Ezekieli 12
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni, na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Huenda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya uasi.
4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale wanaoenda uhamishoni.
5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
8 Asubuhi neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya uasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
10 “Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Unabii huu unamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na watu wote wa nyumba ya Israeli walio huko.’
11 Waambie, ‘Mimi ni ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Wataenda uhamishoni kama mateka.
12 “Mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani wakati wa giza la jioni na kuondoka, na tundu litatobolewa ukutani ili apite. Atafunika uso wake ili asiweze kuiona nchi.
13 Nitamtandazia wavu wangu, naye atanaswa kwenye mtego wangu; nitamleta hadi Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote: watumishi wake na majeshi yake yote; nami nitawafuatilia kwa upanga.
15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa, na kuwatapanya katika nchi zote.
16 Lakini nitawaokoa wachache wao, wasiuawe kwa upanga, njaa na tauni, ili katika mataifa watakakoenda waweze kukiri matendo yao yote ya kuchukiza. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.”
17 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
18 “Mwanadamu, tetemeka unapokula chakula chako, tetemeka kwa hofu unapokunywa maji yako.
19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi kuhusu wakaaji wa Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyang’anywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.’ ”
21 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
22 “Mwanadamu, ni ipi hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia’?
23 Waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia ambapo kila ono litatimizwa.
24 Kwa maana hapatakuwa tena na maono ya uongo wala ubashiri wa kujipendekeza miongoni mwa watu wa Israeli.
25 Lakini Mimi Mwenyezi Mungu nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa kuwa katika siku zako, ewe nyumba ya uasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
26 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
Перекрёстные ссылки
156
- 2Jer 5:21, Mrk 4:12, Jhn 9:39–41, Psa 78:40, Isa 1:23, Jer 9:1–6, Eph 4:18, Mat 13:13–14
- 3Jer 36:3, 2Ti 2:25, Jer 26:3, Luk 20:13, Jer 36:7, Jer 27:2, Luk 13:34, Psa 81:13
- 4Jer 39:4, 2Ki 25:4, Ezk 12:12, Jer 52:7
- 5Jer 39:2–4, 2Ki 25:4
- 6Ezk 4:3, Ezk 24:24, Isa 8:18, 1Sa 28:8, Ezk 12:11–12, 2Sa 15:30, Job 24:17, Isa 20:2–4
- 7Ezk 24:18, Ezk 37:10, Ezk 37:7, Jhn 2:5–8, Jer 32:8–12, Mrk 14:16, Ezk 12:3, Jhn 15:14
- 9Ezk 17:12, Ezk 24:19, Ezk 20:49, Ezk 12:1–3, Ezk 2:5–8
- 10Isa 13:1, 2Ki 9:25, Jer 21:7, Mal 1:1, Jer 24:8, Ezk 7:27, Ezk 21:25–27, Ezk 17:13–21
- 11Jer 15:2, Jer 52:15, Jer 52:28–30, Ezk 12:6
- 122Ki 25:4, Jer 39:4, Ezk 12:6, Jer 52:7, Jer 42:7
- 13Jer 39:7, Ezk 17:20, Hos 7:12, Isa 24:17–18, Ezk 17:16, Ezk 32:3, 2Ki 25:5–7, Psa 11:6
- 14Ezk 5:2, Ezk 17:21, 2Ki 25:4–5, Jer 42:16, Ezk 14:17, Lev 26:33, Ezk 14:21, Jer 42:22
- 15Ezk 6:7, Ezk 6:14, Ezk 12:16, Ezk 12:20, Ezk 24:27, Ezk 5:13, Ezk 26:6, Ezk 11:10
- 16Ezk 6:8–10, Jer 22:8–9, Ezk 14:22–23, Isa 1:9, Jer 4:27, Jer 30:11, Jer 3:24–25, Mat 7:14
- 18Lam 5:9, Deu 28:65, Lev 26:36, Job 3:24, Psa 60:2–3, Deu 28:48, Ezk 4:16–17, Psa 102:4–9
- 19Zec 7:14, Mic 7:13, Ezk 6:14, Ezk 6:6–7, Jer 10:22, 1Co 10:28, Ezk 7:23, Jer 6:7
- 20Isa 7:23–24, Jer 4:7, Jer 25:9, Isa 3:26, Jer 24:8–10, Isa 64:10–11, Jer 16:9, Jer 12:10–12
- 22Ezk 18:2–3, Ezk 11:3, Ezk 12:27, Jer 23:33–40, Amo 6:3, 2Pe 3:3–4, Isa 5:19, Jer 5:12–13
- 23Jol 2:1, Zep 1:14, Ezk 18:3, Mat 24:34, Ezk 7:5–7, Jas 5:8–9, Mal 4:1, Isa 28:22
- 24Jer 14:13–16, Zec 13:2–4, Ezk 13:23, Lam 2:14, Rom 16:18, 1Th 2:5, Pro 26:28, 1Ki 22:17
- 25Isa 55:11, Hab 1:5, Isa 14:24, Ezk 12:28, Mat 24:35, Ezk 12:1–2, Luk 21:33, Ezk 6:10
- 27Dan 10:14, 2Pe 3:4, Ezk 12:22, Isa 28:14–15
- 28Ezk 12:23–25, Mrk 13:32–37, Mat 24:48–51, 1Th 5:2–3