Ezekieli 19
1 “Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli
2 na useme: “ ‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike miongoni mwa simba! Alilala katikati ya wana simba na kulisha watoto wake.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, naye akawa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
4 Mataifa wakasikia habari zake, naye akanaswa katika shimo lao. Wakamwongoza kwa ndoana hadi nchi ya Misri.
5 “ ‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki, nayo matarajio yake yametoweka, akamchukua mwanawe mwingine na kumfanya simba mwenye nguvu.
6 Alizungukazunguka miongoni mwa simba, kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu. Akajifunza kurarua mawindo naye akala watu.
7 Akabomoa ngome zao na kuiharibu miji yao. Nchi na wote waliokuwa ndani yake wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.
8 Kisha mataifa wakaja dhidi yake kutoka sehemu zilizomzunguka. Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake, naye akanaswa katika shimo lao.
9 Wakamvutia kwenye tundu kwa kutumia ndoana, wakamleta kwa mfalme wa Babeli. Wakamfunga gerezani, hivyo kunguruma kwake hakukusikika tena katika milima ya Israeli.
10 “ ‘Mama yako alikuwa kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu uliopandwa kando ya maji, ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi kwa sababu ya wingi wa maji.
11 Matawi yake yalikuwa na nguvu, yaliyofaa kuwa fimbo ya mtawala. Ulikuwa mrefu kupita miti mingine katikati ya matawi manene; ulionekana kwa urahisi kwa ajili ya urefu wake na wingi wa matawi yake.
12 Lakini uling’olewa kwa hasira kali na kutupwa chini. Upepo wa mashariki uliufanya usinyae, matunda yake yakapukutika, matawi yake yenye nguvu yakanyauka na moto ukayateketeza.
13 Sasa umepandwa jangwani katika nchi kame na ya kiu.
14 Moto ulienea kuanzia mojawapo ya matawi yake makubwa na kuteketeza matunda yake. Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake linalofaa kuwa fimbo ya mtawala.’ Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”
Перекрёстные ссылки
95
- 1Ezk 26:17, Ezk 27:2, 2Ki 25:5–7, 2Ki 23:29–30, 2Ki 24:12, Ezk 2:10, 2Ki 23:34, 2Ki 24:6
- 2Isa 11:6–9, Isa 5:29, Psa 58:6, Zec 11:3, Job 4:11, Zep 3:1–4, Nam 2:11–12
- 32Ch 36:1–2, Ezk 22:25, Ezk 19:6, 2Ki 23:31–32
- 42Ch 36:4, 2Ki 23:33–34, Jer 22:11–12, 2Ch 36:6, 2Ki 23:31, Jer 22:18
- 52Ki 23:34–37, Ezk 19:3
- 6Jer 22:13–17, Jer 36:1–32, 2Ch 36:5, 2Ki 24:1–7, 2Ki 24:9, 2Ch 36:9, Jer 26:1–24
- 7Ezk 30:12, Mic 1:2, Pro 28:15–16, Pro 28:3, Amo 6:8, Pro 19:12, Ezk 12:19, Ezk 22:25
- 8Lam 4:20, Ezk 12:13, Ezk 19:4, 2Ki 24:11, 2Ki 24:1–6, Ezk 17:20
- 92Ch 36:6, Ezk 6:2, Jer 22:18–19, Ezk 36:1, Jer 36:30–31, 2Ki 24:15, Ezk 19:7
- 10Psa 80:8–11, Deu 8:7, Mat 21:33–41, Num 24:6–7, Psa 89:25–29, Ezk 15:2–8, Deu 8:9, Ezk 19:2
- 11Ezk 31:3, Psa 80:15, Dan 4:11, Ezr 4:20, Ezk 19:12, Psa 2:8–9, Num 24:17, Psa 110:2
- 12Hos 13:15, Ezk 17:10, Isa 27:11, Ezk 15:4, Ezk 19:11, Jer 31:28, Jer 4:11–12, 2Ki 25:6–7
- 13Hos 2:3, Ezk 19:10, Jer 52:27–31, Psa 63:1, Psa 68:6, 2Ki 24:12–16, Ezk 20:35, Deu 28:47–48
- 142Ki 24:20, Ezk 19:1, Isa 9:18–19, Ezk 19:11, Psa 80:15–16, Rom 9:2–4, Lam 4:20, Jer 52:3