Ezekieli 16
1 Neno la Mwenyezi Mungu likanijia kusema:
2 “Mwanadamu, kabili Yerusalemu kuhusu matendo yake ya kuchukiza,
3 useme, ‘Hili ndilo Bwana Mungu Mwenyezi, analomwambia Yerusalemu: Asili na kuzaliwa kwako kulikuwa ni katika nchi ya Wakanaani; baba yako alikuwa Mwamori, naye mama yako alikuwa Mhiti.
4 Siku uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, wala hukuogeshwa kwa maji ili kukufanya safi, wala hukusuguliwa kwa chumvi wala kufunikwa kwa nguo.
5 Hakuna yeyote aliyekuonea huruma au kukusikitikia kiasi cha kukutendea mojawapo ya mambo haya. Badala yake, ulipozaliwa ulitupwa nje penye uwanja, kwa kuwa katika siku uliyozaliwa ulidharauliwa.
6 “ ‘Nami nikapita karibu nawe nikakuona ukigaagaa kwenye damu yako, nawe ulipokuwa umelala hapo penye hiyo damu nikakuambia, “Ishi!”
7 Nilikufanya uote kama mmea wa shambani. Ukakua na kuongezeka sana, ukawa kito cha thamani kuliko vyote. Matiti yako yakatokeza na nywele zako zikaota, wewe uliyekuwa uchi na bila kitu chochote.
8 “ ‘Baadaye nikapita karibu nawe, nilipokutazama na kukuona kuwa umefikia umri wa kupendwa, niliutandaza upindo wa vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikakuapia na kuingia kwenye agano na wewe, asema Bwana Mungu Mwenyezi, nawe ukawa wangu.
9 “ ‘Nilikuogesha kwa maji, nikakuosha ile damu na kukupaka mafuta.
10 Nikakuvika vazi lililotariziwa na kukuvalisha viatu vya ngozi. Nikakuvika nguo za kitani safi na kukufunika kwa mavazi ya thamani kubwa.
11 Nikakupamba kwa vito: nikakuvika bangili mikononi mwako na mkufu shingoni mwako,
12 nikaweka hazama puani mwako, vipuli masikioni mwako na taji nzuri sana kichwani mwako.
13 Kwa hiyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; nguo zako zilikuwa za kitani safi, na hariri, na nguo iliyokuwa imetariziwa. Chakula chako kilikuwa unga laini, asali na mafuta ya zeituni. Ukawa mzuri sana, ukainuka kuwa malkia.
14 Umaarufu wako ulifahamika miongoni mwa mataifa kwa ajili ya uzuri wako, kwani ulikuwa mkamilifu kwa ajili ya utukufu wangu niliokuwa nimeuweka juu yako, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
15 “ ‘Lakini ulitumainia uzuri wako na kutumia umaarufu wako kuwa kahaba. Ulifanya uasherati na kila mtu aliyepita, nao uzuri wako ukawa wake.
16 Ulichukua baadhi ya mavazi yako, ukayatumia kupamba mahali pako pa juu pa kuabudia, ambapo uliendeleza ukahaba wako. Mambo kama hayo hayastahili kutendeka wala kamwe kufanyika.
17 Pia ulichukua vito vizuri nilivyokupa, vito vilivyotengenezwa kwa dhahabu yangu na fedha yangu, ukajitengenezea navyo sanamu za kiume na ukafanya ukahaba nazo.
18 Ukayachukua mavazi yako yaliyotariziwa, na kuyavalisha hizo sanamu, ukatoa mbele ya hizo sanamu mafuta yangu na uvumba wangu.
19 Pia chakula changu nilichokupa ili ule: unga laini, mafuta ya zeituni na asali, ulivitoa mbele yao kuwa uvumba wa harufu nzuri. Hayo ndiyo yaliyotokea, asema Bwana Mungu Mwenyezi.
