Ezekieli 28
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, mwambie mfalme wa Tiro, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Kwa sababu moyo wako umejivuna na umesema, “Mimi ni mungu; nami ninaketi kwenye kiti cha enzi cha mungu katika moyo wa bahari.” Lakini wewe ni mwanadamu, wala si mungu, ingawa unafikiri kuwa una hekima kama mungu.
3 Je, wewe una hekima kuliko Danieli? Je, hakuna siri iliyofichika kwako?
4 Kwa hekima yako na ufahamu wako, umejipatia utajiri, nawe umejikusanyia dhahabu na fedha katika hazina zako.
5 Kwa werevu wako mwingi katika biashara, umeongeza utajiri wako na kwa sababu ya utajiri wako moyo wako umekuwa na kiburi.
6 “ ‘Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Kwa sababu unafikiri una hekima, mwenye hekima kama mungu,
7 mimi nitawaleta wageni dhidi yako, taifa katili kuliko yote; watafuta panga zao dhidi ya uzuri wa hekima yako, na kuchafua fahari yako inayong’aa.
8 Watakushusha chini shimoni, nawe utakufa kifo cha kikatili katika moyo wa bahari.
9 Je, wakati huo utasema, “Mimi ni mungu,” mbele ya wale wanaokuua? Utakuwa mwanadamu tu, wala si mungu, mikononi mwa hao wanaokuua.
10 Utakufa kifo cha wasiotahiriwa kwa mkono wa wageni. Kwa kuwa mimi nimenena, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
11 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
12 “Mwanadamu, mfanyie maombolezo mfalme wa Tiro, nawe umwambie: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Ulikuwa kipeo cha ukamilifu, ukiwa umejaa hekima na mkamilifu katika uzuri.
13 Ulikuwa ndani ya Edeni, bustani ya Mungu; kila kito cha thamani kilikupamba: akiki nyekundu, yakuti manjano na zumaridi, krisolitho, shohamu na yaspi, yakuti samawi, almasi na zabarajadi. Kuwekwa kwa hayo mapambo na kushikizwa kwake kulifanywa kwa dhahabu; siku ile ulipoumbwa yaliandaliwa tayari.
14 Ulipakwa mafuta kuwa kerubi mlinzi, kwa kuwa hivyo ndivyo nilivyokuweka wakfu. Ulikuwa kwenye mlima mtakatifu wa Mungu; ulitembea katikati ya vito vya moto.
15 Ulikuwa mnyofu katika njia zako tangu siku ile ya kuumbwa kwako, hadi uovu ulipoonekana ndani yako.
16 Kutokana na biashara yako iliyoenea, ulijazwa na dhuluma, nawe ukatenda dhambi. Hivyo nilikuondoa kwa aibu kutoka mlima wa Mungu, nami nikakufukuza, ee kerubi mlinzi, kutoka katikati ya vito vya moto.
17 Moyo wako ukawa na kiburi kwa ajili ya uzuri wako, nawe ukaiharibu hekima yako kwa sababu ya fahari yako. Kwa hiyo nikakutupa chini; nimekufanya kioja mbele ya wafalme.
18 Kwa dhambi zako nyingi na biashara yako ya dhuluma, umenajisi mahali pako patakatifu. Kwa hiyo nilifanya moto utoke ndani yako, nao ukakuteketeza, nami nikakufanya majivu juu ya nchi, machoni pa wote waliokuwa wakitazama.
19 Mataifa yote yaliyokujua yanakustaajabia; umefikia mwisho wa kutisha na hutakuwepo tena milele.’ ”
20 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
21 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Sidoni, ukatabiri dhidi yake,
22 nawe useme: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Mimi ni kinyume chako, ee Sidoni, nami nitapata utukufu ndani yako. Nao watajua kwamba Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapotekeleza hukumu zangu na kuonesha utakatifu wangu ndani yake.
23 Nitapeleka tauni ndani yake na kufanya damu itiririke katika barabara zake. Waliochinjwa wataanguka ndani yake, kwa upanga dhidi yake kila upande. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
24 “ ‘Nyumba ya Israeli hawatakuwa tena na majirani wenye nia ya kuwadhuru, wanaoumiza kama michongoma na miiba mikali. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mungu Mwenyezi.
25 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitakapoikusanya nyumba ya Israeli kutoka mataifa ambako wametawanyika, nitajionesha kuwa mtakatifu miongoni mwao machoni pa mataifa. Ndipo watakapoishi katika nchi yao wenyewe, niliyompa mtumishi wangu Yakobo.
