Ezekieli 24
1 Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo.
3 Nenea nyumba hii ya uasi kwa fumbo, uwaambie: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Teleka sufuria jikoni; iteleke na umimine maji ndani yake,
4 Weka vipande vya nyama ndani yake, vipande vyote vizuri, vya paja na vya bega. Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;
5 chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo. Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa; chochea hadi ichemke na uitokose hiyo mifupa ndani yake.
6 “ ‘Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Ole wa mji unaomwaga damu, ole wa sufuria ambayo sasa ina ukoko ndani yake, ambayo ukoko wake hautoki. Kipakue kipande baada ya kipande, bila kuvipigia kura.
7 “ ‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake: Huyo mwanamke aliimwaga juu ya mwamba ulio wazi; hakuimwaga kwenye ardhi, ambako vumbi lingeifunika.
8 Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi, nimemwaga damu yake juu ya mwamba ulio wazi, ili isifunikwe.
9 “ ‘Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “ ‘Ole wa mji unaomwaga damu! Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.
10 Kwa hiyo lundika kuni na uwashe moto. Pika hiyo nyama vizuri, changanya vikolezo ndani yake, na uiache mifupa iungue kwenye moto.
11 Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa hadi iwe na moto sana na shaba yake ing’ae, ili uchafu wake upate kuyeyuka na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.
12 Imezuia juhudi zote, ukoko wake mwingi haujaondoka, hata ikiwa ni kwa moto.
13 “ ‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutokana na huo uchafu wako, hutatakasika tena hadi ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.
14 “ ‘Mimi Mwenyezi Mungu nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu. Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
15 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
16 “Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote.
17 Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya waombolezaji.”
18 Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Kesho yake asubuhi nilifanya kama nilivyoamriwa.
19 Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”
20 Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Mwenyezi Mungu lilinijia kusema:
21 ‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu wa kiume na wa kike mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
22 Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji.
23 Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake.
24 Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mungu Mwenyezi.’
25 “Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao wa kiume na wa kike vilevile,
26 siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari.
27 Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.”
Перекрёстные ссылки
171
- 1Ezk 8:1, Ezk 20:1, Ezk 40:1, Ezk 33:21, Ezk 32:17, Ezk 29:1, Ezk 26:1, Ezk 29:17
- 22Ki 25:1, Jer 39:1, Jer 52:4, Hab 2:2–3, Isa 30:8–9, Isa 8:1
- 3Ezk 11:3, Ezk 20:49, Ezk 17:2, Isa 1:2, Ezk 2:6, Ezk 2:3, Isa 30:1, Ezk 2:8
- 4Mic 3:2–3, Mat 7:2, Ezk 22:18–22
- 5Jer 52:10, Jer 52:24–27, Jer 39:6, Ezk 20:47, Ezk 34:16–17, Rev 19:20, Ezk 24:9–10, Ezk 34:20
- 6Ezk 22:2, Nam 3:1, Mic 7:2, Nam 3:10, Oba 1:11, 2Ki 24:4, Ezk 22:27, Jos 10:22
- 7Lev 17:13, Deu 12:16, Isa 3:9, Jer 6:15, Jer 2:34, Isa 26:21, Deu 12:24, 1Ki 21:19
- 8Deu 32:21–22, Rev 18:5–10, Ezk 5:13, Rev 17:1–6, 2Ch 36:16–17, Ezk 22:30–31, Ezk 16:37–38, Rev 18:16
- 9Ezk 24:6, Hab 2:12, Nam 3:1, Jud 1:7, Isa 31:9, Rev 14:20, Rev 16:6, 2Pe 3:7–12
- 10Lam 1:10, Jer 17:3, Lam 2:16, Jer 20:5
- 11Jer 21:10, Isa 1:25, Mal 4:1, Jer 32:29, Isa 27:9, Zec 13:1–2, Jer 37:10, Ezk 23:26–27
- 12Jer 5:3, Jer 9:5, Jer 2:13, Dan 9:13–14, Hab 2:13, Jer 51:58, Jer 10:14–15, Hab 2:18–19
- 13Ezk 22:24, Ezk 5:13, Zep 3:2, Ezk 16:42, Ezk 8:18, 2Co 7:1, Rev 22:11, Ezk 24:11
- 14Mat 16:27, Isa 3:11, Ezk 18:30, Rom 2:5–6, Isa 55:11, Ezk 7:4, Ezk 5:11, Jer 13:14
- 16Jer 22:10, Jer 13:17, Sng 7:10, 1Th 4:13, Ezk 24:18, Job 36:18, Lev 10:2–3, Jer 16:5
- 17Hos 9:4, 2Sa 15:30, Lev 21:10, Jer 16:4–7, Lev 10:6, Ezk 24:22–23, Psa 37:7, Hab 2:20
- 181Co 7:29–30
- 19Ezk 12:9, Ezk 37:18, Ezk 20:49, Ezk 21:7, Ezk 17:12, Mal 3:7–8, Mal 3:13
- 21Ezk 23:47, Jer 7:14, Psa 27:4, Ezk 23:25, Jer 16:3–4, Jer 6:11, Psa 84:1, Ezk 24:16
- 22Job 27:15, Psa 78:64, Amo 6:9–10, Ezk 24:16–17, Jer 47:3, Jer 16:4–7
- 23Lev 26:39, Ezk 33:10, Ezk 4:17, Isa 59:11, Psa 78:64, Job 27:15
- 24Ezk 4:3, Luk 11:29–30, Ezk 6:7, Isa 20:3, Ezk 12:11, Luk 21:13, Hos 3:1–4, Ezk 25:5
- 25Ezk 24:21, Psa 50:2, Psa 48:2, Jer 11:22, Deu 28:32, Jer 52:10, Jer 7:4, Psa 122:1–9
- 26Job 1:15–19, Ezk 33:21–22, 1Sa 4:12–18
- 27Ezk 33:22, Ezk 29:21, Exo 6:11–12, Luk 21:15, Eph 6:19, Psa 51:15, Ezk 3:26–27