20 “ ‘Nawe uliwachukua wanao wa kiume na wa kike ulionizalia na kuwatoa kafara kuwa chakula kwa sanamu. Je, ukahaba wako haukukutosha?
21 Uliwachinja watoto wangu na kuwatoa kafara kwa sanamu.
22 Katika matendo yako yote ya machukizo pamoja na ukahaba wako, hukukumbuka siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi kabisa bila kitu chochote, ulipokuwa ukigaagaa kwenye damu yako.
23 “ ‘Ole! Ole wako! Asema Bwana Mungu Mwenyezi. Pamoja na maovu yako yote mengine,
24 Ulijijengea jukwaa na kujifanyia mahali pa fahari pa ibada za sanamu kwenye kila uwanja wa mikutano.
25 Katika kila mwanzo wa barabara ulijenga mahali pa fahari pa ibada za sanamu, na kuuaibisha uzuri wako, ukizidi kuutoa mwili wako kwa uzinzi kwa kila apitaye.
26 Ulifanya ukahaba wako na Wamisri, majirani zako waliojaa tamaa, ukaichochea hasira yangu kwa kuongezeka kwa uzinzi wako.
27 Hivyo niliunyoosha mkono wangu dhidi yako na kuipunguza nchi yako; nikakutia kwenye ulafi wa adui zako, binti za Wafilisti, walioshtushwa na tabia yako ya uasherati.
28 Ulifanya ukahaba na Waashuru pia, kwa kuwa hukuridhika, hata baada ya hayo, ukawa bado hukutosheleka.
29 Ndipo uliuzidisha uzinzi wako kwa kujumuisha Ukaldayo, nchi ya wafanyabiashara; lakini hata katika hili hukutosheka.
30 “ ‘Tazama jinsi ulivyo na dhamiri dhaifu, asema Bwana Mungu Mwenyezi, unapofanya mambo haya yote, unatenda kama kahaba asiye aibu!
31 Ulipojenga jukwaa lako katika mwanzo wa kila barabara, na kutengeneza mahali pako pa fahari pa ibada za sanamu katika kila kiwanja cha wazi, hukuwa kama kahaba, kwa sababu ulidharau malipo.
32 “ ‘Wewe mke mzinzi! Unapenda wageni, kuliko mume wako mwenyewe.
33 Kila kahaba hupokea malipo, lakini wewe hutoa zawadi kwa wapenzi wako wote, ukiwahonga ili waje kwako kutoka kila mahali kwa ajili ya ukahaba wako.
34 Kwa hiyo wewe ulikuwa tofauti na wanawake wengine kwenye ukahaba wako. Hakuna aliyekutongoza ili kuzini naye, bali wewe ulikuwa tofauti kabisa, kwani ulilipa wakati hakuna malipo uliyolipwa wewe.
35 “ ‘Kwa hiyo, wewe kahaba, sikia neno la Mwenyezi Mungu!
36 Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Kwa kuwa umemwaga tamaa zako na kuonesha uchi wako katika uzinzi wako kwa wapenzi wako na kwa sababu ya sanamu zako zote za machukizo na kwa sababu uliwapa damu ya watoto wako,
37 kwa hiyo nitawakusanya wapenzi wako wote, wale uliojifurahisha nao: wale uliowapenda kadhalika na wale uliowachukia. Nitawakusanya wote dhidi yako kutoka pande zote, na nitakuvua nguo mbele yao, nao wataona uchi wako wote.
38 Nitakuhukumia adhabu wanayopewa wanawake wafanyao uasherati na hao wanaomwaga damu; nitaleta juu yako kisasi cha damu cha ghadhabu yangu na hasira yangu yenye wivu.
39 Kisha nitakutia mikononi mwa wapenzi wako, nao watabomoa majukwaa yako na kuharibu mahali pako pa fahari pa ibada za sanamu. Watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vya thamani na kukuacha uchi na bila kitu.