26 Wataishi humo kwa salama na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu, wataishi kwa salama nitakapowaadhibu majirani zao wote ambao waliwafanyia uovu. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wao.’ ”
Перекрёстные ссылки
179
- 2Ezk 28:9, 2Th 2:4, Isa 14:13–14, Psa 9:20, Isa 31:3, Pro 16:18, Act 12:22–23, Isa 2:12
- 3Dan 1:20, Dan 2:22, Dan 2:27–28, 1Ki 10:3, Dan 5:11–12, Job 15:8, 1Ki 4:29–32, Zec 9:2–3
- 4Pro 18:11, Pro 23:4–5, Deu 8:17–18, Zec 9:2–4, Hab 1:16, Ezk 29:3, Ecc 9:11
- 5Psa 52:7, Psa 62:10, Ezk 28:2, Hos 13:6, Hos 12:7–8, Pro 11:28, Jas 4:13–14, Deu 6:11–12
- 6Ezk 28:2, Exo 9:17, 1Co 10:22, Job 9:4, Jas 1:11, 2Th 2:4, Job 40:9–12
- 7Ezk 31:12, Ezk 30:11, Ezk 32:12, Hab 1:6–8, Amo 3:6, Ezk 26:7–14, Deu 28:49–50, Dan 7:7
- 8Ezk 27:34, Ezk 27:26–27, Psa 28:1, Job 33:18, Pro 28:17, Pro 1:12, Ezk 32:18–30, Job 33:28
- 9Ezk 28:2, Psa 82:7, Isa 31:3, Dan 5:23–30, Dan 4:31–32, Act 12:22–23
- 10Ezk 31:18, Ezk 32:19, 1Sa 17:26, 1Sa 17:36, Ezk 32:21, Php 3:3, Jer 6:10, Ezk 32:24–30
- 12Ezk 19:1, Ezk 26:17, Col 2:3, 2Co 1:22, Col 1:9, Jas 3:13–18, Pro 21:30, Act 6:3
- 13Ezk 28:15, Gen 2:8, Ezk 27:16, Isa 54:11–12, Isa 51:3, Gen 3:23–24, Isa 23:16, Isa 14:11
- 14Exo 30:26, Isa 14:12–15, Ezk 28:13, Ezk 20:40, Exo 40:9, Exo 9:16, Exo 25:17–20, Rev 18:16
- 152Pe 2:4, Ezk 28:17–18, Rom 7:9, Gen 1:26–27, Ezk 28:12, Ezk 28:3–6, Ezk 27:3–4, Lam 5:16
- 161Ti 6:9–10, Hab 2:8, Hab 2:17, Gen 3:24, Jhn 2:16, Mic 2:2, Ezk 8:17, Ezk 27:12–36
- 17Ezk 28:5, Pro 16:18, Ezk 31:10, Jas 4:6, Luk 14:11, Ezk 28:2, Ezk 32:10, Pro 11:2
- 18Mal 4:3, Rev 18:8, Amo 1:9–10, Ezk 28:16, Ezk 28:2, 2Pe 2:6, Amo 1:14, Ezk 5:4
- 19Ezk 26:21, Rev 18:15–19, Rev 18:21, Psa 76:12, Isa 14:16–19, Jer 51:63–64, Ezk 26:14, Ezk 27:35–36
- 21Ezk 6:2, Gen 10:15, Ezk 27:8, Ezk 25:2, Jer 25:22, Jer 47:4, Jol 3:4–8, Ezk 32:30
- 22Ezk 39:13, Exo 14:4, Ezk 30:19, Ezk 20:41, Exo 14:17, Jer 50:31, Lev 10:3, Ezk 5:8
- 23Ezk 38:22, Ezk 25:11, Jer 15:2, Ezk 25:7, Ezk 5:12, Ezk 25:17, Ezk 26:6
- 24Jos 23:13, Num 33:55, 2Co 12:7, Ezk 2:6, Isa 55:13, Jdg 2:3, Mic 7:4, Rev 21:4
- 25Jer 32:37, Ezk 20:41, Ezk 11:17, Psa 106:47, Ezk 37:25, Jer 23:8, Ezk 36:28, Ezk 28:22
- 26Ezk 28:24, Ezk 28:22, Amo 9:13–14, Ezk 38:8, Ezk 34:25–28, Jer 32:15, Pro 14:26, Deu 12:10