:
14 Kimo cha msingi kuanzia usawa wa ardhi hadi kwenye mfereji sehemu ya chini kimo chake ni dhiraa mbili na upana wake ni dhiraa moja na kuanzia kwenye ukingo mdogo hadi kwenye ukingo mpana kimo chake ni dhiraa nne na upana wake ni dhiraa moja.
15 Pale panapowashwa moto madhabahuni kimo chake kitakuwa dhiraa nne, na pembe nne zinazoelekeza juu kutoka pale panapowashwa moto.
16 Pale panapowashwa moto pa madhabahu ni mraba, urefu wake ni dhiraa kumi na mbili na upana wa dhiraa kumi na mbili.
17 Pia sehemu ya juu ni mraba, urefu wake dhiraa kumi na nne na upana wa dhiraa kumi na nne, ikiwa na ukingo wa nusu dhiraa na mfereji kuizunguka madhabahu. Ngazi za kupandia madhabahuni zitaelekea upande wa mashariki.”
18 Kisha akaniambia, “Mwanadamu, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Haya ndio yatakayokuwa masharti ya kutoa dhabihu za kuteketezwa na kunyunyiza damu juu ya madhabahu itakapokuwa imejengwa.
19 Utatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya dhambi kwa makuhani, ambao ni Walawi, wa jamaa ya Sadoki, ndio watakaonikaribia kuhudumu mbele zangu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
20 Itakupasa kuchukua sehemu ya hiyo damu ya mnyama huyo, na kuiweka juu ya hizo pembe nne za madhabahu, na juu ya ncha zake nne za sehemu ya juu kuzunguka ukingo wote, ili kuitakasa madhabahu, na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 Itakupasa kumchukua huyo fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi na kumteketeza mahali palipoagizwa katika eneo la Hekalu nje ya mahali Patakatifu.
22 “Siku ya pili yake utamtoa beberu asiye na dosari kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nayo madhabahu itatakaswa kama ilivyotakaswa kwa yule fahali.
23 Utakapokuwa umemaliza kazi ya kuitakasa, utamtoa fahali mchanga pamoja na kondoo dume toka kwenye kundi, wote wawe hawana dosari.
24 Utawatoa mbele za Mwenyezi Mungu, nao makuhani watanyunyizia chumvi juu yao na kuwatoa kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Mwenyezi Mungu.
25 “Kwa siku saba itakupasa kutoa beberu kila siku kwa ajili ya sadaka ya dhambi, pia itakupasa kutoa fahali mchanga na kondoo dume kutoka zizini, wote wawe hawana dosari.
26 Kwa siku saba itawapasa kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuitakasa; hivyo ndivyo watakavyoiweka wakfu.
27 Mwishoni mwa hizi siku saba, kuanzia siku ya nane na kuendelea, itawapasa makuhani kutoa sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za amani juu ya madhabahu. Kisha nitawakubali ninyi, asema Bwana Mungu Mwenyezi.”
Перехресні посилання
160
- 1Ezk 44:1, Ezk 42:15, Ezk 40:6, Ezk 46:1, Ezk 10:19, Ezk 43:4
- 2Rev 18:1, Ezk 11:23, Isa 6:3, Rev 14:2, Ezk 10:18–19, Rev 1:15, Ezk 1:28, Ezk 10:4
- 3Ezk 9:5, Ezk 9:1, Jer 1:10, Ezk 3:23, Ezk 32:18, Ezk 1:3–28, Ezk 9:3, Ezk 8:4
- 4Ezk 10:18–19, Ezk 44:2, Ezk 43:2
- 52Co 12:2–4, Ezk 11:24, 1Ki 8:10–11, Ezk 8:3, Ezk 44:4, Act 8:39, Ezk 3:12–14, Ezk 37:1
- 6Ezk 40:3, Isa 66:6, Rev 16:1, Lev 1:1
- 7Ezk 43:9, Psa 47:8, Lev 26:30, 1Ch 28:2, Psa 99:1, Ezk 20:39, Ezk 1:26, Rev 22:3
- 8Ezk 5:11, Ezk 23:39, Ezk 8:3–16, 2Ch 33:4, Ezk 44:7, 2Ch 33:7, 2Ki 21:4–7, 2Ki 16:14–15
- 9Ezk 43:7, Ezk 37:26–28, Ezk 18:30–31, Col 3:5–9, 2Co 6:16, Ezk 37:23, Hos 2:2
- 10Ezk 40:4, Ezk 16:61, Ezk 43:11, Ezk 16:63, Exo 25:40, Rom 6:21, Ezk 23:31–32, 1Ch 28:19
- 11Ezk 11:20, Ezk 36:27, 1Co 11:2, Jhn 13:17, Ezk 44:5–6, Ezk 40:1–42, Mat 28:20, Ezk 12:3
- 12Ezk 40:2, Rev 21:27, Psa 93:5, Jol 3:17, Ezk 42:20, Zec 14:20–21
- 13Ezk 40:5, Ezk 41:8, 2Ch 4:1, Exo 27:1–8
- 15Exo 27:2, Lev 9:9, Psa 118:27, Isa 29:1–2, 1Ki 2:28, Isa 29:7
- 16Exo 27:1, Ezr 3:3, 2Ch 4:1, Exo 38:1–2
- 17Exo 20:26, Ezk 40:6, Exo 25:25, Neh 9:4, Ezk 8:16, 1Ki 18:32, Exo 30:3, 1Ki 6:8
- 18Exo 40:29, Lev 1:5–17, Ezk 45:18–19, Heb 9:21–22, Lev 8:18–21, Heb 12:24, Ezk 2:1, Heb 9:13
- 19Ezk 40:46, Ezk 44:15, Ezk 45:18–19, Num 16:40, Num 16:5, Heb 7:27, 1Ki 2:35, Lev 8:14–15
- 20Lev 8:15, Lev 16:19, Exo 29:12, Ezk 43:26, Lev 9:9, Ezk 43:22, Exo 29:36, Lev 4:30
- 21Exo 29:14, Lev 4:12, Lev 8:17, Heb 13:11–12
- 22Ezk 43:25–26, Ezk 43:20, Exo 29:15–18, Isa 53:10, Lev 8:18–21, 1Pe 1:19, Isa 53:6
- 23Exo 29:1
- 24Lev 2:13, Mrk 9:49–50, Col 4:6, Num 18:19, Mat 5:13, 2Ch 13:5
- 25Lev 8:33, Exo 29:35–37, Lev 8:35
- 26Exo 32:29, Lev 8:34, Exo 29:24
- 27Lev 9:1, Hos 8:13, Eph 1:6, Lev 17:5, Lev 3:1, Rom 12:1, Heb 13:15, 1Pe 2:5