40 Wataleta kundi la watu dhidi yako, watakaokupiga kwa mawe na kukukatakata vipande vipande kwa panga zao.
41 Watachoma nyumba zako na kutekeleza adhabu juu yako machoni pa wanawake wengi. Nitakomesha ukahaba wako, nawe hutawalipa tena wapenzi wako.
42 Ndipo ghadhabu yangu dhidi yako itapungua, na hasira yangu yenye wivu itakuondokea. Nitatulia, wala sitakasirika tena.
43 “ ‘Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako, lakini ulinighadhibisha kwa mambo haya yote, hakika nitaleta juu ya kichwa chako yale uliyotenda, asema Bwana Mungu Mwenyezi. Je, hukuongeza uasherati juu ya matendo yako mengine ya kuchukiza?
44 “ ‘Kila mtu anayetumia mithali atatumia mithali hii kukuhusu: “Alivyo mama, ndivyo alivyo bintiye.”
45 Wewe ni binti halisi wa mama yako, ambaye alimdharau mume wake na watoto wake; tena wewe ni dada halisi wa dada zako, waliowadharau waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
46 Dada yako mkubwa alikuwa Samaria, aliyeishi upande wako wa kaskazini na binti zake; naye dada yako mdogo, aliyeishi kusini mwako pamoja na binti zake, alikuwa Sodoma.
47 Hukuenda katika njia zao tu na kuiga matendo yao ya kuchukiza, bali baada ya muda mfupi, ulipotoka zaidi yao katika njia zako zote
48 Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mungu Mwenyezi, dada yako Sodoma pamoja na binti zake, kamwe hawakufanya yale ambayo wewe na binti zako mmefanya.
49 “ ‘Sasa hii ndiyo ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: yeye na binti zake walikuwa wenye kujigamba, walafi na wasiojali; hawakuwasaidia maskini na wahitaji.
50 Walijivuna na kufanya mambo ya kuchukiza sana mbele zangu. Kwa hiyo niliwakatilia mbali nami kama mlivyoona.
51 Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi ulizofanya. Wewe umefanya mambo mengi sana ya kuchukiza kuwaliko, nawe umewafanya dada zako waonekane kama wenye haki kwa ajili ya mambo haya yote uliyoyafanya.
52 Chukua aibu yako, kwa kuwa umefanya uovu wa dada zako uwe si kitu, nao waonekane kama wenye haki. Kwa kuwa dhambi zako zilikuwa mbaya kuliko zao, wameonekana wenye haki zaidi yako. Kwa hiyo basi, chukua aibu yako, kwa kuwa umewafanya dada zako waonekane wenye haki.
53 “ ‘Lakini nitarudisha baraka za Sodoma na binti zake na za Samaria na binti zake, nami nitarudisha baraka zako pamoja na zao,
54 ili upate kuchukua aibu yako na kufedheheka kwa ajili ya yote uliyotenda ambayo yamekuwa faraja kwao wakijilinganisha na wewe.
55 Nao dada zako, Sodoma na binti zake na Samaria na binti zake, watarudishwa kama vile walivyokuwa mwanzoni, nawe pamoja na binti zako mtarudishwa kama mlivyokuwa hapo awali.
56 Hukuweza hata kumtaja dada yako Sodoma kwa sababu ya dharau yako katika siku za kiburi chako,
57 kabla uovu wako haujafunuliwa. Hata hivyo, sasa unadhihakiwa na binti za Shamu na majirani zake wote, na binti za Wafilisti, wale wote wanaokuzunguka wanakudharau.
58 Utachukua matokeo ya uasherati wako na matendo yako ya kuchukiza, asema Mwenyezi Mungu.
59 “ ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: Nitakutendea kama unavyostahili, kwa kuwa umedharau kiapo changu kwa kuvunja agano.
