Ezekieli 30
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, toa unabii na useme: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Ombolezeni ninyi na mseme, “Ole wa siku ile!”
3 Kwa kuwa siku ile imekaribia, siku ya Mwenyezi Mungu imekaribia, siku ya mawingu, siku ya maangamizi kwa mataifa.
4 Upanga utakuja dhidi ya Misri, nayo maumivu makuu yataijia Kushi. Mauaji yatakapoangukia Misri, utajiri wake utachukuliwa na misingi yake itabomolewa.
5 Kushi na Putu, Ludi na Arabia yote, Kubu na watu wa nchi ya agano watauawa kwa upanga pamoja na Misri.
6 “ ‘Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “ ‘Wale walioungana na Misri wataanguka na kiburi cha nguvu zake kitashindwa. Kutoka Migdoli hadi Aswani, watauawa ndani yake kwa upanga, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
7 Hizo nchi zitakua ukiwa miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yao itakuwa magofu miongoni mwa miji iliyo magofu.
8 Ndipo watajua kuwa mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapoiwasha Misri moto na wasaidizi wake wote watapondwa.
9 “ ‘Siku hiyo wajumbe watatoka kwangu kwa merikebu, ili kuwatia hofu Ethiopia, wakiwa katika hali yao ya kuridhika. Maumivu makali yatawapata siku ya maangamizi ya Misri, kwa kuwa hakika itakuja.
10 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Nitakomesha makundi ya Misri kwa mkono wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
11 Yeye na jeshi lake, taifa lililo katili kuliko mataifa yote, ataletwa ili kuangamiza nchi. Watafuta panga zao dhidi ya Misri na kuijaza nchi kwa waliouawa.
12 Nitakausha vijito vya Mto Naili, na kuiuza nchi kwa watu waovu; kwa mkono wa wageni, nitaifanya nchi ukiwa na kila kitu kilicho ndani yake. Mimi Mwenyezi Mungu nimenena haya.
13 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Nitaangamiza sanamu na kukomesha vinyago katika Memfisi. Hapatakuwa tena na mkuu katika nchi ya Misri, nami nitaeneza hofu katika nchi nzima.
14 Nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa na kuitia moto Soani, nami nitaipiga Thebesi kwa adhabu.
15 Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu, ngome ya Misri, nami nitakatilia mbali makundi ya Thebesi.
16 Nitaitia moto nchi ya Misri; Pelusiumu itagaagaa kwa maumivu makuu. Thebesi itachukuliwa na tufani, Memfisi itakuwa katika taabu daima.
17 Wanaume vijana wa Oni na wa Pi-Besethi wataanguka kwa upanga nayo hiyo miji itatekwa.
18 Huko Tapanesi mchana utatiwa giza nitakapovunja nira ya Misri; hapo kiburi cha nguvu zake kitakoma. Atafunikwa na mawingu na vijiji vyake vitatekwa.
19 Kwa hiyo nitaipiga Misri kwa adhabu, nao watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
20 Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
21 “Mwanadamu, nimevunja mkono wa Farao mfalme wa Misri. Haukufungwa ili upone au kuwekewa kipande cha ubao ili upate nguvu za kuweza kuchukua upanga.
22 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mimi ni kinyume na Farao mfalme wa Misri. Nitavunja mikono yake yote miwili, ule mkono ulio mzima pia na ule uliovunjika na kuufanya upanga uanguke toka mkononi mwake.
23 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatapanya katika nchi zote.
24 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa huzuni mbele yake kama mtu aliyetiwa jeraha la kumfisha.
25 Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao italegea. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye ataunyoosha dhidi ya Misri.
26 Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatapanya katika nchi nyingine. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.”
Перекрёстные ссылки
159
- 2Isa 13:6, Jol 1:5, Ezk 21:12, Jol 1:11, Isa 15:2, Jer 4:8, Isa 65:14, Rev 18:10
- 3Oba 1:15, Jol 2:1–2, Ezk 30:18, Ezk 7:12, Ezk 7:7, Isa 24:21–23, Zep 1:14, Ezk 34:12
- 4Ezk 29:19, Ezk 29:8, Ezk 29:12, Jer 50:35–37, Isa 16:7, Psa 48:6–7, Rev 18:9–10, Ezk 30:9–10
- 5Jer 25:20, Ezk 27:10, Jer 25:24, Isa 20:4, Jer 44:27, Jer 50:37, Jer 46:9, Isa 18:1
- 6Ezk 29:10, Isa 20:3–6, Nam 3:9, Isa 31:3, Job 9:13
- 7Ezk 29:12, Jer 25:18–26, Jer 46:1–28, Ezk 32:18–32
- 8Ezk 29:6, Amo 1:12, Amo 1:10, Ezk 22:31, Ezk 29:16, Amo 1:14, Ezk 30:16, Amo 1:7
- 9Isa 18:1–2, Ezk 32:9–10, Isa 23:5, Ezk 26:16, Ezk 27:35, Jer 49:21, Isa 20:5, Ezk 33:33
- 10Ezk 29:19, Ezk 29:4–5, Ezk 32:11–16, Ezk 30:24–25
- 11Ezk 28:7, Hab 1:6–9, Isa 14:4–6, Ezk 31:12, Ezk 32:12, Isa 34:3–7, Zep 1:17–18, Jer 51:20–23
- 12Ezk 29:3, Isa 19:4–10, Jer 50:38, Jdg 2:14, 1Co 10:26, Rev 16:12, Jer 51:36, Ezk 31:12
- 13Zec 10:11, Jer 2:16, Jer 46:14, Hos 9:6, Ezk 29:14–15, Zec 13:2, Jer 43:12–44:1, Zep 2:11
- 14Ezk 29:14, Jer 46:25, Psa 78:12, Psa 78:43, Isa 19:11, Nam 3:8, Num 13:22, Isa 11:11
- 15Psa 11:6, Nam 1:6, Rev 16:1
- 16Ezk 30:8–9, Ezk 28:18
- 17Gen 41:45
- 18Ezk 30:3, Ezk 29:15, Jer 2:16, Isa 10:27, Isa 13:10, Ezk 32:18–32, Ezk 31:18, Isa 5:30
- 19Rev 17:1, Ezk 30:14, Num 33:4, Ezk 5:8, Rom 2:5, Ezk 5:15, Ezk 25:11, Psa 9:16
- 20Ezk 26:1, Ezk 29:17, Ezk 29:1, Ezk 31:1, Ezk 1:2
- 21Jer 46:11, Jer 30:13, Psa 37:17, Jer 48:25, Psa 10:15, Ezk 30:24, Nam 3:16, Jer 51:8–9
- 22Psa 37:17, Ezk 29:3, 2Ki 24:7, Jer 37:7, Jer 46:1–12, Jer 46:21–25, Ezk 34:16
- 23Ezk 30:17–18, Ezk 30:26, Ezk 29:12–13
- 24Zep 2:12, Ezk 30:25, Isa 45:1, Isa 45:5, Neh 6:9, Psa 18:39, Isa 10:15, Psa 17:13
- 25Ezk 29:16, Ezk 30:26, Ezk 38:16, Ezk 39:21–22, Ezk 30:19, Ezk 38:23, Psa 9:16, Ezk 29:21
- 26Dan 11:42, Ezk 29:12, Ezk 30:23, Ezk 6:13, Ezk 30:17–18