Ezekieli 29
1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, ewe mnyama mkubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
5 Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
6 Ndipo wale wote wanaoishi Misri watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu. “ ‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
8 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu. “ ‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliuumba,”
10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpaka wa Kushi.
11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwatapanya katika nchi nyingine.
13 “ ‘Lakini hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
14 Nitawarejesha hao Wamisri kutoka kutekwa kwao na kuwaweka Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Mwenyezi Mungu likanijia, kusema:
18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upara na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
19 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali ya Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.”
Перекрёстные ссылки
136
- 1Ezk 29:17, Ezk 26:1, Ezk 20:1, Ezk 1:2, Ezk 8:1, Ezk 40:1
- 2Ezk 6:2, Jer 44:30, Jer 46:2–16, Jol 3:19, Zec 14:18–19, Isa 18:1–19:17, Jer 25:18–19, Ezk 28:21–22
- 3Isa 27:1, Ezk 32:2, Jer 44:30, Ezk 29:9–10, Deu 8:17, Rev 12:3–4, Isa 10:13–14, Dan 4:30–31
- 4Ezk 38:4, 2Ki 19:28, Job 41:1–2, Hab 1:14–15, Amo 4:2, Isa 37:29
- 5Jer 8:2, Jer 7:33, Ezk 32:4–6, Jer 34:20, Jer 25:33, Psa 110:5–6, Psa 74:14, Ezk 39:11–20
- 6Isa 36:6, 2Ki 18:21, Lam 4:17, Jer 2:36, Exo 14:18, Isa 30:2–7, Isa 31:1–3, Isa 20:5–6
- 7Isa 36:6, Ezk 17:15–17, Jer 17:5–6, Pro 25:19, Psa 146:3–4, Jer 37:5–11, Psa 118:8–9
- 8Ezk 14:17, Ezk 29:19–20, Jer 46:13–26, Ezk 30:4, Exo 12:12, Gen 6:7, Ezk 30:10, Ezk 25:13
- 9Ezk 29:3, Ezk 29:10–12, Pro 18:12, Pro 16:18, Ezk 30:13–19, Ezk 30:7–8, Jer 43:10–13, Pro 29:23
- 10Ezk 30:12, Ezk 30:6–9, Jer 46:14, Exo 14:2, Hab 3:8, Jer 44:1, Ezk 29:11
- 11Ezk 32:13, Jer 43:11–12, Ezk 31:12, Isa 23:17, Jer 29:10, Jer 25:11–12, Ezk 36:28, Dan 9:2
- 12Ezk 30:23, Ezk 30:7, Jer 46:19, Ezk 30:26, Jer 25:15–19, Jer 27:6–11
- 13Isa 19:22, Jer 46:26
- 14Ezk 30:14, Isa 11:11, Jer 44:1, 1Ch 1:12, Gen 10:14
- 15Ezk 30:13, Zec 10:11, Ezk 17:14, Ezk 31:2, Ezk 32:2, Nam 3:8–9, Ezk 17:6, Dan 11:42–43
- 16Hos 8:13, Isa 20:5, Ezk 29:6–7, Jer 2:36–37, Ezk 21:23, Isa 30:1–6, Isa 64:9, Psa 25:7
- 17Ezk 29:1, Ezk 24:1, Ezk 1:2
- 18Jer 27:6, Jer 25:9, Ezk 26:7–12, Jer 48:37
- 19Ezk 30:24–25, Jer 43:10–13, Ezk 30:10–12, Ezk 32:11, Ezk 30:4, Ezk 29:8–10
- 20Isa 10:6–7, Jer 25:9, Isa 45:1–3, 2Ki 10:30
- 211Sa 2:10, Psa 132:17, Luk 21:15, Amo 3:7–8, Ezk 33:22, Ezk 24:27, Psa 92:10, Luk 1:69