60 Lakini nitakumbuka agano nililolifanya nawe wakati wa ujana wako, nami nitaweka nawe agano imara la milele.
61 Ndipo utakapozikumbuka njia zako na kuona aibu utakapowapokea dada zako, wale walio wakubwa wako na wadogo wako. Nitakupa hao wawe binti zako, lakini si katika msingi wa agano langu na wewe.
62 Hivyo nitalifanya imara agano langu na wewe, nawe utajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.
63 Basi, nitakapofanya upatanisho kwa ajili yako, kwa yale yote uliyoyatenda, utakumbuka na kuaibika, nawe kamwe hutafumbua tena kinywa chako kwa sababu ya aibu yako, asema Bwana Mungu Mwenyezi.’ ”
Перекрёстные ссылки
430
- 2Ezk 22:2, Ezk 20:4, Isa 58:1, Hos 8:1, Ezk 8:9–17, Ezk 33:7–9, Ezk 23:36
- 3Ezk 16:45, Isa 51:1–2, Deu 20:17, Jhn 8:44, Neh 9:7, Luk 3:7, Isa 1:10, Gen 15:16
- 4Hos 2:3, Jos 24:2, Deu 15:15, Gen 15:13, Exo 5:16–21, Exo 2:23–24, Act 7:6–7, Deu 5:6
- 5Deu 32:10, Num 19:16, Lam 4:3, Gen 21:10, Exo 1:22, Isa 49:15, Lam 2:19, Ezk 2:6
- 6Eph 2:4–5, Jhn 5:25, Tit 3:3–7, Act 7:34, Mat 5:13, Exo 19:4–6, Exo 2:24–25, Exo 3:7–8
- 7Deu 1:10, Exo 1:7, Isa 62:3, Ezk 16:10–13, Ezk 16:22, Psa 148:14, Psa 149:2–4, Hos 2:3
- 8Rut 3:9, Jer 2:2–3, Rom 5:8, Isa 43:4, Exo 32:13, 1Sa 12:22, Exo 19:4–8, Hos 11:1
- 9Psa 23:5, Rut 3:3, 1Jn 5:8, 1Jn 2:27, 1Co 6:11, Heb 9:10–14, Rev 1:5–6, Ezk 36:25
- 10Ezk 16:18, Ezk 16:13, Isa 61:10, Exo 26:36, Psa 45:13–14, Ezk 27:16, Exo 39:27–28, Exo 26:14
- 11Gen 24:22, Isa 3:19, Gen 24:47, Gen 41:42, Pro 1:9, Ezk 23:42, Num 31:50, Rev 4:10
- 12Isa 3:21, Isa 28:5
- 13Deu 32:13–14, Psa 50:2, 1Ki 4:21, Psa 48:2, Psa 45:13–14, Ezk 16:19, 1Sa 10:1, 2Sa 8:15
- 14Lam 2:15, 1Ki 10:24, 1Co 4:7, Deu 4:6–8, Jos 2:9–11, Deu 4:32–38, Jos 9:6–9, 2Ch 9:23
- 15Ezk 16:25, Jer 2:20, Isa 57:8, Jer 7:4, Ezk 23:3, Hos 1:2, Ezk 23:8, Isa 1:21
- 162Ki 23:7, 2Ch 28:24, Ezk 7:20, Hos 2:8
- 17Ezk 23:14–21, Jer 2:27–28, Ezk 7:19–20, Isa 57:7–8, Isa 44:19–20, Ezk 16:11, Hos 10:1, Hos 2:13
- 19Ezk 16:13, Deu 32:14–17, Gen 8:21, Hos 2:8–13
- 20Ezk 23:37, Psa 106:37–38, Exo 13:2, Ezk 20:31, Jer 7:31, Ezk 20:26, Ezk 23:39, Deu 29:11–12
- 212Ki 17:17, Jer 19:5, Lev 18:21, Deu 18:10, 2Ki 21:6, Psa 106:37, 2Ki 23:10, Lev 20:1–5
- 22Jer 2:2, Ezk 16:43, Hos 11:1, Hos 2:3, Ezk 16:3–7, Ezk 16:60–63
- 23Rev 12:12, Ezk 24:6, Ezk 2:10, Ezk 13:3, Rev 8:13, Zep 3:1, Jer 13:27, Mat 23:13–29
- 24Isa 57:7, Jer 2:20, Ezk 16:31, Psa 78:58, Ezk 16:39, Jer 3:2, Ezk 20:28–29, 2Ki 21:3–7
- 25Ezk 16:31, Jer 3:2, Ezk 16:15, Rev 17:12–13, Ezk 23:32, Ezk 23:9–10, Rev 17:1–5, Jer 6:15
- 26Ezk 23:19–21, Ezk 20:7–8, Ezk 8:14, Exo 32:4, Ezk 23:3, Jer 7:18–19, Ezk 23:8, Ezk 8:10
- 27Isa 9:12, Ezk 16:57, Ezk 16:37, Jer 34:21, 2Ki 24:2, Isa 9:17, Isa 3:1, Ezk 23:28–29
- 282Ki 16:7, Jer 2:36, Hos 10:6, Jer 2:18, 2Ki 16:10–18, 2Ch 28:23, 2Ch 28:16, Jdg 10:6
- 292Ki 21:9, Ezk 23:14–21, Ezk 13:14–23, Jdg 2:12–19
- 30Isa 1:3, Jer 3:3, Pro 9:13, Isa 3:9, Jer 4:22, Jer 2:12–13, Rev 17:1–6, Jdg 16:15–16
- 31Isa 52:3, Ezk 16:33–34, Hos 12:11, Ezk 16:24–25, Ezk 16:39
- 32Jer 2:28, Hos 2:2, Jer 3:8–9, Hos 3:1, Jer 3:20, Jer 2:25, Ezk 23:45, Ezk 23:37
- 33Isa 57:9, Hos 8:9–10, Isa 30:3, Isa 30:6–7, Hos 2:12, Jol 3:3, Gen 38:16–18, Luk 15:30
- 35Amo 7:16, Ezk 20:47, Ezk 34:7, Isa 1:10, Jer 3:6–8, Jhn 4:18, Isa 1:21, Jhn 4:10
- 36Ezk 23:10, Rev 3:18, Ezk 23:18, Gen 3:7, Jer 19:5, Ezk 16:15–22, Zep 3:1, Psa 139:11–12
- 37Jer 13:22, Hos 2:3, Hos 2:10, Lam 1:8, Nam 3:5–6, Hos 8:10, Jer 13:26, Rev 17:16
- 38Gen 9:6, Lev 20:10, Jer 18:21, Zep 1:17, Ezk 16:20–21, Rev 16:6, Jhn 8:3–5, Deu 22:22–24
- 39Hos 2:3, Ezk 23:26, Ezk 16:24–25, Ezk 23:29, Isa 27:9, Ezk 7:22–24, Ezk 16:10–20, Ezk 16:31
- 40Ezk 23:47, Hab 1:6–10, Ezk 24:21, Jer 25:9, Ezk 23:10, Jhn 8:5–7
- 41Ezk 23:48, Jer 39:8, 2Ki 25:9, Jer 52:13, Ezk 23:27, Ezk 5:8, Deu 13:16, Ezk 23:10
- 42Ezk 5:13, Ezk 21:17, Ezk 39:29, Isa 40:1–2, Zec 6:8, Isa 54:9–10, 2Sa 21:14, Isa 1:24
- 43Ezk 16:22, Psa 78:42, Ezk 22:31, Ezk 11:21, Isa 63:10, Psa 106:13, Ezk 6:9, Jer 2:32
- 44Ezk 18:2–3, 1Sa 24:13, Psa 106:35–38, Ezk 16:3, Ezr 9:1, 2Ki 21:9, 2Ki 17:15, 1Ki 21:16
- 45Isa 1:4, Zec 11:8, Ezk 23:37–39, Ezk 16:15, Rom 1:30–31, Deu 12:31, Ezk 16:8, Ezk 23:2
- 46Ezk 23:4, Ezk 16:61, Ezk 16:48–49, Gen 13:10–13, Jer 3:8–11, Ezk 16:51, Ezk 16:53–56, Jud 1:7
- 472Ki 21:9, Ezk 5:6–7, Ezk 16:48, Ezk 16:51, 1Ki 16:31, Jhn 15:21–22, 2Ki 21:16, 1Co 5:1
- 48Mat 10:15, Act 7:52, Mrk 6:11, Mat 11:23–24, Luk 10:12
- 49Gen 13:10, Ezk 28:2, Psa 138:6, Luk 12:16–20, Ezk 18:12, Dan 5:23, Ezk 18:16, Pro 18:12
- 50Gen 18:20, Gen 13:13, Gen 19:5, Gen 19:24, Rom 1:26–27, Pro 18:12, Job 18:15, Isa 13:19
- 51Jer 3:8–11, Rom 3:9–20, Luk 12:47–48, Mat 12:41–42
- 52Mat 7:1–5, Jer 23:40, Ezk 44:13, Gen 38:26, Ezk 16:56, Rom 2:26–27, Rom 2:10, Rom 6:21
- 53Jer 12:16, Ezk 39:25, Isa 19:24–25, Ezk 29:14, Psa 14:7, Jer 49:39, Psa 126:1, Jer 20:16
- 54Ezk 14:22–23, Jer 2:26, Ezk 16:52, Ezk 16:63, Ezk 36:31–32
- 55Ezk 36:11, Ezk 16:53, Mal 3:4
- 56Isa 65:5, Zep 3:11, Luk 18:11, Luk 15:28–30
- 572Ki 16:5–7, 2Ch 28:18–23, 2Ch 28:5–6, Isa 7:1, Ezk 16:36–37, Hos 2:10, Num 23:7, Hos 7:1
- 58Ezk 23:49, Gen 4:13, Lam 5:7
- 59Isa 24:5, Ezk 17:19, Exo 24:1–8, Rom 2:8–9, Ezk 14:4, Deu 29:10–15, Jer 31:32, Ezk 7:8–9
- 60Hos 2:19–20, Jer 50:5, Heb 12:24, Heb 8:10, Ezk 16:8, Jer 31:31–34, Lev 26:42, Isa 55:3
- 61Gal 4:26–31, Heb 8:13, Eph 3:6, Rom 15:16, Isa 66:7–12, Ezk 20:43, Rom 11:11, Jer 50:4–5
- 62Jer 24:7, Ezk 6:7, Ezk 16:60, Jol 3:17, Hos 2:18–23, Ezk 20:43–44, Ezk 20:37, Ezk 39:22
- 63Rom 3:19, Psa 39:9, Tit 3:3–7, Job 40:4–5, Dan 9:7–8, Ezk 36:31–32, Rom 2:1, Ezk 16:61
Темы в этой главе
59
Ablution, Adultery, Backsliders, Badger, Beauty, Blessing, Blood, Bracelet, Bride, Bridegroom, Children, Church, Covenant, Crown, Depravity of Man, Embroidery, Ezekiel, Falsehood, Food, God, Gold, High Places, Humility, Idleness, Idolatry, Ingratitude, Israel, Prophecies Concerning, Jealousy, Jewels, Judgment, Lasciviousness, Linen, Lukewarmness, Marriage, Midwifery, Molech, Navel, Nose, Obstetrics, Offerings, Oil, Parents, Poor, Pride, Prophecy, Proverbs, Punishment, Regeneration, Repentance, Sanitation, Shoe, Silk, Sin, Sodom, Swaddle, Symbols and Similitudes, Whoredom, Wicked (People), Women